ZeMarcopolo
Platinum Member
- May 11, 2008
- 14,017
- 7,220
Kwenye Siasa hakuna vitu vinavyotokea tu hivihivi. Kila jambo unaloliona ujue limepangwa.
Katika mazungumzo kati ya Ikulu na viongozi wa vyama vya siasa, Mangula alionekana tofauti kabisa na wengine wote waliohudhuria mkutano huo.
Yapasa kujiuliza kwanini Mangula alikuwa tofauti?
Jibu lake ni kwamba CCM inarudi kwa WATU. Watu wengi vijijini na mijini wanavaa kama jinsi alivyovaa Mangula leo. Kisiasa, mtu wa namna hiyo ni rahisi zaidi kuaminiwa na watu kuliko mtu aliyevaa suti.
Vazi la Mangula limeonyesha mwakilishi wa CCM ni mtu wa kawaida asiye na makuu. Hii picha inatuma ujumbe huo kwa watu.
Siasa ni taaluma. Tukumbushane tu kuwa Mangula alipata kuwa Mkuu wa Chuo Cha Siasa Kigamboni.
Be sure, Mangula anajua anachokifanya...