SUPER PREDATOR
JF-Expert Member
- Apr 29, 2014
- 2,093
- 725
Toka nchi hii ipate Uhuru haijawahi kutokea CCM ikapata kipigo cha mtema kuni cha kupata kura chini ya 60% kama ilivyotokea mwaka huu, na haijawahi kutokea CCM kupoteza viti Vingi vya ubunge kama ilivyotokea mwaka huu, kutokana na kipigo hicho cha mtema kuni ruzuku ya CHADEMA itakaribiana sana na ya CCM. Sipendi kuzungumzia ya zanzibari maana nawajua CCM mtachukia.
Najua mtasingizia kuwa kipigo hicho kimetokana na viongozi wengi wa ngazi ya juu ya chama na serikali kuhamia ukawa, najua pia mtasingizia kuwa kipigo hicho kimetokana na upinzani kuanza kujitambua na kuanza kushirikiana, sasa pamoja na hayo yote nyie kama viongozi wa ngazi ya juu ya chama tunawaomba muondoke wenyewe kabla wananchi hatujaamua, na mkumbuke kwamba pamoja na kwamba nipo ukawa lakini ninaweza na nina haki ya kuhamia chama chochote, wakati wowote nikiona inafaa kufanya hivyo.
Kwahiyo ushauri huu muuchukulie kuwa unatoka kwa mwananchi ambaye anaweza kuwa mwanachama wa CCM muda wowote.
Cc; Lizaboni, FaizaFoxy na jingalao - kwa utekelezaji
Najua mtasingizia kuwa kipigo hicho kimetokana na viongozi wengi wa ngazi ya juu ya chama na serikali kuhamia ukawa, najua pia mtasingizia kuwa kipigo hicho kimetokana na upinzani kuanza kujitambua na kuanza kushirikiana, sasa pamoja na hayo yote nyie kama viongozi wa ngazi ya juu ya chama tunawaomba muondoke wenyewe kabla wananchi hatujaamua, na mkumbuke kwamba pamoja na kwamba nipo ukawa lakini ninaweza na nina haki ya kuhamia chama chochote, wakati wowote nikiona inafaa kufanya hivyo.
Kwahiyo ushauri huu muuchukulie kuwa unatoka kwa mwananchi ambaye anaweza kuwa mwanachama wa CCM muda wowote.
Cc; Lizaboni, FaizaFoxy na jingalao - kwa utekelezaji