BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,792
- 287,994
Wiki hii, Mwandishi mmoja kutoka Chombo kimoja cha Habari maarufu katika nchi za Afrika Mashariki alimhoji Askofu Mwamakula kuhusiana na "Matembezi ya Hiyari"! Ufuatao ni muhutasari (paraphrased) wa mahojiano hayo!
Simu: Tilililili! Talalilalila! Tololololo!
Askofu Mwamakula: Halo! Ninaongea na nani?!
Jibu: Naitwa .... Ni mwandishi wa habari wa...
Askofu Mwamakula: Unasemaje?
Mwandishi: Nataka kukuhoji kuhusu "Matembezi ya Hiyari"!
Askofu Mwamakula: Karibu!
Mwandishi: Tunataka kujua kama "Matembezi ya Hiyari" yamepata kibari kutoka Kanisa la ....!
Askofu Mwamakula: Kanisa halihusiki katika kuandaa kwa kuwa yanaandaliwa na Askofu kwa nafasi yake. Askofu anao wajibu kwa watu wote wakiwemo hata wapagani!
Mwandishi: Tunataka kujua majimbo mengine ya Kanisa la ....yatashirikije!
Askofu Mwamakula: Hili siyo suala la Kanisa la ....! Ni suala la Watanzania wote pasipo kujali dini zao au makabila yao!
Mwandishi: Sasa mnadai Katiba Mpya, kwa nini msiende Mahakamani?
Askofu Mwamakula: Mahakama zetu ni zao la Katiba iliyopo kwa hiyo haziwezi kujipinga na wala haziwezi kwenda kinyume na Katiba iliyopo!
Mwandishi: Tena mnadai Tume Huru ya Uchaguzi, kwani iliyopo ina shida gani?
Askofu Mwamakula: Mimi ni shabiki wa Simba, wewe?
Mwandishi: Yanga!
Askofu Mwamakula: Simba ndiyo mabingwa watetezi! Unaonaje kama wao ndio wangeteua TFF, wateue marefa, wateue makamisaa, nk?
Mwandishi: Ha ha ha! Haiwezekani!
Askofu Mwamakula: Kwa hiyo Tume iliyopo ni huru?
Mwandishi: Ha ha ha! Siyo Huru!
Mwandishi: Unawaambiaje wanaokukosoa kuwa unachanganya dini na siasa?
Askofu Mwamakula: Hivi watu wanapouana kutokana na vurugu za Uchaguzi kutokana na ufinyaji wa haki na upendeleo Askofu haitwi kuendesha ibada za mazishi?
Mwandishi: Anaitwa!
Askofu Mwamakula: Askofu akiwaambia watu kuwa ili kuepuka kuuana ni vizuri tutengeneze mfumo wa haki utakaozuia mauaji atakuwa anakosea?!
Mwandishi: Hapana!
Askofu Mwamakula: Kuna swali lingine?!
Mwandishi: Hakuna Baba Askofu, kama tukikuhitaji tena tutakutafuta!
Askofu Mwamakula: Hakuna shida! Karibu!
Simu: Tilililili! Talalilalila! Tololololo!
Askofu Mwamakula: Halo! Ninaongea na nani?!
Jibu: Naitwa .... Ni mwandishi wa habari wa...
Askofu Mwamakula: Unasemaje?
Mwandishi: Nataka kukuhoji kuhusu "Matembezi ya Hiyari"!
Askofu Mwamakula: Karibu!
Mwandishi: Tunataka kujua kama "Matembezi ya Hiyari" yamepata kibari kutoka Kanisa la ....!
Askofu Mwamakula: Kanisa halihusiki katika kuandaa kwa kuwa yanaandaliwa na Askofu kwa nafasi yake. Askofu anao wajibu kwa watu wote wakiwemo hata wapagani!
Mwandishi: Tunataka kujua majimbo mengine ya Kanisa la ....yatashirikije!
Askofu Mwamakula: Hili siyo suala la Kanisa la ....! Ni suala la Watanzania wote pasipo kujali dini zao au makabila yao!
Mwandishi: Sasa mnadai Katiba Mpya, kwa nini msiende Mahakamani?
Askofu Mwamakula: Mahakama zetu ni zao la Katiba iliyopo kwa hiyo haziwezi kujipinga na wala haziwezi kwenda kinyume na Katiba iliyopo!
Mwandishi: Tena mnadai Tume Huru ya Uchaguzi, kwani iliyopo ina shida gani?
Askofu Mwamakula: Mimi ni shabiki wa Simba, wewe?
Mwandishi: Yanga!
Askofu Mwamakula: Simba ndiyo mabingwa watetezi! Unaonaje kama wao ndio wangeteua TFF, wateue marefa, wateue makamisaa, nk?
Mwandishi: Ha ha ha! Haiwezekani!
Askofu Mwamakula: Kwa hiyo Tume iliyopo ni huru?
Mwandishi: Ha ha ha! Siyo Huru!
Mwandishi: Unawaambiaje wanaokukosoa kuwa unachanganya dini na siasa?
Askofu Mwamakula: Hivi watu wanapouana kutokana na vurugu za Uchaguzi kutokana na ufinyaji wa haki na upendeleo Askofu haitwi kuendesha ibada za mazishi?
Mwandishi: Anaitwa!
Askofu Mwamakula: Askofu akiwaambia watu kuwa ili kuepuka kuuana ni vizuri tutengeneze mfumo wa haki utakaozuia mauaji atakuwa anakosea?!
Mwandishi: Hapana!
Askofu Mwamakula: Kuna swali lingine?!
Mwandishi: Hakuna Baba Askofu, kama tukikuhitaji tena tutakutafuta!
Askofu Mwamakula: Hakuna shida! Karibu!