Dr am 4 real PhD
JF-Expert Member
- Jun 30, 2016
- 6,019
- 11,024
Nimeku quote.....Katika marais walioiharibu nchi ni magu...
Ameshindwa kuifanya serikali iwe inapelekewa kodi na wafanyabiashara matokeo yake serikali ndio inafuata kodi.
Moja ya eneo ambalo anafanya kosa kubwa sana ni kujenga uadui na wafanyabiashara huku akijua ndio sekta muhimu sana kwa taifa, kila siku anabuni mbinu za kuinyonya badala kuisaidia izidi kukua
Mfano sasa hivi wametakiwa kuweka barcord kwenye risiti za mashine ya EFD na gharama yake ni laki na nusu si wizi kabisa huu?
Umezungumza habari ya wamachinga, hawa wapo kwa kazi rasmi ya kuua wafanyabiashara wakubwa na ni mpango mkakati maalumu na wala usitarajie waondolewe awamu hii,
Ndio maana wao hawalipi kodi zaidi ya kitambulisho tu haijalishi ana mtaji mkubwa kiasi gani, wala hawatakiwi kutoa risiti wakati sheria inasema risiti inatolewa kuanzia bidhaa ya sh 500,
Akikamatwa mwenye duka hajatoa risiti hata ya 1000 faini milioni 3 mmachinga hata auze bidhaa ya laki haina shida,
Mwenye duka analipa kodi lukuki
1)kodi ya mapato,
2)leseni ya biashara,
3)huduma ya jiji (service leavy)
4)mkataba wa frem au stoo nao unalipiwa kodi.
5)fire extingisher
6)huduma za taka
7)kodi ya frem na stoo kama anayo
Mmachinga hapo analipa elfu 20 kamaliza kazi.
Biashara za maduka nchini zimedorora sana, yaani mfanyabiashara serikali hii anadharauliwa sana hasikilizwi tena yaani kifupi ni adui wa serikali.
Ukiona tawi ya benk kubwa kama NMB kkoo senta tangu lifunguliwe 2012 wanatoa huduma hadi siku za jumapili lakini sasa hivi hawafungui ujue kuna shida pamoja maduka ya kuabadili fedha kufungwa watu wanabadilisha bank lkn bank zinafungwa,
Ukiona bank zinafunga matawi yao katikati ya mji kama kkoo ujue ipo shida mahali tena kubwa sana.
Kuna mengi ya unyanyasaji wa wafanyabiashara tunayajua lakini siwezi kuyaandika hapa sababu sasa hivi jf ni kama fb haina uhuru tena nisije kupelekwa kusikojulikana.
Kwa mkakati wake huu wala hatushangai maana alishasema mapemaaa "WAFANYABIASHARA NA MATAJIRI WATAISHI KAMA MASHETANI"
Kwa hiyo kwa mfumo huu ni kusubiri tu atoke madarakani hakuna namna, mfumo wake wa kiuongozi hauzoeleki wala haiwezekani kwenda nae sawa ndio maana hata viongozi wenzake wanamuogopa sio kumuheshimu.
"Mwenye duka analipa kodi lukuki
1)kodi ya mapato,
2)leseni ya biashara,
3)huduma ya jiji (service leavy)
4)mkataba wa frem au stoo nao unalipiwa kodi.
5)fire extingisher
6)huduma za taka
7)kodi ya frem na stoo kama anayo
Mmachinga hapo analipa elfu 20 kamaliza kazi"
Umepiga Sana spana