ABC ZA 2025
JF-Expert Member
- May 2, 2018
- 1,158
- 701
Excellent madame PresidentKihistoria,Wilaya ya Manyoni ndio Wilaya ya kwanza Tanzania kuwa na DC wa kwanza Mwafrica|Mtanzania kwa lugha nyepesi Manyoni ni miongoni mwawilaya za kwanza kwanza kuasisiwa kabla hata ya Uhuru wa Tanganyika mwaka 1961
Nikweli kwamba,Wilaya hii kongwe imesahaulika karibu na awamu zote zilizowahi kutawala nchi hii yaani tangu ile ya Hayati Mwl Julius Kambarage Nyerere hata ile ya Hayati Dkt John John Joseph Pombe Magufuli zote ziliitupa Wilaya ya Manyoni kwani iko duni sana kimaendeleo hata sasa,
Ujio wa Rais Samia Suluhu Hassan unaipa Manyoni tumaini jipya la kupata maendeleo kwa kasi hasa baada ya kutoa zaidi ya TZS 3.5BL kwaajili ya Ujenzi wa shule ya wasichana ya mkoa "Singida Girls Sec School " inayotarajiwa kujengwa Kata ya Makutupora Tarafa ya Kintinku,
Awamu hii ya Sita ikichagizwa na uwepo wa Uongozi mahiri wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya chini ya Mwenyekiti hodari na Shupavu wa Chama Cha Mapinduzi Mhe Jumanne Makanda ( J4 ) kwa kushirikiana na DC Rahabu pamoja na viongozi wengine kasi ya Ukuaji wa Wilaya hii inaanza kukuna wadau wengi wa maendeleo ndani na nje ya mkoa wa Singida kwani kila kijiji kuna mradi wa Rais Samia Suluhu Hassan unaendelea,
"Mhe Rais Samia Suluhu Hassan tunamkaribisha Manyoni Sisi tuko na YeYe mpaka 2030 kwa kudra za mwenyezi Mungu " alisema Saidi mkazi wa Maweni,
View attachment 2046954View attachment 2046956
View attachment 2046952
View attachment 2046955