Mantiki ya kutaka bei za chakula zishuke au zisipande wakati wa mwezi wa Ramadhani nini?

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,614
141,432
Nauliza tu mantiki ya wanasiasa na wananchi kwa ujumla kuratibu bei za vyakula wakati wa mwezi wa Ramadhani. Nijuavyo mimi kufunga ni ibada na tufungapo mambo yanatakiwa kuwa kama yapasavyo na si kutengeneza nafuu/ urahisi fulani katika mfungo. Wale wafungao Kwaresma vitabu vinawataka wasiwe kama wanafiki wenye nyuso za kukunjamana na midomo mikavu bali waenende bila kujulikana kama wapo katika swaumu. Nitashukuru nikipata majawabu, amen!
 
Kichwa cha Mada kiko sawa ila maelezo ni kama umeteguka kidogo kidole gumba.

Nadhani swala la bei ya vyakula kupanda bei ikiwemo mafuta na sukari lingewekewa nguvu hii hii siku zote inayowekwa kwenye mwezi huu na mimi ningekuwa nakunywa chai hadi leo. Lakini kutokana na kujisahau kwa wanasiasa, chai nilishaisahau aslani.
 
Funga ya wanafiki huambatana na mbiu/matangazo.
According to Jesus.
mswalie mtume mkuu. hakuna unafiki wala matangazo kwenye funga hii.
swali. ni watz wangapi wanakula magimbi na viazi vitamu siku za kawaida kulinganisha na wakati huu wa mfungo?
ni wangapi wanakula na kunywa uji dairly kipindi cha kawaida kulinganisha na wakati wa mfungo?
demand vs supply
 
ni dhahiri kunaongezeko kubwa la matumizi ya vyakula ,hivyo kuwapa fursa wafanyabiashara kujineemesha.
 
Wale wafungao Kwaresma vitabu vinawataka wasiwe kama wanafiki wenye nyuso za kukunjamana na midomo mikavu bali waenende bila kujulikana kama wapo katika swaumu
Ndio hivyo hats kwa Waislam, USO unatakiwa uwe tabasamu wakati wote, ukioga upake mafuta usiwe umepauka swaumu ni ibada sio adhabu.kuhusu kupanda kwa bei nadhani kunawatu wameshajibu. Ila kwa kifupi demand huongezeka zaidi kwa mahitaji Fulani. Unapouliza swali jitahidi kuuliza kwa kujifunza sio kwa dhihaka. Remember about Religious tolorence
 
Ni lini baadhi yenu mtaacha chuki zisizo na maana, unauliza swali inaonesha nia yako sio kupata jibu ila ni kwakua unakitu kinakutekenya rohoni.
Siachi kukujibu anywayz,
Kipindi cha ramadhani mahitaji ya vyakula hasa mihogo, mgimbi, viazi, sukari n.k huongezeka mara dufu hivyo baadhi ya wafanyabiashara kwa tamaa zao hupandisha bei kiholelaa, na kusababisha usumbufu kwa waumini. Wito wa kutopandisha bei hutolewa kutokana na kasumba hiyo ya kupandisha bei kiholela.
Note: kwarezima wengi wenu huwa hamfungi so impact kwenye bidhaa huwa haipo.
 
Ni lini baadhi yenu mtaacha chuki zisizo na maana, unauliza swali inaonesha nia yako sio kupata jibu ila ni kwakua unakitu kinakutekenya rohoni.
Siachi kukujibu anywayz,
Kipindi cha ramadhani mahitaji ya vyakula hasa mihogo, mgimbi, viazi, sukari n.k huongezeka mara dufu hivyo baadhi ya wafanyabiashara kwa tamaa zao hupandisha bei kiholelaa, na kusababisha usumbufu kwa waumini. Wito wa kutopandisha bei hutolewa kutokana na kasumba hiyo ya kupandisha bei kiholela.
Note: kwarezima wengi wenu huwa hamfungi so impact kwenye bidhaa huwa haipo.
Na cha ajabu wafanyabiashara wengi wa bidhaa hizo ni watu wa imani yetu
 
Back
Top Bottom