Manispaa zetu zinapotuongezea mahandaki barabarani!!

Mzee wa Gumzo

Senior Member
Apr 21, 2008
197
5
Kwa wakazi wa Dar es Salaam na hususani wale wanaoitumia barabara ya Uhuru watakubaliana nami kuwa hiyo ni moja kati ya barabara mbaya sana Tanzania.Awali eneo lililokuwa baya lilikuwa kati ya amana hospitali na bungoni.Angalau kwa sasa mahadhaki yamepunguzwa japo kwa vifusi na kuchimbwa kwa greda.

Tatizo jingine kwenye barabara hii lipo kati ya buguruni malapa na sheli (Kobil Petrol station).Kwa muda mrefu eneo hilo limekuwa na mashimo madogomadogo njiani.Wiki tatu zilizopita manispaa husika ilituma watenda kazi wakiwa na mashine ndogongogo wakaanza kukata lami kwenye maeneo yaliyokuwa na mashimo.Hivi sasa ni wiki tatu zimepita tangu wakate lami kwa ajili ya kuziba mashimo lakini hakuna kilichofanyika.

Hivi sasa kama unaendesha ni afadhali usipite njia hiyo na kama upo kwenye daladala utaionea huruma gari la mwenzio.Ni mashimo makubwa yameachwa tena ni mabaya kwa usalama wa magari kwa kuwa walipokata yamekuwa makubwa na yana kingo zinazoharibu gari mara tairi linapoingia.

Madereva wanaotumia njia hiyo wanakwenda mwendo wa zig zag kukwepa mashimo yanayokwepeka japo ni kazi ngumu.

Najiuliza inakuwaje manispaa wakate lami kabla ya kujiandaa kuziba mashimo?HIvi kweli tunaowatendaji walio makini kwenye manispaa zetu? Ni utovu mkubwa wa nidhamu na udhaifu wa watendaji wetu pale wanapofanya jambo kwa kukurupuka pasipo kujipanga.

Sijui kama ni kila mtu analiona hili kuwa kero? au tushajichokea mwaego?
 
Usishangae ya barabara tu. Kila jambo la serikali linashangaza. Neno dharura au emergency halimo kabisa katika kamusi ya serikali. Muda mrefu sasa nawaza ivo kweli hawa watu haya hawayaoni au ndo dharau tu. Almuradi maisha yanakwenda. Angalia umuhimu wa traffic lights, hasa baada ya magari kuzidi kama yalivyo sasa. Ni kitu gani kinachosababisha taa isiwake. Labda bulb imeunguwa au waya zimechomoka. Serikali ndio ishindwe kweli. Kabla ya uhuru barabara nyingi kama si zote za Gerezani, Kariako Upanga na kwengineko zilikuwa na lami kamili. Imepotea hivi hivi wananchi wakilalamika na serikali ikifedheheka. Labda kabla tu ya uchaguzi ujao mambo yatakuwa mazuri. Vuta subra , sema Insha- Allah.
 
Hivi sasa kama unaendesha ni afadhali usipite njia hiyo na kama upo kwenye daladala utaionea huruma gari la mwenzio.Ni mashimo makubwa yameachwa tena ni mabaya kwa usalama wa magari kwa kuwa walipokata yamekuwa makubwa na yana kingo zinazoharibu gari mara tairi linapoingia.

Madereva wanaotumia njia hiyo wanakwenda mwendo wa zig zag kukwepa mashimo yanayokwepeka japo ni kazi ngumu.



One european behind the wheel was puzzled and asked something like "which side do you drive, on the right or left side of the road"?
Mwenyeji wake (mTZ) ambaye alikuwa kiti cha abiria akamjibu huku akionyesha kwa kidole, "...on the side where there are no pits" :)





.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom