NYAMKANG'ILI
JF-Expert Member
- Apr 1, 2012
- 223
- 112
Baadhi ya "maajabu" ya siasa za CCM ni:
1) Kabla ya uchaguzi wao CCM kufanyika, WAKATI WA MCHAKATO hakuna anayezungumzia rushwa na ufisadi, bila shaka ni kwa vile kila mmoja wao huwa anahonga (VIBARAKA, MAFISADI & MANABII 7 FEKI WA KUPINGA UFISADI), tofauti pekee ni viwango vya hongo kati yao, baadhi wanakusanya na kuhonga mabilioni na baadhi vijisenti. Baada ya zoezi la uchaguzi; wote washindi na washindwa hujitokeza na kulalama kuwa rushwa ilitawala - hili ni AJABU LA CCM
2) Mshitakiwa ndiye hakimu katika kesi yake. CCM kilimdhamini JK ili agombee urais TZ. CCM wakasaini naye mkataba, ilani ya uchaguzi. Vivyo JK anapokuja kwenye NEC, CC & MKUTANO MKUU ni sawa na mshitakiwa kufikishwa mbele ya JAJI (NEC, CC & MKUT MKUU) - JK anawekwa kitimoto, aeleze ametekeza vipi mkataba, ILANI. LAKINI hapa JK kwa siasa za CCM hugeuka na kuwa JAJI, basi hapo badala ya yeye kuhojiwa, yeye ndiye anayeanza kuwaweka kitimoto hao CC, NEC & MKUT MKUU. Baada ya vikao hivyo kuisha, utasikia BAADHI YAO (NAPE & KINANA) wanaanza ngwe ya kuzunguka nchi na "kuiagiza serikali kutekeleza ilani". Haya ni amaigizo, kwa sababu wa kuagiza ni JK na walikuwa naye "juzi" mbona hawakumuagiza, sasa KIGOMA WANAMUAGIZA NANI? - hili nalo ni AJABU LA CCM
3) AJABU kabambe, ni MANGULA kushindwa kuchaguliwa katika ngazi ya WILAYA kwamba hafai, alafu akachaguliwa kwa 100% katika ngazi ya TAIFA. Naamini hili ajabu linadhihirisha kwamba mgombea mmoja wa nafasi yoyote ni janga, kwa sababu naamini MANGULA angesimamishwa na yeyote kwenye u-makamu chair CCM asingeambaulia kitu - HILI NALO NI AJABU
KWA MUSTAKABALI wa TAIFA letu, tuungane kupambana na MAAJABU HAYA YA CCM, ni majanga
1) Kabla ya uchaguzi wao CCM kufanyika, WAKATI WA MCHAKATO hakuna anayezungumzia rushwa na ufisadi, bila shaka ni kwa vile kila mmoja wao huwa anahonga (VIBARAKA, MAFISADI & MANABII 7 FEKI WA KUPINGA UFISADI), tofauti pekee ni viwango vya hongo kati yao, baadhi wanakusanya na kuhonga mabilioni na baadhi vijisenti. Baada ya zoezi la uchaguzi; wote washindi na washindwa hujitokeza na kulalama kuwa rushwa ilitawala - hili ni AJABU LA CCM
2) Mshitakiwa ndiye hakimu katika kesi yake. CCM kilimdhamini JK ili agombee urais TZ. CCM wakasaini naye mkataba, ilani ya uchaguzi. Vivyo JK anapokuja kwenye NEC, CC & MKUTANO MKUU ni sawa na mshitakiwa kufikishwa mbele ya JAJI (NEC, CC & MKUT MKUU) - JK anawekwa kitimoto, aeleze ametekeza vipi mkataba, ILANI. LAKINI hapa JK kwa siasa za CCM hugeuka na kuwa JAJI, basi hapo badala ya yeye kuhojiwa, yeye ndiye anayeanza kuwaweka kitimoto hao CC, NEC & MKUT MKUU. Baada ya vikao hivyo kuisha, utasikia BAADHI YAO (NAPE & KINANA) wanaanza ngwe ya kuzunguka nchi na "kuiagiza serikali kutekeleza ilani". Haya ni amaigizo, kwa sababu wa kuagiza ni JK na walikuwa naye "juzi" mbona hawakumuagiza, sasa KIGOMA WANAMUAGIZA NANI? - hili nalo ni AJABU LA CCM
3) AJABU kabambe, ni MANGULA kushindwa kuchaguliwa katika ngazi ya WILAYA kwamba hafai, alafu akachaguliwa kwa 100% katika ngazi ya TAIFA. Naamini hili ajabu linadhihirisha kwamba mgombea mmoja wa nafasi yoyote ni janga, kwa sababu naamini MANGULA angesimamishwa na yeyote kwenye u-makamu chair CCM asingeambaulia kitu - HILI NALO NI AJABU
KWA MUSTAKABALI wa TAIFA letu, tuungane kupambana na MAAJABU HAYA YA CCM, ni majanga