incredible terminator
JF-Expert Member
- Aug 1, 2016
- 2,229
- 3,525
Habari za leo wakuu, tusiende mbali ningeomba mamlaka kama humu JF zinapata pita basi zipitie hili, maana hata pakulalamikia hatuna nilishaenda TAKUKURU zaidi ya mara moja ila ninaambiwa niende polisi hukohuko Wilayani BAHI sasa swali langu ni je tangu lini mtuhumiwa akapewa nafasi ya kujitolea hukumu?
Kama hizi taasisi kama TAKUKURU wanashindwa kutekeleza majukumu yao waturuhusu sisi wenyewe tutadeal nao najua wao wanasiraha za moto ila siraha ya moto si chochote mbele ya chuma cha chogo kwa mwenye hasira aliyekupania pasipokujijua,
Hawa polisi wanawanyanyasa sana wafanya biashara wadogo wanaotegemea minada ili kuendesha shughuli zao.
Wanachokifanya huwa siku za minada wanachukua Gari lao wanaenda wanatafta eneo la njia panda ambayo inaelekea mnadani wanapaki gari lao vichakani na wao kujibana pembeni ya barabara, kinachofanyika huwa ni kila anaepita na chochote, awe na kuku anapeleka mnadani wanamkamata, awe na mbuzi au awe na bodaboda na belo lake la mitumba wanamkamata kisha wanakaa nao.
Kama mnavyojua wafanya biashara wanaopenda kuwahi wanawatoza pesa kiasi cha elfu 30 hadi 20 na kisha kuwaachia, cha kushangaza ni kwamba wanamkamata bodaboda na kama mnavyofahamu bodaboda za ndugu zetu wa vijijini huwa ni chombo za kazi wakimkamata mtu wanampigia kila kosa elfu 30.
Hebu imagine wanakagua kuanzia sitemirror, indicators, tyre, helmet, lessen, breaklite, drivingboot, unakuta bodaboda mmoja anapigiwa galama ya laki3 au nne kisha wanakuomba ulipe 20 au 30 wanakuachia na usipolipa wanashinda na bodaboda yako siku nzima hadi watakapoondoka ndio wanazioacha au mda mwingine wanaweza kuondoka nazo, na kama mnavyojua watu sio kwamba hawajui haki haki wanazijua ila wanawatengenezea mlolongo ambao unaona ni bora tu uwape hela ili wakuachie uendelee na mambo yako,
Nimekutana nao katika minada karibia yote wilayani BAHI Ikiwemo MNADA WA NONDWA, MNADA WA MDEMU, MNADA WA LAMAITI, MNADA WA KIGWE, MNADA WA BAHI, na taarifa zilishawafikia TAKUKURU lakini mlolongo unarudi kuwa ulele, kiufupi nilitegemea kwamba TAKUKULU wangekuwa upande wangu kuwa siku nikiwakuta niwapgie waje washuhudie kinachofanyika ila mambo niliyoambiwa TAKUKURU ni yaleyale kuwa nikiwaona nipige simu Kituo cha polisi kilichopo karbia na mimi sasa hapa nikajiuliza unashtakije polisi mbele ya polisi mwenzie?
Kama hizi taasisi kama TAKUKURU wanashindwa kutekeleza majukumu yao waturuhusu sisi wenyewe tutadeal nao najua wao wanasiraha za moto ila siraha ya moto si chochote mbele ya chuma cha chogo kwa mwenye hasira aliyekupania pasipokujijua,
Hawa polisi wanawanyanyasa sana wafanya biashara wadogo wanaotegemea minada ili kuendesha shughuli zao.
Wanachokifanya huwa siku za minada wanachukua Gari lao wanaenda wanatafta eneo la njia panda ambayo inaelekea mnadani wanapaki gari lao vichakani na wao kujibana pembeni ya barabara, kinachofanyika huwa ni kila anaepita na chochote, awe na kuku anapeleka mnadani wanamkamata, awe na mbuzi au awe na bodaboda na belo lake la mitumba wanamkamata kisha wanakaa nao.
Kama mnavyojua wafanya biashara wanaopenda kuwahi wanawatoza pesa kiasi cha elfu 30 hadi 20 na kisha kuwaachia, cha kushangaza ni kwamba wanamkamata bodaboda na kama mnavyofahamu bodaboda za ndugu zetu wa vijijini huwa ni chombo za kazi wakimkamata mtu wanampigia kila kosa elfu 30.
Hebu imagine wanakagua kuanzia sitemirror, indicators, tyre, helmet, lessen, breaklite, drivingboot, unakuta bodaboda mmoja anapigiwa galama ya laki3 au nne kisha wanakuomba ulipe 20 au 30 wanakuachia na usipolipa wanashinda na bodaboda yako siku nzima hadi watakapoondoka ndio wanazioacha au mda mwingine wanaweza kuondoka nazo, na kama mnavyojua watu sio kwamba hawajui haki haki wanazijua ila wanawatengenezea mlolongo ambao unaona ni bora tu uwape hela ili wakuachie uendelee na mambo yako,
Nimekutana nao katika minada karibia yote wilayani BAHI Ikiwemo MNADA WA NONDWA, MNADA WA MDEMU, MNADA WA LAMAITI, MNADA WA KIGWE, MNADA WA BAHI, na taarifa zilishawafikia TAKUKURU lakini mlolongo unarudi kuwa ulele, kiufupi nilitegemea kwamba TAKUKULU wangekuwa upande wangu kuwa siku nikiwakuta niwapgie waje washuhudie kinachofanyika ila mambo niliyoambiwa TAKUKURU ni yaleyale kuwa nikiwaona nipige simu Kituo cha polisi kilichopo karbia na mimi sasa hapa nikajiuliza unashtakije polisi mbele ya polisi mwenzie?