Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,615
- 5,690
Kama ilivyofanyika kwa huyu mtendaji basi ifanyike kwa wale vigogo wengine, maana wachini wanajifunza kwa wakubwa.
================
Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Ruvu Remit wilayani Simanjiro mkoani Manyara, Godbless Mollel, amehukumiwa kifungo cha miaka 20 jela baada ya kupatikana na hatia ya ubadhirifu na wizi wa fedha za kijiji.
Hukumu hiyo imetolewa Mei 28, 2026 na Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Wilaya ya Simanjiro, Onesmo Nicodemos, katika shauri la uhujumu uchumi lililoendeshwa na mwendesha mashtaka wa TAKUKURU, Faustin Mushi.
Soma Pia: Aliyekuwa Mtendaji wa Kijiji cha Ruvu Remiti - Manyara afikishwa Mahakamani kwa makosa ya rushwa na wizi
Mahakama imeeleza kuwa Mollel alipatikana na hatia ya makosa mawili ya ufujaji na ubadhirifu baada ya kutoa Sh4.3 milioni kutoka akaunti ya kijiji mwaka 2022, ambapo Sh3.3 milioni zilidaiwa kutumika kwenye shughuli za kijiji huku fedha hizo zikiibwa.
================
Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Ruvu Remit wilayani Simanjiro mkoani Manyara, Godbless Mollel, amehukumiwa kifungo cha miaka 20 jela baada ya kupatikana na hatia ya ubadhirifu na wizi wa fedha za kijiji.
Hukumu hiyo imetolewa Mei 28, 2026 na Hakimu Mkazi Mwandamizi wa Wilaya ya Simanjiro, Onesmo Nicodemos, katika shauri la uhujumu uchumi lililoendeshwa na mwendesha mashtaka wa TAKUKURU, Faustin Mushi.
Soma Pia: Aliyekuwa Mtendaji wa Kijiji cha Ruvu Remiti - Manyara afikishwa Mahakamani kwa makosa ya rushwa na wizi
Mahakama imeeleza kuwa Mollel alipatikana na hatia ya makosa mawili ya ufujaji na ubadhirifu baada ya kutoa Sh4.3 milioni kutoka akaunti ya kijiji mwaka 2022, ambapo Sh3.3 milioni zilidaiwa kutumika kwenye shughuli za kijiji huku fedha hizo zikiibwa.