Maofisa habari waonywa kwa kuuza siri za serikali

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,006
Na Veronica Mheta | Daily News | June 21, 2008

Serikali imesema kuwa baadhi ya maofisa habari wamekuwa wakivujisha siri za serikali kwa kuziuza kwenye magazeti wapate fedha kama mgawo kwa kufanikisha uuzwaji wa siri hizo, na kwamba sasa itachukua hatua za kisheria kukomesha hali hiyo.

Inadaiwa kuwa maofisa habari wengine huwapigia simu wahusika wa magazeti na kuwapatia siri hizo wazichapishe magazetini. Hayo yalisemwa Dar es Salaam jana na Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Kassim Mpenda, wakati akitoa maazimio ya mkutano uliofanyika mjini Morogoro hivi karibuni mbele ya maofisa habari kutoka wizara zote za serikali.

Mpenda alisema kutokana na udhaifu wa maofisa hao, magazeti yamekuwa yakinunua siri za serikali na kuzichapisha kutokana na uuzaji wa siri hizo unaofanywa na maofisa hao. Alisema ofisa habari yeyote atakayebainika kuuza au kutoa siri za serikali ili ziandikwe magazetini atachukuliwa hatua kali za kisheria.

"Jamani tushirikiane kuhakikisha siri za serikali hazitoki nje au kwenye magazeti hivyo tuhakikishe tunazilinda siri hizo. Si vyema kuandikwa magazetini na kama kuna ofisa atabainika kuuza siri hizo atachukuliwa hatua kali za sheria," alisema Mpenda.

Alisema baadhi ya mapendekezo yaliyopendekezwa na maofisa habari ni kuimarisha Idara ya Habari (MAELEZO) ili iratibu shughuli za vitengo vya Habari, Elimu na Mawasiliano ili kufanikisha utoaji taarifa za serikali kwa umma.

Aliwataka maofisa habari kuhakikisha wanaandaa taarifa za mipango watakayoifanya kwa mwaka mzima kurahisisha kutoa habari zinazohusu maendeleo ya kila wizara husika.

Aliiomba serikali iangalie jinsi ya kushughulikia vyombo vya habari binafsi vinavyoipinga serikali kwa kupotosha umma na alizitaka wizara zitumie vyombo vya habari vya serikali kutoa taarifa zake kwa umma.
 
Mpenda bwana,

Yaani hata habari siri ama mpango huo ni wa kulihujumu Taifa wewe unaita ni siri ya serikali wenye uchungu wasiilete hapa JF ?
 
Salva Rweyemamu mwingine huyu. Officer of propaganda wa Sirikali.

Tunahitaji sheria inayofanana na "Freedom of Information Act" ya kulazimisha Serikali kutoa info wanazo ziita siri wakati hazitakiwi kuwa siri.

Ukitakata kuua utandawazi unaiita kila kitu siri ya Serikali.

What bull!
 
Mpenda bwana .Yaani hata habari siri ama mpango huo ni wa kulihujumu Taifa wewe unaita ni siri ya serikali wenye uchungu wasiilete hapa JF ?

Hivi SIRI KALI ina siri gani inazozificha dhidi ya wananchi wake waliyoiweka SIRI KALI hiyo madarakani? Hakutakiwi kuwe na siri yoyote.
 
wapenda maendeleo ya nchi wataziuza hizo newz kwa umma.Kassim na wenzake huko serikalini wakifuatwa na wanahabari kutoa habari wanaanza kupiga danadana.Na pia hawatoi habari kwa wakati muafaka hadi waambiwe cha kusema.Huyu Kassim ndo aliyekimbia wanahabari kutoa taarifa ya kifo cha balali?Au anasema habari zipi?

Jana watu hawajasafiri ATCL,ndege zimeegeshwa na hakuna taarifa,sasa hapo mtu akiuza habari kuna kosa gani?Serikali ni waoga wa kutoa ukweli hadi wapange propaganda.
 
Maofisa habari waonywa kwa kuuza siri za serikali
Veronica Mheta
Daily News; Saturday,June 21, 2008 @00:01

Inadaiwa kuwa maofisa habari wengine huwapigia simu wahusika wa magazeti na kuwapatia siri hizo wazichapishe magazetini. Hayo yalisemwa Dar es Salaam jana na Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Kassim Mpenda, wakati akitoa maazimio ya mkutano uliofanyika mjini Morogoro hivi karibuni mbele ya maofisa habari kutoka wizara zote za serikali.

Mnajua kuwa Tanzania bali ya kuwa masikini ni nchi mojawapo ambayo ina mikutano mingi sana,misherehe mingi sana mpaka wahusika wanashindwa la kuongelea bai pumba tuuuu.

“Jamani tushirikiane kuhakikisha siri za serikali hazitoki nje au kwenye magazeti hivyo tuhakikishe tunazilinda siri hizo. Si vyema kuandikwa magazetini na kama kuna ofisa atabainika kuuza siri hizo atachukuliwa hatua kali za sheria,” alisema Mpenda.

Sasa,hii ni ajabu kweli yaani ghafla wananchi wamekuwa nje,yaani tumekuwa maadui?
Halafu haya mambo ya kuchota mi vijisenti yetu mnataka iwe siri tu mpaka lini?
Ndugu Mpenda inaonekana Salva ndie alikuamrisha uongee utumbo huo...pole sana....
 
Suala la kwamba serikali ni ya watu na inawekwa madarakani na watu ili kuwatumikia hao watu naona halizingatiwi hapa. Viongozi wanalewa madaraka. Wanasahau kwamba wako madarakani kwaajili ya kuwatumikia wananchi. Iweje serikali inakuwa na siri kama sio mambo machafu na ya kifisadi? Naamini kila habari ya serikali inapaswa kuwa wazi, na pale wanapoleta usiri, basi kuna harufu ya rushwa, wizi, uongo na ufisadi.
 
hIVI SIRI INAFIKAJE KWA MAAFISA HABARI! SERIKALI INA CONFIDENTIAL ISSUES KAMA ZA KIINTELIGENSIA LAKINI HIZO HAZITOLEWI KWA MAAFISA HABARI. ZINAONEKANA NA WANAOHUSIKA PEKE YAKE . HABARI IKIENDA KWA MAAFISA HABARI SI SIRI TENA.
 
Mpenda bwana .Yaani hata habari siri ama mpango huo ni wa kulihujumu Taifa wewe unaita ni siri ya serikali wenye uchungu wasiilete hapa JF ?

Hawajaonaga siri nini?
Watu wazima kama MOSSAD,KGB,CIA zinaleak sembuse hivyo vidubuwasha wanavyoviita siri?toboeni kila kitu wakikasirika wasage chupa wanywe.
 
Hatuwezi kufika kama kila kitu tunafanya siri, kama tusingekuwa na watu wenye uchungu na hii nchi hata hayo mambo ya EPA kiwira n.k bado serikali ingefanya siri...wakati wananchi tulitakiwa kujua kinagaubaga ilikuwaje watu wanajipendelea hivyo wakati ni jasho la kila mwanchi??Mpenda kama unawatisha hao wanaotupa taarifa muhimu kuhusu nchi yetu BASI sisi tunawaomba wasitishike sisi Tuko nao Pamoja waendelee kutupa taarifa maana bila wao tunaweza kukuta tumeuzwa bila kujijua.
 
Huu ni ushahidi mwingine wa jinsi ambavyo viongozi wetu wamelewa madaraka na kujisahau kiasi cha kuanza kuamini kwamba serekali ni mali yao na si ya wananchi. Bwana Mpenda anaonekana kabisa anaamini kuwa ni kosa kubwa kwa serekali kuwajika na kuripoti kwa wananchi! Kitu ambacho wengi huko serekalini hawakijui ni kwamba ni asilimia ndogo sana ya maafisa wa serekali wanaovujisha hizo taarifa kwa pesa, wengi huzitoa bure kwa kuwa wana uchungu na nchi yao.
 
Mpenda, Slava na Mama Anna Abdalla,

Je mnategemea hawa maofisa habari wale wapi? Mishahara yao ni midogo, hawana masurufu manono, mbaya zaidi wanaona jinsi wakubwa wao wa Kazi wanavyojichotea na kuhujumu nchi.

Mpenda unazungumzia maadili, maadili gani ya kukosa uzalendo kuficha uhujumu?

Sasa kuna ubaya gani wao wakiuza hizi "nyeti" kwa Waandishi na wengine ili kujipatia japo nauli ya basi na uhakika wa chakula cha kutosha kulisha familia zao?

Kwani walichouza ni kibaya kujulikana nasi? Waacheni nao wapate japo kianzio cha "halali" kuuza habari na si kuwasakama kwa kutoa undani wa uovu wenu wa ulaji rushwa na ufisadi.
 
Mada kuhusu Mengi na Masha zimekuwa na vumbi jingi sana kiasi kuwa in akuwa vigumu kutafuta karanga za kuchambua. Nimemua kuhamisha baadhi ya post ambazo kwa maoni yangu nadhani zinahitaji kuchambuliwa kwa makini kwani zinaweza kusukuma haja ya serikali kuongeza transparency katika utendaji wake. Hizi ni zile zinazohusu siri za serikali.

Swali langu kila siku ni: "Siri za serikali yetu ni nini, na kwanini ni siri, na ni siri kwa nani?"


Hivi Siku 7 zimekwisha au la?....

Kwa Maoni yangu...Mengi Kama alikuwa na ushahidi kwanini Hakwenda Mahakamani...au ndio kutafuta attentions na sympathy za wananchi...?...Angeunguziwa Products zake kama Bakhresa ingekuwaje....

Sijui wapi Masha kazungumza hii issue ya Kodi dhidi ya Mengi...kwa kuwa Masha mlevi kuna uwezekano mkubwa akawa kaitoa hio statement ktk Vikao vya ULEVI...

Ikiwa Masha kaizungumza ktk VIKAO rasmi vya SERIKALI...basi hapo kuna mambo ya msingi ya kuyaangalia.....Nadhani pia kama Mengi anajua hili limezungumzwa huko, basi hata yeye anakhoufu kwenda Mahakamani asije ulizwa Habari hizi nani kakupa...na hapo ndipo mzozo utakapokuwa mkubwa!!!!.....Let us wait n see the GAME in the court.



Ndugu nisaidieni, hivi kweli ni sahihi kwa serikali kupanga mipango ya kuwa nyanyasa kwa namna yoyote ile raia wake? Binafsi nilidhani kazi ya serikali ni pamoja na kuwalinda raia wake?

Nilipo sikia sakata hili, nilidhani pengine Mengi kalishwa KASA habari hii si kweli, Yaani nipo ndani ya butwaa kusikia kwamba serikali inamtafuta waziri aliye vujisha siri hizo ikiwa na maana kwamba ni kweli walikaa na kupanga hivo!!

Mbona hii ina inatisha??? YAANI HII NI BALAA!!


Mimi sio mwanasheria lakini sheria inasemaje kuhusiana na HAKI YA HABARI/TAARIFA kati ya mtoaji, mpokeaji na mwenye habari! Inavyoendelea sasa inaonekana ni kama lilikua tamko au kikao "nyeti" ndo kilikua kina-discuss hayo mambo! Nani aliitoa hiyo nyeti kwa Mengi! Its obviously ni wazalendo na wasio taka uonevu na ufisadi katika TAnzania hii ya leo lakini ambae alibahatika kuwa mmoja wa hao wakulu na hivyo kuingia kwenye hiko Kikao.

Lakini pia Mengi anapenda publicity stunt na jamii wa Watanzania wamuone kama mtetezi wa wanyonge lakini kikubwa mara nyingi kuonekana kwamba anaonewa na vyombo vya serikali ili shughuli zake ambazo ni "halali" ziendelee.

Japo hakumtaja jina, at last tumemjua ni Masha! Sasa huyu Bwana si wavutane mahakamani kama hawataki kutoa vielelezi ( supporting evidence) hadharani! Ili tupate ukweli?

Naamini Mengi amesema ukweli, na he can prove that in the court of law! Maana hiyo issue ni kubwa na inayohitaji Masha angekuwa ashajiuzulu! Au kwa sababu ni kilikua kikao nyeti kina splitting au divided responsibility:kwamba hiko kikao ni breeding ground for evasion of responsibility and inefficiency as "group" responsibility means every member feeling unaccountable?

It looks maybe there's a light at the end of the tunnel!

Hakuna suala la nyeti za serikali kwenye vikao batili au siri ni batili. Viapo wanavyoapa hawa mawaziri na Katiba vinatosha kuifanya nyeti hiyo kutokuwa nyeti tena. Mf. Baraza la mawaziri haliwezi kaa likapitisha maazimio ya kuipindua nchi, au kuwauwa wananchi wake au kuuza nchi then still hizo zionekane ni nyeti za serikali. Nyeti za serikali ni lazima ziwe halali. Sasa kama kweli Mengi atakuwa kweli kaipata toka ndani ya baraza na ikathitishwa kuwa kweli ilizungumzwa then, lazima iangaliwe uhalali wake kwanza ndo Mahakama watatafsiri usiri wake. Sio kila kila kitu kinakuwa siri eti tu kwa kuwa sheria ipo.

Huyu Masha anaonekana ana shombo ya ufisadi na ulimbukeni wa madaraka. Tanzania mpya hii babake mpaka kufuli zitambana.


Baada ya serikali kuwa inakataa kuonyesha mikataba ya madini hata kwa wabunge na kamati yake inayohusika na madini, na sasa kusoma kuwa mkakati wa kumfilisi Mengi ulijadiliwa katika kikao kimoja cha viongozi wa cha serikali, ninajiuliza maswali matatu:

(a) Je tuna sheria inayolazimisha records za serikali kama vile agenda za vikao vyote vinavyofanywa na viongozi, barua na email wanazoandika, na maongezi yao ya simu kuwekwa kumbukumbu ya kudumu? Nina wasi wasi kuwa huenda hapana kwa vile Ikulu yetu inatumia e-mail ya Yahoo, na hakuna uthibiti wa matumizi ya simu?

(b) Je tuna sheria inayolazimisha vyombo vya habari na raia wa kawaida kuwa na haki ya kupewa habari zozote zinazuhusu serikali? Yaani kitu kama "Freedom of Information Act" ya marekani.

(c) Kama hatuna utaratibu wa kutunza records za serikali, na hatuna Freedom of information act ya kuilazimisha serikali kutoa habari za uhakika, na serikali ikaamua kudanganya wananchi kwa kudai kuwa kikao hicho hakikuwapo, na hivyo Mengi ni mwongo, je itakuwaje? Je Mengi ana uwezo wa kuthibitisha kuwa kikao hicho kilifanyika kweli iwapo serikali itakikana (hata kama kweli kilikuwapo)?
 
Vipi, hakuna anayejua lolote kuhusu haki za wananchi kufahamishwa mambo yazungumzwayo na yafanywayo na viongozi wao serikalini? Je kila atakalosema kiongozi wa serikali ni jambo nyeti linabaki ni siri ya serikali?
 
Vipi, hakuna anayejua lolote kuhusu haki za wananchi kufahamishwa mambo yazungumzwayo na yafanywayo na viongozi wao serikalini? Je kila atakalosema kiongozi wa serikali ni jambo nyeti linabaki ni siri ya serikali?


Ikiwa kuna mwanya kwa hizo 'siri' kuendelea kuwa siri milele basi kuna kasoro kubwa. Expiry date is necessary I think.
Nataraji kwamba, kwa mujibu wa katiba mahakama itakuwa na uwezo wa kutumia hizo 'siri' kwenye shughuli za mashtaka kama kielelezo inapobidi.
 
Vipi, hakuna anayejua lolote kuhusu haki za wananchi kufahamishwa mambo yazungumzwayo na yafanywayo na viongozi wao serikalini? Je kila atakalosema kiongozi wa serikali ni jambo nyeti linabaki ni siri ya serikali?

Kichuguu,

Kuna mambo ambayo inabidi kuwa siri (yaani kuna mambo huwa mimi sitaki kuyajua kabisa) ila mambo mengi yanayosemwa au kufanywa na viongozi wa serikali sio siri na hayafai kuwa siri kabisa.
 
Sasa tukiangalia tena hili la Mengi na Masha, kama lilifanyika kwenye vikao "nyeti" vya viongozi wa serikali, halafu hakuna sheria inayolazimisha majadiliano hayo ya viongozi kuwekwa kumbukumbu za kudumu ambazo zinaweza kusomwa na mahakama iktakiwa, hamuoni kuwa serikali inaweza kusema kuwa hakuna viongozi waliopanga mkakati huo na wala hakukuwa na kikao cha namna hiyo, hivyo mengi akaonekana ni mwongo ingawa kweli walikutana?

Nadhani kuwa kwa nchi kama marekani, hata handwritten notes zinazoandikwa na viongozi wakati wa kikao cha kiserikali zinaingia kwenye national archives; ndiyo maana Sandy Berger alijikuta matatizoni kwa kupoteza handwritten notes alizoandika yeye mwenyewe.

Ninadhani inabidi tujenge system yenye transparency kuzuia viongozi wasiwe wanajifanyia mambo kivyao vyao halafu wanasingizia kuwa ni nyeti.
 
Back
Top Bottom