Jipu-bishi
Senior Member
- Feb 16, 2016
- 107
- 102
Dr. John Pombe Magufuli ni kama Dr. Nkwame Nkurumah kiutendaji.... Wewe unasemaje?
Kama alivyo JPM Dr.Nkwame alikuwa mwalimu msomi sana na alipata PhD yake kutoka University of Pennslvania sasa UPenn (One of the best Universities in the World). Kama alivyo JPM Uzalendo wa Nkurumah ulikuwa mkubwa sana, akiwa masomoni US alianza kueneza vuguvugu la ukombozi barani afrika. Wazungu hawakumpenda, na hasa Wamarekani.
Kwa Rais wetu JPM, ni mzalendo ambaye ameanzisha vuguvugu la Ukombozi wa mara ya pili kuwatoa Watanzania kutoka kwenye mikono ya Wakoloni weusi wanaosadikiwa kuwa wabaya na wakatili kuliko Wajerumani
Mwalimu Nkurumah aliondoka Ghana akiwa kijana mdogo kwenda US kusoma Chuo Kikuu cha Lincoln katika jimbo la Pennyslvania baadaya ya masomo ya miaka kumi Dr. Nkurumah aliondoka US Kwenda London UK kusoma laws na kufanya Thesis ya PhD yake. Huko London alikutana na mwanamapinduzi George Padmore Kijana Mtrinidad aliyehamia London kutoka US, kwa pamoja wakaandaa Pan African Congress kwenye mji wa Manchester 1945, hapo wakakutana na akina Marcus Garvey, Mjamaica wanamapinduzi, William Edward Burghardt Du Bois, Booker T Washingyon Wamerikani mweusi wanatema cheche ya ukombozi wakatengeneza bond na kuamua kuwa muda wa Africa kupata uhuru ni sasa na Nkurumah akatumwa arudi Gold Coast(Ghana ya sasa) kuwasaidia Africa ipate uhuru wao wakarudi makwao kuanzisha sokomoko la Usawa (civil right movement) Historia haijasema kama Mwalimu alikuwa anafahamu hii movement kwa wakati huu lakini kwa chronological events, Mwalimu alikuwa Tabora boys kabla ya kwenda Makerere.
Hawa watu walikuwa na Uchungu sana, ninapomwona Rais Magufuli akikutana na Akina Paul Kagame, rais ambaye ameamua kutengeneza nchi iliyopasuka vipande na kuifanya Rwanda ya kutamani, ni Uzalendo wa Hali ya Juu sana. Rais wetu ana uchungu mkubwa sana na wananchi wake anataka kutengeneza alliance ambayo haiwaibii wala kuchukua kutoka kwa wananchi wake bali kuongeza kwenye hazina yao na ukiangalia Paul Kagame anafanya hayo kati ya Marais wanaotuzunguka Tanzania.
Mwaka 1947, Dr. Nkurumah alifunga virago akarudi Ghana akakuta kuna vyama vya upinzani tayari, UGCC wakafanya kama CHADEMA, wakamkaribisha na kumpa ukatibu mkuu, sasa Mwenyekiti anaelimu ya Kwa baba paroko na Katibu Mkuu ana PhD mtaelewana lini? Akaanzisha harakati za Uhuru chini ya msukosuko mkubwa wa Mwingereza ambapo viongozi wote wa UGCC wakaswekwa ndani, viongozi wenzie wakasema kaa isiwe tabu wakamfukuza akahama chama na kuanzisha CPP chama kipya.
Mwaka 1950 miezi michache kabla ya uchaguzi akakamatwa akawekwa rokap lakini sauti ya Watu sauti ya Mungu uchaguzi ulipofika alipigiwa Kura akiwa gerezani kwa asilimia zaidi ya Tisini, Governor akamtoa ili aanzishe serikali akiwa Waziri Mkuu, uchaguzi uliofuata 1956 akashinda tena, na this time akatangaza Uhuru wa Ghana 1957 Marcha 6.
Uzalendo wa Nkurumah haukishia kwenye kuta za gereza zilinguruma ndani na nje ya gereza kwa sauti kubwa kuliko vipaza sauti zote nchini. kumweka ndani mpigania haki ni sawa na kumpa promo, na kumsogeza karibu na media
Baada ya Dr Nkurumah kupata Uhuru na kuwa Rais kamili, akawa na ndoto ya kuiunganisha Afrika na kuwa Rais wa kwanza wa United States of Africa. Ndoto ya Nkurumah ya kuwaunganisha waafrika ukawa mkubwa, lakini akawasahau Waghana, akaanza kutaka kuwa Rais wa Waafrika akaacha Urais wa Ghana, akaanza kutoa misaada ya Kifedha Guinea na Bukina Faso akawaacha wananchi wa Ghana wakitaabika kwa njaa.
Rais Kipenzi akaanza kupoteza imani kutoka kwa wananchi wake, na baya zaidi akaanzisha a Single Party State, akanyoosha fimbo ya Dola akaanza kuwabana wapinzani waliomkaribisha mwanzoni kwa kuwafunga magerezani na hakuna aliyesema kitu.
Kila sheria aliyotaka kupitisha ilipita Bungeni bila pingamizi, Wapinzani walifukuzwa Bungeni na kuanza kuandamwa na polisi kila kona, kesi kila mahakama, marufuku kila kitu walichotia mikononi, akawa rais kweli kweli.
Katika kipindi hiki wananchi waliendelea kutaabika. Dr. Nkurumah alikoswa kuawa mara tano katika kipindi kifupi sana. Waghana wakatamani utawala wa Wazungu, maisha yakawa magumu kupindukia, uchumi ukaharibika sana Na baya Zaidi akaamua kuchukua pesa za walipakodi Ghana akampa Rafiki yake Sekou Toure wa Guinea ili arekebishe uchumi wa nchi yake.
Alikoishia Mungu ndo anajua hata mke wake hajui. Rais wangu, usjisahau, Urais ni sawa n kuwa Mganga wa Kienyeji na Mchungaji kwa wakati moja, ikibidi unaloga, na ikibidi unawekea mikono. Wapinzani wako ni ndugu zako na zaidi ya yote wanauwezo wa kukuchonganisha na wananchi wako kirahisi sana, heri upoteze support ya watu wako wa karibu Ikulu lakini usipoteze support ya wananchi wako.
Simama katikati mkutane kati, sijui kilichotokea Ghana baada ya hapo lakini ninajchojua History has nothing to do with the Future but it give an indication of what the future is going to be. " wote tunajua siku alipopinduliwa wananchi walicheza na kunywa usiku kucha "Where did beloved son of Africa go wrong"
Lets have an open converstion my fellow Africans.
Thanks
Jipubishi
Kama alivyo JPM Dr.Nkwame alikuwa mwalimu msomi sana na alipata PhD yake kutoka University of Pennslvania sasa UPenn (One of the best Universities in the World). Kama alivyo JPM Uzalendo wa Nkurumah ulikuwa mkubwa sana, akiwa masomoni US alianza kueneza vuguvugu la ukombozi barani afrika. Wazungu hawakumpenda, na hasa Wamarekani.
Kwa Rais wetu JPM, ni mzalendo ambaye ameanzisha vuguvugu la Ukombozi wa mara ya pili kuwatoa Watanzania kutoka kwenye mikono ya Wakoloni weusi wanaosadikiwa kuwa wabaya na wakatili kuliko Wajerumani
Mwalimu Nkurumah aliondoka Ghana akiwa kijana mdogo kwenda US kusoma Chuo Kikuu cha Lincoln katika jimbo la Pennyslvania baadaya ya masomo ya miaka kumi Dr. Nkurumah aliondoka US Kwenda London UK kusoma laws na kufanya Thesis ya PhD yake. Huko London alikutana na mwanamapinduzi George Padmore Kijana Mtrinidad aliyehamia London kutoka US, kwa pamoja wakaandaa Pan African Congress kwenye mji wa Manchester 1945, hapo wakakutana na akina Marcus Garvey, Mjamaica wanamapinduzi, William Edward Burghardt Du Bois, Booker T Washingyon Wamerikani mweusi wanatema cheche ya ukombozi wakatengeneza bond na kuamua kuwa muda wa Africa kupata uhuru ni sasa na Nkurumah akatumwa arudi Gold Coast(Ghana ya sasa) kuwasaidia Africa ipate uhuru wao wakarudi makwao kuanzisha sokomoko la Usawa (civil right movement) Historia haijasema kama Mwalimu alikuwa anafahamu hii movement kwa wakati huu lakini kwa chronological events, Mwalimu alikuwa Tabora boys kabla ya kwenda Makerere.
Hawa watu walikuwa na Uchungu sana, ninapomwona Rais Magufuli akikutana na Akina Paul Kagame, rais ambaye ameamua kutengeneza nchi iliyopasuka vipande na kuifanya Rwanda ya kutamani, ni Uzalendo wa Hali ya Juu sana. Rais wetu ana uchungu mkubwa sana na wananchi wake anataka kutengeneza alliance ambayo haiwaibii wala kuchukua kutoka kwa wananchi wake bali kuongeza kwenye hazina yao na ukiangalia Paul Kagame anafanya hayo kati ya Marais wanaotuzunguka Tanzania.
Mwaka 1947, Dr. Nkurumah alifunga virago akarudi Ghana akakuta kuna vyama vya upinzani tayari, UGCC wakafanya kama CHADEMA, wakamkaribisha na kumpa ukatibu mkuu, sasa Mwenyekiti anaelimu ya Kwa baba paroko na Katibu Mkuu ana PhD mtaelewana lini? Akaanzisha harakati za Uhuru chini ya msukosuko mkubwa wa Mwingereza ambapo viongozi wote wa UGCC wakaswekwa ndani, viongozi wenzie wakasema kaa isiwe tabu wakamfukuza akahama chama na kuanzisha CPP chama kipya.
Mwaka 1950 miezi michache kabla ya uchaguzi akakamatwa akawekwa rokap lakini sauti ya Watu sauti ya Mungu uchaguzi ulipofika alipigiwa Kura akiwa gerezani kwa asilimia zaidi ya Tisini, Governor akamtoa ili aanzishe serikali akiwa Waziri Mkuu, uchaguzi uliofuata 1956 akashinda tena, na this time akatangaza Uhuru wa Ghana 1957 Marcha 6.
Uzalendo wa Nkurumah haukishia kwenye kuta za gereza zilinguruma ndani na nje ya gereza kwa sauti kubwa kuliko vipaza sauti zote nchini. kumweka ndani mpigania haki ni sawa na kumpa promo, na kumsogeza karibu na media
Baada ya Dr Nkurumah kupata Uhuru na kuwa Rais kamili, akawa na ndoto ya kuiunganisha Afrika na kuwa Rais wa kwanza wa United States of Africa. Ndoto ya Nkurumah ya kuwaunganisha waafrika ukawa mkubwa, lakini akawasahau Waghana, akaanza kutaka kuwa Rais wa Waafrika akaacha Urais wa Ghana, akaanza kutoa misaada ya Kifedha Guinea na Bukina Faso akawaacha wananchi wa Ghana wakitaabika kwa njaa.
Rais Kipenzi akaanza kupoteza imani kutoka kwa wananchi wake, na baya zaidi akaanzisha a Single Party State, akanyoosha fimbo ya Dola akaanza kuwabana wapinzani waliomkaribisha mwanzoni kwa kuwafunga magerezani na hakuna aliyesema kitu.
Kila sheria aliyotaka kupitisha ilipita Bungeni bila pingamizi, Wapinzani walifukuzwa Bungeni na kuanza kuandamwa na polisi kila kona, kesi kila mahakama, marufuku kila kitu walichotia mikononi, akawa rais kweli kweli.
Katika kipindi hiki wananchi waliendelea kutaabika. Dr. Nkurumah alikoswa kuawa mara tano katika kipindi kifupi sana. Waghana wakatamani utawala wa Wazungu, maisha yakawa magumu kupindukia, uchumi ukaharibika sana Na baya Zaidi akaamua kuchukua pesa za walipakodi Ghana akampa Rafiki yake Sekou Toure wa Guinea ili arekebishe uchumi wa nchi yake.
Alikoishia Mungu ndo anajua hata mke wake hajui. Rais wangu, usjisahau, Urais ni sawa n kuwa Mganga wa Kienyeji na Mchungaji kwa wakati moja, ikibidi unaloga, na ikibidi unawekea mikono. Wapinzani wako ni ndugu zako na zaidi ya yote wanauwezo wa kukuchonganisha na wananchi wako kirahisi sana, heri upoteze support ya watu wako wa karibu Ikulu lakini usipoteze support ya wananchi wako.
Simama katikati mkutane kati, sijui kilichotokea Ghana baada ya hapo lakini ninajchojua History has nothing to do with the Future but it give an indication of what the future is going to be. " wote tunajua siku alipopinduliwa wananchi walicheza na kunywa usiku kucha "Where did beloved son of Africa go wrong"
Lets have an open converstion my fellow Africans.
Thanks
Jipubishi