Manyanyaso ya askari wa barabarani, wananchi tususie kuendesha magari..

Kajuni

JF-Expert Member
May 27, 2009
486
186
Wanajamvi salamu kwa wote.

Natumaini kama ni mmiliki wa chombo cha moto hususani hapa Dar e's salaam utakuwa umeisha kutana na kadhia hii.

Siku hizi askari wa barabarani wamekuwa kero kwa kuwalipisha faini kwa makosa hata madogo ambayo kama wangezingatia weledi hakuna haja ya kumlipisha dereva faini.

Hivi kwa umoja wetu hatuwezi siku moja madereva wote kususia kuendesha magari na tutembee kwa miguu ili kufikisha ujumbe kwa mamlaka husika?

Tukiendelea kukaa kimya hakika tutakufa.

Naomba kuwakilisha.
 
Wanajamvi salamu kwa wote.
Natumaini kama ni mmiliki wa chombo cha moto hususani hapa Dar e's salaam utakuwa umeisha kutana na kadhia hii. Siku hizi askari wa barabarani wamekuwa kero kwa kuwalipisha faini kwa makosa hata madogo ambayo kama wangezingatia weledi hakuna haja ya kumlipisha dereva faini.
Hivi kwa umoja wetu hatuwezi siku moja madereva wote kususia kuendesha magari na tutembee kwa miguu ili kufikisha ujumbe kwa mamlaka husika?
Tukiendelea kukaa kimya hakika tutakufa.
Naomba kuwakilisha.

Fuata sheria za barabarani hutalipishwa faini.... mbona wengine hatulipishwi kwa kuwa tunafuta sheria!!!
 
Hii ni nchi ya watu waoga, ukisusa wengine wala, hii haiwezekani tz na ukizingatia kwasasa kila mtu anapambana na hali yake.
PAMBANA NA HALI YAKO MKUU
 
Chunga saana.....jamaa alilipa faini kwa kosa la kuwa na sharubu kama za Ponyii...yaani Polisi.
 
Fuata sheria za barabarani hutalipishwa faini.... mbona wengine hatulipishwi kwa kuwa tunafuta sheria!!!
Sisemi kwamba tuvunje sheria za barabarani la hasha!! Askari police anawajibu wa kukuelimisha, kukupa onyo na mwisho kukupa faini ama kukupeleka mahakani. Lakini kwa sasa hakuna majadiliano wala wasaha wa kujieleza ama kuelimishwa hata kwa kosa dogo!!
Hii itapelekea watu kuwaogpa na wakati mwingine kutotiii!!
 
Tatizo wamekuwa sehemu ya kukusanya mapato wacha watukamue si umeona mapato yameshuka mwezi uliopita
 
Wanajamvi salamu kwa wote.
Natumaini kama ni mmiliki wa chombo cha moto hususani hapa Dar e's salaam utakuwa umeisha kutana na kadhia hii. Siku hizi askari wa barabarani wamekuwa kero kwa kuwalipisha faini kwa makosa hata madogo ambayo kama wangezingatia weledi hakuna haja ya kumlipisha dereva faini.
Hivi kwa umoja wetu hatuwezi siku moja madereva wote kususia kuendesha magari na tutembee kwa miguu ili kufikisha ujumbe kwa mamlaka husika?
Tukiendelea kukaa kimya hakika tutakufa.
Naomba kuwakilisha.
Hakuna kosa dogo barabarani. Mutuka inaweza badilisha jina la mtu ndani ya sekunde.
Fuata sheria tu ndg yangu
 
Back
Top Bottom