Maofisa ubalozi wanawanyanyasa Watanzania

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,006
Maofisa ubalozi wanawanyanyasa Watanzania
JIBU LA SWALI LA MBUNGE KIGOMA KASKAZINI

na Peter Nyanje na Rachael Chizoza, Dodoma
Tanzania Daima~Sauti ya Watu

WATANZANIA wengi walioko nje ya nchi hawaoni umuhimu wa kwenda kujiandikisha katika ofisi za balozi kutokana na manyanyaso wanayoyapata kutoka katika ofisi hizo, Mbunge wa Viti Maalum, Magdalena Sakaya alisema jana.

Akiuliza swali la nyongeza, Sakaya alisema kuwa balozi nyingi haziwajali Watanzania wanaoishi nje katika maeneo yao kiasi kwamba hawaoni umuhimu wa kwenda ubalozini kujiandikisha.

Aliutaja ubalozi wa Canada kama mfano wa balozi ambazo haziwajali Watanzania na kuihoji serikali inachukua hatua gani kurekebisha hali hiyo.

Katika swali la msingi, Kabwe Zitto (CHADEMA) alihoji serikali ina mpango gani wa kuwa na maofisa maalum wa kushughulikia masuala ya jumuiya za Watanzania wanaoishi nje ya nchi.

Katika swali la nyongeza, Zitto alisema balozi kadhaa haziwajali Watanzania wanaoishi nje na kutolea mfano wa vifo vya Watanzania wawili waliouawa Michigan, Marekani zaidi ya mwaka mmoja uliopita, lakini hadi sasa ubalozi haujaonyesha juhudi zozote za kuwasaka waliofanya mauaji hayo.

Akijibu maswali hayo, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Seif Idd, alisema iwapo kuna balozi zinazowanyanyasa Watanzania, zinakwenda kinyume cha majukumu yake.

Alisema kazi kubwa ya balozi hizo ni kulinda maslahi ya Watanzania walioko kwenye nchi hizo kwani zinahesabika kama sehemu ya Tanzania katika nchi ziliko.

Aidha, Naibu Waziri huyo alikubaliana na Zitto kuwa jumuiya za Watanzania wanaoishi nje ya nchi, zinaongezeka kutokana na kukua kwa mahusiano baina ya Tanzania na nchi nyingine kiuchumi, kisiasa na kijamii.

Alisema kila Mtanzania anayekwenda nje ya nchi anatakiwa kwenda kujiandikisha katika ofisi ya ubalozi ulio karibu na kutoa taarifa zake ili kuwawezesha maofisa wa ubalozi kujua yuko wapi na shughuli zipi.

Naibu Waziri huyo alisema kutokana na ongezeko la Watanzania katika baadhi ya nchi, hivi karibuni wizara ilichukua hatua ya kupeleka maofisa uhamiaji katika balozi kama vile London, Washington, Nairobi, Pretoria, Bujumbura na Abu Dhabi.

Alisema tatizo lipo kwa Watanzania wanaoingia katika nchi hizo isivyo halali kwa kuwa wahamiaji wa aina hii hawapeleki taarifa zao ubalozini, hivyo kuwa vigumu kuwapatia huduma za kijamii kupitia balozi hizo.
 
Ninajiamini kwa silimia 100 kwamba Naibu waziri (Bwana Seif) hajui alisemalo. Uki-analyse aliyoyasema utafikia conclusion kwamba hajajibu kifasaha hata swali moja kati ya maswali yote aliyoulizwa. Kwa analysis yangu ya kiharakaharaka ninadhani Bwana Seif siku za zamani atakua alikuwa ni mmojawapo wa wale jamaa waliojazana kwenye balozi zetu za nje wanaopiga mihayo 24/7 bila ya kujua what they've to do kutimiza wajibu zao kama maafisa balozi huko nje.

Anasema

1. "kila Mtanzania anayekwenda nje ya nchi anatakiwa kwenda kujiandikisha katika ofisi ya ubalozi ulio karibu na kutoa taarifa zake ili kuwawezesha maofisa wa ubalozi kujua yuko wapi na shughuli zipi."

Swali langu kwake ni je hao maafisa balozi wazembe wakishajua niko wapi na nafanya shughuli zipi, je watatumia taarifa hizo kufanyia kitu gani cha maana ambacho kitani-benefit mimi binafsi pamoja na watanzania wenzangu? Tumeshuhudia watu kadhaa wakifariki nje ya nchi na cha maana zaidi kitakachotoka balozini ni salamu za rambirambi zikielekezwa tu kwa wale marehemu ambao walibahatika kuwa watu maarufu wakati wakiwa hai. Akina Zuberi Ayubu ama Christopher Alexander wakifariki hautakuja sikia balozi zikituma angalau hizo salamu za rambirambi kwa wafiwa. Hivyo basi sikuelewi ndugu Naibu waziri unapoeleza kwamba watu waendao nje wanatakiwa kujiandikisha balozini kwa sababu I do not think it will help me anyway. It is just a waste of resources (kalamu, karatasi na mafaili) ambazo zingeweza pelekwa vijijini kuwasaidia wanafunzi wanaoshindwa kununua madaftari.

2. "Naibu Waziri huyo alisema kutokana na ongezeko la Watanzania katika baadhi ya nchi, hivi karibuni wizara ilichukua hatua ya kupeleka maofisa uhamiaji katika balozi kama vile London, Washington, Nairobi, Pretoria, Bujumbura na Abu Dhabi."

Mbona hatujaona uongezekaji wowote ki-efficiency katika balozi hizo? Mbona malalamiko ya watanzania waishio nje bado yamo palepale? Rudisha watu wako nchini maana hawana faida yoyote zaidi ya kuongeza cost kwa nchi yetu. Pesa ya kumweka afisa balozi mmoja nje ya nchi ingetosha kununua ambulance moja itakayowasaidia akina mama wajawazito huko vijijini. Ni bora ikanunuliwa ambulance kijijini kuliko kuweka corrupt and inefficient people huko abroad.

3. "Alisema tatizo lipo kwa Watanzania wanaoingia katika nchi hizo isivyo halali kwa kuwa wahamiaji wa aina hii hawapeleki taarifa zao ubalozini, hivyo kuwa vigumu kuwapatia huduma za kijamii kupitia balozi hizo."

Ndugu Naibu waziri you are flat wrong kwenye hili. Kuna very influential professionals uko nje ambao hata siku moja hutakuja sikia wametia mguu wao ubalozini. Wengi hawaendi ubalozini kwa kuwa hakuna benefit yoyote watakayopata zaidi ya kwenda kushuhudia inefficient & undeserving people abusing tax payers' funds. It hurts...

Kama Serikali inataka kuwe na mabadiliko huko balozini ni bora wangefanya mabadiliko katika mfumo mzima wa uendeshaji wa balozi na uteuaji wa maafisa balozi. I do not believe kwamba maafisa balozi waliomo kwenye balozi zetu ni mojawapo wa bright Tanzanians ambao wanaweza fanya kazi ya kuiuza (in a good way) nchi yetu. Balozi zinapaswa kuwa staffed na intelligent people, na sio wavaa ndala ambao tumezoea kuwaona balozini ambao sifahamu vigezo gani vilitumika kuwaweka mumo. We want to see intelligent people kwenye balozi zetu, na sio maafisa waliojaa inferiority complex ambayo inawasababishia wawe na maghadhabu ya ajabu wawaonapo watanzania wakienda mabalozini.

I strongly recommend kwa Serikali ingekuwa ikiwafanyia performance review mara kwa mara hawa Mawaziri, manaibu waziri na makatibu wizara wetu. Ni aibu kubwa sana kwa mimi mdanganyika kuona watu wa dizaini za huyu jamaa wakiwa wanaendelea kuongoza serikali yetu wakati tunao watu wengi ambao wana uwezo mkubwa wa kufikiri zaidi yao. Sitaki kufikiria namna mtu za dizaini hizi (Bwana Seif) zinavyojieleza in case wakiwa kwenye capacity ya kui-represent nchi yetu kwenye makongamano ama mikutano yeyote ya kimataifa. Ni aibu tupu...
 
Hawa UBALOZI nao ni sehemu ya kurekebisha kwani hawatutumikii sisi hilo liko wazi!
Na pia si waelewa kwani sidhani kama wanatoa ushauri mzuri kwa viongozi wetu kuhusiana na issue mbali mbali!
Sasa ni kweli kama hawawatumikii watanzania...THEN SI HAKI KUSEMA WANATUMIKIA MAFISADI?
Kama watanzania wanataka kuwekeza nchini mwao na wao wanagangamala na watu wa MIKATABA MIBOVU...THEN NA NYIE NI WA KULAUMIWA UBALOZI!
NA HABARI ZA BALLALI KUTUFICHA FICHA NDIO KABISAA!
 
Kuna haja ya kuanza ku-question uwezo wa hawa wanaopewa hizi kazi. Kilichosemwa na wabunge kinaonekana kuwa ni kweli, na balozi ameshindwa kujibu. Ameambiwa kuwa balozi zinakwenda kinyume na taratibu na yeye anarudia swali lilelile na kuliita jibu. So poor, he needed to give a bit more intelligent answer.
 
Kuna haja ya kuanza ku-question uwezo wa hawa wanaopewa hizi kazi.

...Ameambiwa kuwa balozi zinakwenda kinyume na taratibu na yeye anarudia swali lilelile na kuliita jibu. So poor, he needed to give a bit more intelligent answer.

Halafu kaambiwa watu hawajiandikishi kwa sababu hawaoni faida yake na wananyanyaswa, na yeye anarudia kusisitiza "watu waende kujiandikisha..."

Yani viongozi wa Bongo vituko!
 
Hili tatizo halikuanza leo wala jana, sisi tuliopanda meli in the 80s ndio tunawajua vizuri sana maofisa wa ubalozi,

Na si balozi zote, kuna baadhi ya balozi ambazo zina maofisa wastaarabu na kuna zile ambazo zina maofisa mafisadi, nyingi tunazijua kwa majina mpaka maofisa na mabalozi wajinga wajinga, wabunge walipaswa kutaja majina ya ofisi na majina ya maofisa kwa sababu tunayo yote, tunaweza kuwapatia!
 
Hili tatizo halikuanza leo wala jana, sisi tuliopanda meli in the 80s ndio tunawajua vizuri sana maofisa wa ubalozi,

Ki vipi, nini connection ya mabalozi, mabaharia, na the '80?

Nilifikiri mabahiria huwa ni ki vyao vyao, au?
 
Mkuu kuuliza sio ujinga, ni sisi wasela ndio tuliaoanzisha tabia ya kuwa-ignore mabalozi na ofisi zao, katika hiyo miaka ninayoisema majuu wabongo hawakuwa wengi sana kama siku hizi, ninaweza hata kukutajia majina ya wabongo wote waliokuwepo London mwaka 1985 nilipokuwepo pale, lakini leo siwezi kabisaa, enzi hizo ilikuwa ni wanafunzi na sisi wasela, wanafunzi walikuwa wanakubalika sana kwenye ofisi zetu za kibalozi, lakini sio sisi wazamiaji, the matter of fact hawa maofisa enzi hizo walikuwa na mandate ya kuto tusaidia kabisaa na sisi tukaamua since then kuwa ni afadhali kufa kuliko kwenda ofisi ya ubalozi, haya ya sasa ni marudio tu mkuu ndio ninachokisema,

Makelele ya sasa ni kwa sababu hatimaye sasa hizi ofisi zimewageuzia kibao hata wananfunzi, ndio maana unasikia kilio mpaka bungeni, lakini ukweli ni kwamba ofisi hizi zimekuwa na tabia hizi mbaya toka zamani, ndio hasa point yangu.
 
kweli baadhi ya maafisa katika balozi zetu wana matatizo na hawatumii ustaarabu katika utekelezaji wa majukumu yao. si kweli hali hii ipo kwa
maofisa wote waliopo ubalozini.

nadhani ni vizuri tuzingatie ukweli kwamba katika balozi wapo maafisa kutoka
wizara mbali mbali, mfano mambo ya nje, ulinzi, mambo ya ndani, ofisi ya rais, na biashara. mchanganyiko huu unategemea majukumu ya ubalozi. sasa kwa hali hii kama ubalozi haujaeleza vizuri katika tovuti zao (kama wanazo) au sehemu nyingine zinazohusika nani anahusika na nini basi ni rahisi sana kwa mtu kwenda kueleza matatizo kwa mtu asiye husika. sasa ikiwa bahati mbaya afisa huyo akiwa ndio baadhi ya wale wenye nyodo basi inakuwa taabu. kuepuka na hili ni vizuri balozi zingeweka wazi majukumu ya maafisa wake ili wananchi wajue nani wa kuwasiliana nae.

lakini pia inabidi nasi tujitazame kama kweli hatuchangii katika kujenga hali hii. ni wangapi hawajiandikishi ubalozini kwa vile wamesikia maafisa wa ubalozi ni bomu? tena mara nyingine utakuta mtu kalalamikia huduma aliyoipata ubalozi a basi yeye hata akienda ubalozi b,c au hata d anaona wote ni hao hao.

je inawezekana kwamba mtu kaambiwa njoo kesho kwa sababu mhusika hayupo akachukulia hiyo ni nyodo kwani anaamini afisa wa ubalozi yeyote anauwezo wa kumsikilia na kumpa jibu linalotosheleza.

nafahamu fika maafisa wa ubalozi wanapita hapa kwa hiyo "mnasikia wanachi wanavyosema, jirekebisheni ili balozi zetu ziwe kweli sehemu ambayo mtanzania atakuwa na imani napo."
 
Sidhani kama kuna Mtanzania Serikalini anajua maana ya maneno 'performance review.'

Mkuu Kuhani,

Kitu hiki kipo serikalini. Idara ya Utumishi ilitumia mapesa mengi mno kutengeneza mfumo huu (OPRAS) in the early 2000's. Watumishi wote wa serikali (including wahudumu) wakawa trained kuhusiana na mambo ya job performance appraisal system, lakini sidhani kama wanau-apply sincerelly.

Kwa maelezo zaidi kuhusu OPRAS system unaweza angalia links hizi (ama google to utumishi+opras)
1. http://216.15.130.90/index2.php?option=com_content&do_pdf=1&id=75
2. http://www.utumishi.go.tz/index2.php?option=com_content&do_pdf=1&id=47

Kama hawa maafisa ubalozi tunaowazungumzia wangekuwa wakifanyiwa OPRAS fairly, sidhani kama wengi wao wange-survive mpaka sasa, kwa sababu the majority of them wanasifika kwa incompetency. Kitu kingine kibaya zaidi katika mfumo mzima wa OPRAS ni kwamba Maofisa wa juu ndio wanaowafanyia review maofisa wa chini. This means, kama ofisa wa juu akiwa ni mtu wa kupiga mihayo 24/7 what do you expect the evaluation report kwa ofisa wa chini yake itakuaje?

Nilikuwa nafikiri pia hata hawa viongozi wa serikali ambao wako juu ya watumishi wa kawaida wa serikali (i.e mawaziri, manaibu waziri na makatibu wakuu) nao wangekuwa wanafanyiwa performance review. In that way, kama zoezi zima la evaluation lingefanyika fairly bila kujali ushkaji kwamba labda fulani alinipigia sana kampeni, wababaishaji wengi wanaotoa statements za kujiaibisha nafsi zao wangeweza kuwa eliminated easily, ingawa ni vigumu mno kwa kitu hiki kufanyika in a rotten (corrupt) system kama ya kwetu. We really need competent & honest people to guide our country in moving to the next level.
 
Hili tatizo halikuanza leo wala jana, sisi tuliopanda meli in the 80s ndio tunawajua vizuri sana maofisa wa ubalozi,

Na si balozi zote, kuna baadhi ya balozi ambazo zina maofisa wastaarabu na kuna zile ambazo zina maofisa mafisadi, nyingi tunazijua kwa majina mpaka maofisa na mabalozi wajinga wajinga, wabunge walipaswa kutaja majina ya ofisi na majina ya maofisa kwa sababu tunayo yote, tunaweza kuwapatia!

Ulichosema FMES nakubaliana nacho kabisa... sio balozi zote zenye watu wasiotaka kuwaona WATZ wenzao wakienda ubalozini.Binafsi nadhani wenye hiyo tendency ya kuwaangalia wenzao wanaoenda ubalozini like something the cat has brought into the house ni aidha walioajiriwa kama locals huko japo ni watz ..huenda hawana skills esp.people skills kujua wanapaswa kubehave vipi. Mimi my experience imekuwa ya aina mbili.... kukutana na watz wazuri sana ubalozini hasa kama mnafahamiana toka home..au kukutana na wale wanaokuuliza unataka nini ubalozini!...na mark you huduma ubalozini sio kwa wale wanaoishi huko ughaibuni tu bali hata wenye kwenda kimatembezi au kikazi.Inabidi Wizara ya Foreign wawape angalau induction/orientation ili wasigeuke kero wanapokalia viti huko ubalozini.
 
Back
Top Bottom