Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,870
- 155,831
Nina mwaka wa nane wa ndoa na hakika nimekuwa ni mvumilivu Sana na mwaminifu Sana kwa ndoa yetu.
Nimezaliwa na kukulia kwenye familia ya Kikristo yenye msimamo mkali wa kiimani, hivyo Basi sijawahi kuvuta sigara, kunywa Pombe na hata uzinzi sio mzinzi, mke wangu ni mwanamke pekee kulala naye tangu nizaliwe.
Kinachonikera kwa miaka yote hiyo mke wangu amekuwa akitamani sana kumjua mwanamke ninaye tembea naye nje ya ndoa.
Mara ya Kwanza nikajua ananitania, Mara kwa Mara alikuwa ananiambia darling natamani nimjue mwanamke unayetembea naye, nione kanizidi nini?
Daima jibu langu Mimi nimeokoka siwezi kuwa na mtu mwingine zaidi yako. Haniamini na haamini majibu yangu, simu zangu na e mails yeye ndiye huset password, ana access nazo muda wote.
Sasa kuanzia juzi Yuko kwenye maombi, anaomba aonyeshwe kwa namna yoyote mwanamke ninayetembea naye, maana anachojua yeye hamna mwanaume asiyechepuka.
Mbaya zaidi anaomba kwa kulia kwa sauti huku akipigapiga ukutani.
Nimezaliwa na kukulia kwenye familia ya Kikristo yenye msimamo mkali wa kiimani, hivyo Basi sijawahi kuvuta sigara, kunywa Pombe na hata uzinzi sio mzinzi, mke wangu ni mwanamke pekee kulala naye tangu nizaliwe.
Kinachonikera kwa miaka yote hiyo mke wangu amekuwa akitamani sana kumjua mwanamke ninaye tembea naye nje ya ndoa.
Mara ya Kwanza nikajua ananitania, Mara kwa Mara alikuwa ananiambia darling natamani nimjue mwanamke unayetembea naye, nione kanizidi nini?
Daima jibu langu Mimi nimeokoka siwezi kuwa na mtu mwingine zaidi yako. Haniamini na haamini majibu yangu, simu zangu na e mails yeye ndiye huset password, ana access nazo muda wote.
Sasa kuanzia juzi Yuko kwenye maombi, anaomba aonyeshwe kwa namna yoyote mwanamke ninayetembea naye, maana anachojua yeye hamna mwanaume asiyechepuka.
Mbaya zaidi anaomba kwa kulia kwa sauti huku akipigapiga ukutani.