Manyanyaso ya askari wa barabarani, wananchi tususie kuendesha magari..

Kuna hawa wanaokaa hapa mbezi interchick na torch muda wa jioni,Askari pale Makonde anavuta magari yanayotoka mjini halafu hapo interchick kuna Askari mwenye torch ili tu akubambikie kosa la ku-overspeed.
Na hapa mjini torch za nani,mbona asubuhi mnavuta magari Kwa speed 100.
 
watanzania bila kupigwa fini....huwa tunakuwa wagumu kuelewa...lkn tukipigwa mikeka minne kwa mwezi ya faini...automatically tutafata sheria
 
Hakuna kosa dogo barabarani. Mutuka inaweza badilisha jina la mtu ndani ya sekunde.
Fuata sheria tu ndg yangu
Sheria ni sheria siku hizi hata ukipita service road opposite site unachukua cheti nafikiri kosa kama hili ni kukuelimisha dereva asitumie service road ya opposite side. Na kama ni mstaarabu basi polisi anaweza mrudisha dereva aliko toka kama adhabu!!
 
Sitoi sipokei rushwa. Gari nimeuza siku nyingi baada ya manyanyaso ya trafiki. Siku hizi mwendo carbon fibre mountain bicycle - amani tupu na mazoezi juu.
 
Baadhi ya polisi njaa hadi wanachukiza. Usiku wa manane polisi anasimama katikati ya barabara na kitochi chake kusimamisha magari. Polisi anahatarisha maisha kudai rushwa.
 
Pia kuna wale trafiki wanaokaaga kwenye mataa ya external haswa kituo cha external. Wanavizia ikikuwakia taa ya njano na ukapita unao, walivyoona madereva wa magari wamegundua janja yao sasa hivi wanavizia magari yanayotokea external ya jeshini/tfda, ukikata kushoto tu kuelekea ubungo unao Wakati kwenye mataa yoyote ukikata kushoto husubiri taa. Ila wao wakikudaka hati ya elf 30 inakuhusu
 
Wewe huna gari.
Nikweli sina gari lakini siwezi tetea uvunjwaji sheria wa makusudi wa wenye magari kisa tu eti hili ni kosa dogo upewe onyo.
Fuateni sheria za barabarani msituletee balaa
 
Cha msingi ni kufuata sheria za barabarani na kuhakikisha gari yako iko safi hapo ukipigwa faini una haki ya kuhoji na pia mamlaka husika zipo km ukutendewa haki,japo wapo baadhi ya wasimamia sheria Kwa sababu ya mapungufu yao wanakiuka kidogo utendaji,
 
Wanajamvi salamu kwa wote.

Natumaini kama ni mmiliki wa chombo cha moto hususani hapa Dar e's salaam utakuwa umeisha kutana na kadhia hii.

Siku hizi askari wa barabarani wamekuwa kero kwa kuwalipisha faini kwa makosa hata madogo ambayo kama wangezingatia weledi hakuna haja ya kumlipisha dereva faini.

Hivi kwa umoja wetu hatuwezi siku moja madereva wote kususia kuendesha magari na tutembee kwa miguu ili kufikisha ujumbe kwa mamlaka husika?

Tukiendelea kukaa kimya hakika tutakufa.

Naomba kuwakilisha.
hao ni sehemu ya TRA........... izoee hali hiyo,
 
Polisi wanatumika vibaya na serikali ,ni njaa zinasumbua wanabambikia makosa ,mimi jana Goba kanisimamisha eti tairi chafu sijaosha kaniandikia faini 30000, anaitwa INNOCENCIA huyo dada ... kwenye mkeka eti tairi mbovu wakati zipo vizuri
 
Huyu afande dada INNOCENCIA wa Goba huku Dar ntamfungulia kesi mahakamani
 
Na usilogwe kulipia zile faini zao kupitia tigo pesa sijui Mpesa aisee. Unashangaa wanakupiga mkono kukueleza kuwa hukulipa faini. Bora ulipe kwa Max Malipo maana ndio yenye receipt.
 
Back
Top Bottom