Maombi yangu kwa wahusika wa Julius Nyerere International Airport

GREAT INVESTOR

Senior Member
Nov 13, 2018
128
295
Salam wana JF,

Kwanza niipongeze serikal zote za Tanzania kuanzia ya Nyerere mpaka ya Magufuli kwa waliyofanya na wanayofanya hata kama ni machache kuendeleza uwanja wa ndege wa JN.

Jana nlikua na safari tokea Tanzania na safari yangu ilianzia JN Airport kwa shirika la ndege la Qatar Airways, maajabu ni kuwa airport niliulizwa kirahisi tu kama una vitu ambavyo si salama kwa safari kama vimiminika nk nkajibu hapana, nilisachiwa na begi langu la mgongoni walili scan ila nliambiwa niko safe kusafiri, safari ikaanza.

Nimefika Doha international airport begi langu la mgongoni likawa scanned. Baada ya kuscan beg picha ya scana ikachora mistari mipana miwili, Dada mmoja akaniulizi is this bag yours? Japo alikua anajua ni langu, nikamjibu yes the bag is mine. Akaniambia take your shoes, belt and your jacket wear them and wait aside akaniletea kiti nkakaa, kidogo akaja police na jamaa aliyejitambulisha ni usalama jamaa wa usalama alikua Mwafrika akaanza kuongea na boss wake kwa radio call, kidogo nkaambiwa stand and face camera so as my boss may see you. Nikaingiwa na wasiwasi kutakua na nini kwenye begi mbona sijaweka chochote kibaya.

Basi akachukua passport yangu ya kusafiria na ticket zangu coz nlikua na connect ndege, zikachorwa kwa markerpen nyuma, upepo ukanijaaa wakachukua maelezo pale yule afisa usalama mu Africa akajua nimejaa upepo,akaja akaniambia usihofu hakuna kitakachoharibika,niamini mimi ni Mwafrica mwenzako kama kuna chochote kitatokea kama ku cancel ur remaining journey ntakua responsible kwa chochote upepo ukanitoka kidogo utaratibu wa kusachi bag ukafuata, nkaambiwa your going to help and witness what is inside nkasema OK, nkaambiwa open you bag and empty every thing basi nkafanya ivyo zipu ya kwanza kukawa hakuna kitu kibaya, Jamaa akiangalia scana ile mistar anaionyesha kwenye zipu ndogo akaniambia nifungue zipu ndogo kiukweli ndani kulikua na markerpens, nail cutter na nyembe fulani inavalishwaga kwenye kisu.

Conclusion ikawa ni kitu cha ncha kali, ivi vitu sikua najua kama viko ndani ya beg langu.

Walinichukua maelekezo tena huku wanajaza form wakatengeneza report yao.

Swali kuu lilikua, UMETOKEA NCHI GANI NA JE MNAKAGULIWA KABLA YA KU BOARD, nkajibu ndiyo, wakauliza aina gani ya Inspection vitu kama hivi vinapita, sikua na jibu, wakaniambia your not first Tanzanian cought with sharp objects inside your bag.

Maana ya mimi si Mtanzania wa kwanza kukutwa na sharp object kwenye beg kwa maelezo yao though naamini hata wanaokutwa na hivi vitu huwa hawajui kama vipo kwenye mabegi yao.

Kauli ya mwisho ya police, ni kwamba we have to be more carefully with Tanzanian connect flights or who ends here during inspection.

MAOMBI YANGU KWA WAHUSIKA JN

Kama uwanja wa ndg ndo tegemezi na ndo unaconnect watu na mataifa mengine basi jaribuni sana kutafuta mashine za kuscan na kuweza kubaini vitu visivyokubalika vilivyopo ndani ya mabegi, hili litapunguza Tanzania kunyooshewa kidole.

Naamin kama kungekua na hizo mashine ingekua ngumu sana kusikia Mtanzania kashikwa na dawa zisizo ruhusiwa nje ya nchi au vitu kama sharp objects kwenye bag AU PENGINE IZI MASHINE ZIPO ILA WAHUSIKA HAWAZITUMII IPASAVYO.
 
Mbona JKIA kuna check in mbili? Ya chini na ya juu yenye escalator belt, na zote lazima umwage vitu chini. Sasa wewe ilikuwaje hata sielewi.
 
Swali kuu sababu gani unatia vitu vya ncha kali ktk begi lako unaloingia nalo ndani ya ndege wakati ni vitu havistahili kuwepo ndani ya begi lako?

Shukuru watu wa Qatar walikuwa waelewa, ila tusome maangalizo yanayo kataza vimiminika, vitu vya ncha kali au vinavyoweza kutumika kama kifaa cha kuumiza pia tuhakikishe mabegi yetu tunayapakia vitu wenyewe siyo kumuachia mtu akuwekee vitu ambayo hafahamu kuwa vinakatazwa.

Mara kadhaa watu wa usalama airport wanaweza kupitiwa na wasione vitu kama hivyo.
 
Mmmh international flights unapakije bila kuhakikisha huna vitu vyenye ncha kali?

Habari ziwafikie wasiojua kukagua vizuri!

Everyday is Saturday............................... :cool:
 
Makosa yako unataka kuwatupia watu wengine unaposafiri jaribu kukagua beg lako lote vile vinavyohusika ndio uende navyo wengine wanakung'uta kabisa beg huku likiwa zip zipo wazi ili aanze kuweka nguo zake. Safari ina code zake ukizijua utasafiri miaka nenda miaka rudi hakuna utakachokutana nacho.
 
Siyo airport tu hata sehemu sensitive kuingia na kitu chenye ncha unakuta umeoita navyo, kutakuwa na tatizo sehemu.
 
Hivi huwa mnapaki tu manguo bila kujua kwenye mifuko midogo kuna nini?
We waache tu. Ingekua marekani halafu akasachiwa na Askari anaechukia weusi muda huu jamaa yetu angekua kwenye penitentiary moja halafu isolation block. Kama anajina la kiarabu wangekua wanafikiria kumpeleka Guantanamo bay huku amefungwa kitambaa cheusi usoni.
We unadhani Nani mbaguzi angedhani umeviweka hivyo vitu kibahati mbaya na hukudhamiria ku dhuru? Huku unaitwa Abdulshit
 
Kauli ya mwisho ya police, ni kwamba we have to be more carefully with Tanzanian connects flights or who ends hear during inspection.
Polisi kauli yao ya mwisho wakakwambia:

"we have to be more carefully with Tanzanian connects flights or who ends hear"

Kwa maelezo kama hayo hakuna atakaekuchukulia kwa uzito.
 
Kama uwanja wa ndg ndo tegemezi na ndo unaconnect watu na mataifa mengine basi jaribuni sana kutafuta mashine za kuscan na kuweza kubaini vitu visivyokubalika vilivyopo ndani ya mabegi, hili litapunguza Tanzania kunyooshewa kidole.

Naamin kama kungekua na hizo mashine ingekua ngumu sana kusikia mtanzania kashikwa na dawa zisizo ruhusiwa nje ya nchi au vitu kama sharp objects kwenye bag AU PENGINE IZI MASHINE ZIPO ILA WAHUSIKA HAWAZITUMII IPASAVYO.
Ujuaji wetu ndiyo unatuponza, hii ni dalili kwamba tumefungiwa mashine fake kwenye huo uwanja wetu.
 
Swali kuu sababu gani unatia vitu vya ncha kali ktk begi lako unaloingia nalo ndani ya ndege wakati ni vitu havistahili kuwepo ndani ya begi lako?

Shukuru watu wa Qatar walikuwa waelewa, ila tusome maangalizo yanayo kataza vimiminika, vitu vya ncha kali au vinavyoweza kutumika kama kifaa cha kuumiza pia tuhakikishe mabegi yetu tunayapakia vitu wenyewe siyo kumuachia mtu akuwekee vitu ambayo hafahamu kuwa vinakatazwa.

Mara kadhaa watu wa usalama airport wanaweza kupitiwa na wasione vitu kama hivyo.
Begi linavimifuko vingi sana sasa sikujua kama kuna sehemu sijakqgua.

Ila mwsho wa yote JN ivi vitu mbona visijulikane kama vipo kwenye bag
 
Begi linavimifuko vingi sana sasa sikujua kama kuna sehemu sijakqgua.

Ila mwsho wa yote JN ivi vitu mbona visijulikane kama vipo kwenye bag
Ur bag is ur responsibility, ungekaguliwa JNIA ukakutwa na bangi ungesema haya?? Ashakum si matusi

Wao wamezembea ila wewe umezembea zaidi!

Everyday is Saturday............................... :cool:
 
Salam wana JF,

Kwanza niipongeze serikal zote za Tanzania kuanzia ya Nyerere mpaka ya Magufuli kwa waliyofanya na wanayofanya hata kama ni machache kuendeleza uwanja wa ndege wa JN.

Jana nlikua na safari tokea Tanzania na safari yangu ilianzia JN Airport kwa shirika la ndege la Qatar Airways, maajabu ni kuwa airport niliulizwa kirahisi tu kama una vitu ambavyo si salama kwa safari kama vimiminika nk nkajibu hapana, nilisachiwa na begi langu la mgongoni walili scan ila nliambiwa niko safe kusafiri, safari ikaanza.

Nimefika Doha international airport begi langu la mgongoni likawa scanned. Baada ya kuscan beg picha ya scana ikachora mistari mipana miwili, Dada mmoja akaniulizi is this bag yours? Japo alikua anajua ni langu, nikamjibu yes the bag is mine. Akaniambia take your shoes, belt and your jacket wear them and wait aside akaniletea kiti nkakaa, kidogo akaja police na jamaa aliyejitambulisha ni usalama jamaa wa usalama alikua Mwafrika akaanza kuongea na boss wake kwa radio call, kidogo nkaambiwa stand and face camera so as my boss may see you. Nikaingiwa na wasiwasi kutakua na nini kwenye begi mbona sijaweka chochote kibaya.

Basi akachukua passport yangu ya kusafiria na ticket zangu coz nlikua na connect ndege, zikachorwa kwa markerpen nyuma, upepo ukanijaaa wakachukua maelezo pale yule afisa usalama mu Africa akajua nimejaa upepo,akaja akaniambia usihofu hakuna kitakachoharibika,niamini mimi ni Mwafrica mwenzako kama kuna chochote kitatokea kama ku cancel ur remaining journey ntakua responsible kwa chochote upepo ukanitoka kidogo utaratibu wa kusachi bag ukafuata, nkaambiwa your going to help and witness what is inside nkasema OK, nkaambiwa open you bag and empty every thing basi nkafanya ivyo zipu ya kwanza kukawa hakuna kitu kibaya, Jamaa akiangalia scana ile mistar anaionyesha kwenye zipu ndogo akaniambia nifungue zipu ndogo kiukweli ndani kulikua na markerpens, nail cutter na nyembe fulani inavalishwaga kwenye kisu.

Conclusion ikawa ni kitu cha ncha kali, ivi vitu sikua najua kama viko ndani ya beg langu.

Walinichukua maelekezo tena huku wanajaza form wakatengeneza report yao.

Swali kuu lilikua, UMETOKEA NCHI GANI NA JE MNAKAGULIWA KABLA YA KU BOARD, nkajibu ndiyo, wakauliza aina gani ya Inspection vitu kama hivi vinapita, sikua na jibu, wakaniambia your not first Tanzanian cought with sharp objects inside your bag.

Maana ya mimi si Mtanzania wa kwanza kukutwa na sharp object kwenye beg kwa maelezo yao though naamini hata wanaokutwa na hivi vitu huwa hawajui kama vipo kwenye mabegi yao.

Kauli ya mwisho ya police, ni kwamba we have to be more carefully with Tanzanian connect flights or who ends here during inspection.

MAOMBI YANGU KWA WAHUSIKA JN

Kama uwanja wa ndg ndo tegemezi na ndo unaconnect watu na mataifa mengine basi jaribuni sana kutafuta mashine za kuscan na kuweza kubaini vitu visivyokubalika vilivyopo ndani ya mabegi, hili litapunguza Tanzania kunyooshewa kidole.

Naamin kama kungekua na hizo mashine ingekua ngumu sana kusikia Mtanzania kashikwa na dawa zisizo ruhusiwa nje ya nchi au vitu kama sharp objects kwenye bag AU PENGINE IZI MASHINE ZIPO ILA WAHUSIKA HAWAZITUMII IPASAVYO.
Kweli mkuu
 
Swali kuu sababu gani unatia vitu vya ncha kali ktk begi lako unaloingia nalo ndani ya ndege wakati ni vitu havistahili kuwepo ndani ya begi lako?

Shukuru watu wa Qatar walikuwa waelewa, ila tusome maangalizo yanayo kataza vimiminika, vitu vya ncha kali au vinavyoweza kutumika kama kifaa cha kuumiza pia tuhakikishe mabegi yetu tunayapakia vitu wenyewe siyo kumuachia mtu akuwekee vitu ambayo hafahamu kuwa vinakatazwa.

Mara kadhaa watu wa usalama airport wanaweza kupitiwa na wasione vitu kama hivyo.
Wabongo wengi tunapenda kulalamika baada ya tatizo kujulikana ilihali mwanzo walikuwa hawalijui tatizo na chanzo.

Mkuu unamuuliza huyu maswali kama hayo kwanini usiulize kwanini pale airport wameshindwa kubaini hayo na wakamuulizia palepale, mmesubiri mpaka watu wanaoelewa majukumu yao vema kubaini tatizo ndipo mnarudi kumlaumu mhusika.

Tunapenda sana kujitetea kuonekana tupo sawa. Yaani hatunaga muda wa kuwajibika na kujifunza kutokana na makosa yetu.

Kilichotokea kwa mtoa mada na jinsi ulivyohoji maswali ni sawa tu na kilichonitokea mwaka fulani na kupewa kesi kisha kukaa mahabusu zaidi ya wiki moja kisha baadae ndo uchunguzi kukamilika na maelezo yangu kuonekana ni kweli na sina hatia.

Nilisikitika sana maana jinsi walivyokuwa wanahangaika na jambo dogo kabisa huku ukweli ukiwa wazi na maswali yao kuwa dizaini hii jinsi unavyouliza niliwaona hata zile nafasi wamepewa tu.

Huku kwetu utekelezajj wa majukumu kwa baadhi ya watu ni ZERO KABISA, mtu umewekwa kukagua na umekutana na mtu unamuuliza kama kabeba kitu cha hatari, just simple tu hivyo kisha unamruhusu anapita anaenda dakwa nchi zingine huko, bado hilo halionekani.

Watu unasikia amekamatwa airport huko na madawa halafu katoka nazo Tanzania. Swali ni je kapitaje nazo airport ya Tanzania???

Huku akija ndiyo kama hivi unamuuliza wewe kwanini umebeba vitu hivyo ilihali haviruhusiwi? Hivi ndivyo tunavyofanya kazi.

Inasikktisha sana.

Sent from my TECNO W2 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom