Maoni: Baraza la Mawaziri lifanye kazi ya ushauri sawa sawa, Rais hakutakiwa kwenda bandarini

iparamasa

JF-Expert Member
Nov 14, 2013
13,438
14,916
Kuna baadhi ya mambo ukiyaona yanatia haya moyoni, kuna baadhi ya mambo Serikali inajiumbua yenyewe na kujiaibisha, mfano mzuri ni pale Bandarini
haya mambo yalitakiwa yamalizikie ofisini.

Rais amwite waziri anayehusika na bandari, amwite Mkuu wa Bandari pamoja na watendaji wote, amwite Mkuu wa Taasisi ya vipimo kuhusu masuala ya mita, awahoji akiwa na kamati yake inayomshauri kuhusu hayo (kamati hiyo iwe well informed na ihusishe watu wa sekta binafsi na umma kila mmoja imshauri kwa wakati tofauti).

Baada ya kuhojiana nao labda angejua kwa nini flow meter za mafuta hazijafungwa na kwa nini mashine za ukaguzi ziko chache, pili rais aweke maeneo nyeti kiuchumi ambayo yatatakiwa kutoa taarifa kwake kila mwezi au wiki mbili. Nne, rais ashauriwe kuhusu baadhi ya sekta ambazo zinaweza kuupeleka uchumi mbele kwa haraka na mgawanyo mkubwa ki nchi hivyo kuupeleka uchumi mbele, mfano utalii, kisiwa cha Rubondo kina uwezo wa kuwavuta watalii Geita na Burigi na hata Bukoba, cha msingi ni uwekezaji tu.

Kile kisiwa ukifanyika uwekezaji, pamoja na visiwa vyote vya ziwa Viktoria, Nyasa, Tanganyika, Bahari ya Hindi tutapata hela nyingi za kigeni, utalii unalipa sana na baraza la mawaziri limwambie rais hivyo.

Tuna haja ya kupanua mawazo kuhusu kusogeza nchi mbele. Sasa tunahangaika na vitambulisho lukuki vya nchi. Makampuni ya simu yamejitahidi kututoa kwenye mabunda ya noti. Tulitaraji vitambulisho vya taifa vituwezeshe kununua bia baa, tiketi ya ndege kwa kuwa na programu maalum ya kielektroniki inayowezesha kuhifadhi taarifa kadha wa kadha ikiwemo TIN number.
 
Ni nchi gani hapa duniani vitambulisho vya Taifa vinanunuwa bia bar?

Hivi wewe una viwango vya kutowa ushauri au ni wakushauriwa pia?
 
nina imani visiwa hivi hatuvitendei haki,serikali iteue baadhi ya visiwa(viwe vingi) ivipime,itangaze tenda ya kuvikodisha kwa wawekezaji wa kimataifa kwa muda fulani kwa kodi nzuri,mkataba huo uwalazimishe wawekeze hoteli za kisasa kabla visiwa hivyo havijavamiwa na wananchi hasa wavuvi,
bandari isimpe rais presha,mambo ya kuipa nchi faida ni mengi mno,anaweza kutenga maeneo ya bandari mapya ziwa victoria,bahari ya hindi.
 
Ni nchi gani hapa duniani vitambulisho vya Taifa vinanunuwa bia bar?

Hivi wewe una viwango vya kutowa ushauri au ni wakushauriwa pia?
namaanisha sio mpaka uwe na simu ndipo ulipe kwa mpesa au tigo pesa,programe inawekwa ya kielekroniki inayokufanya uchague kwamba una akaunti ya mpesa au tigo pesa,unaijaza hela ukienda kulipia kaunta unaswap tu,but unakuwa umeiweka salio
 
Tatizo washauri wenyewe wanafiki.....
Kama washauri ndio wakina Mpango ambao wamegeuka kuwa wanafiki unategemea nn??
 
Mkuu hiyo inaitwa MBWA management by walking around. Sometimes you need to do that to ensure things are in order and thats how their supposed to be. JPM ana speed anatembea nayo inawezekana hao ulio wataja they don't match it.
tunasubiri amtembelee afisa kilimo wa kijiji huku mpitimbwi,akitoka aende muleba,tarime,mererani mgodini
 
namaanisha sio mpaka uwe na simu ndipo ulipe kwa mpesa au tigo pesa,programe inawekwa ya kielekroniki inayokufanya uchague kwamba una akaunti ya mpesa au tigo pesa,unaijaza hela ukienda kulipia kaunta unaswap tu,but unakuwa umeiweka salio
Hebu acha kukurupuka una uelewa wowote wa Viza card na Debit card?

Wewe ndio huna.
 
Hebu acha kukurupuka una uelewa wowote wa Viza card na Debit card?

Wewe ndio huna.
kwa hiyo unamshangaa angela kairuki anapoingiza mpaka taarifa za vyeti vya watumishi na mengineyo?
akili yako imeganda,hovyo kabisa
 
Mkuu hiyo inaitwa MBWA management by walking around. Sometimes you need to do that to ensure things are in order and thats how their supposed to be. JPM ana speed anatembea nayo inawezekana hao ulio wataja they don't match it.
Nakuunga mkono kabisa Mr Jicho. Hizo style anazopendekeza Bw Iparamasa ndio zimeifikisha hii nchi hapa tulipo. Wacha watu waumbuliwe. Mambo ya kubembelezana kwa kweli hapana. Management za kistaarabu/heshima NO! Afterall kwa miaka lukuki Watanzania tumefichwa mengi. Unakutana na viongozi unawatetemikia unawapa heshima kumbe ni mabomu ya kutuangamiza. JPM Hivyo hivyo.
 
Nakuunga mkono kabisa Mr Jicho. Hizo style anazopendekeza Bw Iparamasa ndio zimeifikisha hii nchi hapa tulipo. Wacha watu waumbuliwe. Mambo ya kubembelezana kwa kweli hapana. Management za kistaarabu/heshima NO! Afterall kwa miaka lukuki Watanzania tumefichwa mengi. Unakutana na viongozi unawatetemikia unawapa heshima kumbe ni mabomu ya kutuangamiza. JPM Hivyo hivyo.
hao watu mnaosema wanaumbuliwa,walipewa hela za kununua vifaa wakakataa?
 
Mkuu iparamasa kwa hali ya Bandari iliyopokuwa imefika, mwache Rais afanye anayoyafanya.. maana sasa ni 'full' kudanganyana, hakuna utelezaji, watu hawawajibiki,ubunifu 'zero' n.k.
  • Kweli ilihitaji Rais kuwaambia Maafisa wa Bandari katika ukaguzi wa mizigo kuwa na Ofisi yenye vioo ili kuona ni gari linalokaguliwa 'physically'?
  • Kweli ilihitaji Rais kwenda kuwaelekeza nini cha kufanya ili 'flow meters' za kupimia mafuta ziweze kufanya kazi?
  • Kweli ilihitaji Rais kwenda Bandarini ili kuwaelekeza Menejimenti ya Bandari namna ya kutumia 'Capex Budget' ili kununua 'scanner'?
  • Kweli ilihitaji Rais kwenda Bandarini ili kugundua upokeaji usio na uwiano wa mizigo ('asymetrical allocation') kati ya TPA na TICTS?
  • Kweli ilihitaji Rais kwenda Bandarini ili kuweza kutambua kuwa Mkataba kati ya TPA na TICTS una walakini na unahitaji kurejewa upya?
Kama Rais anapokanyaga sehemu na majibu na masuluhisho yanapatikana, acheni aende..
Mimi nashauri ni wakati sasa kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano na Katibu Mkuu wake, Waziri wa Fedha na Mipango na Katibu Mkuu wake, Kamishna Mkuu wa TRA, Mtendaji Mkuu wa TEMESA n.k kuhamishia Ofisi zao Bandarini mpaka hali itakapotengamaa..
Kwa wastani Customs & Excise kwa bandari bila JKNI ni zaidi ya asilimia 87 ya mapato yote ya kodi ya ushuru na forodha ya nchi na Customs & Excise inatoa asilimia 41 ya mapato yote ya nchi ya kodi - mengine yanatoka kwa Large Taxpayers 41% na Domestic Revenue 18%. Hizi ni data za mwaka 2015/16.
Naona hapa umuhimu wa bandari kama 'Life Line' ya nchi inaonekana..
 
tunasubiri amtembelee afisa kilimo wa kijiji huku mpitimbwi,akitoka aende muleba,tarime,mererani mgodini
Mkuu I'm neither a politician nor a member of any political part mm Ni mwananchi kwenye utashi wangu Rais anapofanya mambo mazuri kwa nn tusiunge mkono? Na anapokosea pia tunakosoa. Nadhani JPM siyo mwehu kuamua kwenda bandarini Na asiende kwa Afisa Kilimo naona Kama mifano yako uliyo toa haina mashiko
 
Nakuunga mkono kabisa Mr Jicho. Hizo style anazopendekeza Bw Iparamasa ndio zimeifikisha hii nchi hapa tulipo. Wacha watu waumbuliwe. Mambo ya kubembelezana kwa kweli hapana. Management za kistaarabu/heshima NO! Afterall kwa miaka lukuki Watanzania tumefichwa mengi. Unakutana na viongozi unawatetemikia unawapa heshima kumbe ni mabomu ya kutuangamiza. JPM Hivyo hivyo.

Lakini wale wa FLOW METERS waliunbuliwa tangu mwezi february na amri ikatolewa zifungwe, miezi minane hadi jana HOLAAAA!!!

Hivi hatuoni kuna tatizo la msingi kabisa liko sehemu?

Mleta hoja wala hajasema MBWA isitumiwe na Rais, lakini anapaswa kwenda sehemu akiwa yuko informed pamoja na hatua za kuchukua!!

Ni nini alifanya jana zaidi ya kupandwa na jazba tu? Maana yake mpaka arudi ofisini, wajadiliane ndiyo wajue tatizo na kisha hatua za kuchukua!!

I think this is what is meant by the Author...!!
 
Mkuu iparamasa kwa hali ya Bandari iliyopokuwa imefika, mwache Rais afanye anayoyafanya.. maana sasa ni 'full' kudanganyana, hakuna utelezaji, watu hawawajibiki,ubunifu 'zero' n.k.
  • Kweli ilihitaji Rais kuwaambia Maafisa wa Bandari katika ukaguzi wa mizigo kuwa na Ofisi yenye vioo ili kuona ni gari linalokaguliwa 'physically'?
  • Kweli ilihitaji Rais kwenda kuwaelekeza nini cha kufanya ili 'flow meters' za kupimia mafuta ziweze kufanya kazi?
  • Kweli ilihitaji Rais kwenda Bandarini ili kuwaelekeza Menejimenti ya Bandari namna ya kutumia 'Capex Budget' ili kununua 'scanner'?
  • Kweli ilihitaji Rais kwenda Bandarini ili kugundua upokeaji usio na uwiano wa mizigo ('asymetrical allocation') kati ya TPA na TICTS?
  • Kweli ilihitaji Rais kwenda Bandarini ili kuweza kutambua kuwa Mkataba kati ya TPA na TICTS una walakini na unahitaji kurejewa upya?
Kama Rais anapokanyaga sehemu na majibu na masuluhisho yanapatikana, acheni aende..
Mimi nashauri ni wakati sasa kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano na Katibu Mkuu wake, Waziri wa Fedha na Mipango na Katibu Mkuu wake, Kamishna Mkuu wa TRA, Mtendaji Mkuu wa TEMESA n.k kuhamishia Ofisi zao Bandarini mpaka hali itakapotengamaa..
Kwa wastani Customs & Excise kwa bandari bila JKNI ni zaidi ya asilimia 87 ya mapato yote ya kodi ya ushuru na forodha ya nchi na Customs & Excise inatoa asilimia 41 ya mapato yote ya nchi ya kodi - mengine yanatoka kwa Large Taxpayers 41% na Domestic Revenue 18%. Hizi ni data za mwaka 2015/16.
Naona hapa umuhimu wa bandari kama 'Life Line' ya nchi inaonekana..
tushughulike na mfumo au matukio?
crisis ya bandari(kama kweli ipo)ipo tangu mwaka jana mwishoni,si bora iundwe technical commitee itakayoshughulika na mfumo?
Bodi ya wakurugenzi ina kazi gani?
waziri ana kazi gani?
katibu mkuu?
Je ishu inayofanya mapato yashuke ni hiyo?
 
Mkuu iparamasa kwa hali ya Bandari iliyopokuwa imefika, mwache Rais afanye anayoyafanya.. maana sasa ni 'full' kudanganyana, hakuna utelezaji, watu hawawajibiki,ubunifu 'zero' n.k.
  • Kweli ilihitaji Rais kuwaambia Maafisa wa Bandari katika ukaguzi wa mizigo kuwa na Ofisi yenye vioo ili kuona ni gari linalokaguliwa 'physically'?
  • Kweli ilihitaji Rais kwenda kuwaelekeza nini cha kufanya ili 'flow meters' za kupimia mafuta ziweze kufanya kazi?
  • Kweli ilihitaji Rais kwenda Bandarini ili kuwaelekeza Menejimenti ya Bandari namna ya kutumia 'Capex Budget' ili kununua 'scanner'?
  • Kweli ilihitaji Rais kwenda Bandarini ili kugundua upokeaji usio na uwiano wa mizigo ('asymetrical allocation') kati ya TPA na TICTS?
  • Kweli ilihitaji Rais kwenda Bandarini ili kuweza kutambua kuwa Mkataba kati ya TPA na TICTS una walakini na unahitaji kurejewa upya?
Kama Rais anapokanyaga sehemu na majibu na masuluhisho yanapatikana, acheni aende..
Mimi nashauri ni wakati sasa kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano na Katibu Mkuu wake, Waziri wa Fedha na Mipango na Katibu Mkuu wake, Kamishna Mkuu wa TRA, Mtendaji Mkuu wa TEMESA n.k kuhamishia Ofisi zao Bandarini mpaka hali itakapotengamaa..
Kwa wastani Customs & Excise kwa bandari bila JKNI ni zaidi ya asilimia 87 ya mapato yote ya kodi ya ushuru na forodha ya nchi na Customs & Excise inatoa asilimia 41 ya mapato yote ya nchi ya kodi - mengine yanatoka kwa Large Taxpayers 41% na Domestic Revenue 18%. Hizi ni data za mwaka 2015/16.
Naona hapa umuhimu wa bandari kama 'Life Line' ya nchi inaonekana..

Mkuu, umenena vema kabisa na upo 100% sawa.

Ila tatizo kubwa ambalo watu wengi tumeliona ni elimu.

Ni watanzania wengi sana wenye vyeti vya kughushi wamepata kazi bandarini na sasa ni wakati wa kuwa-flush out.

Ni bora TPA inawasomeshe wale wafanyakazi waliopo wenye vyeti halisi na pia kuwavutia watanzania ambao wana sifa za uendeshaji bandari.

Hili liwe zoezi kwa bandari zote za nchi hii ambazo ndizo nguzo kuu ya maingizo ya fedha.

Hapa sizungumzii clearing & Forwarding bali nazungumzia watu wenye utaalam wa shipping management, maana nna uhakika kuna wafanyakazi pale TPA hawafahamu hata kutumia office packages kwenye kompyuta na wamewekwa pale kwa memo.

TPA ni mlango mkubwa sana wa maingizo ya mapato kwa serikali maana biashara zote za kimataifa zinatuletea fedha kupitia mizigo.
 
Lakini wale wa FLOW METERS waliunbuliwa tangu mwezi february na amri ikatolewa zifungwe, miezi minane hadi jana HOLAAAA!!!

Hivi hatuoni kuna tatizo la msingi kabisa liko sehemu?

Mleta hoja wala hajasema MBWA isitumiwe na Rais, lakini anapaswa kwenda sehemu akiwa yuko informed pamoja na hatua za kuchukua!!

Ni nini alifanya jana zaidi ya kupandwa na jazba tu? Maana yake mpaka arudi ofisini, wajadiliane ndiyo wajue tatizo na kisha hatua za kuchukua!!

I think this is what is meant by the Author...!!
kuna clip moja nafikiri ilihusu mtu wa flow meter....nafikiri alikuwa anasema waliomba hela,sijui hajapewa na serikali!!I.e za kufunga mita/kurekebisha
 
Back
Top Bottom