Mchambuzi
JF-Expert Member
- Aug 24, 2007
- 4,850
- 9,405
SEHEMU YA KWANZA
Mabadiliko ya uongozi ndani ya CCM yaliyotokea hivi karibuni yameleta matumaini kwa baadhi ya watanzania kwamba – ujio wa Mangula utarudisha imani na uhai wa CCM kwa umma wa Tanzania; Hizi ni habari njema, sio kwa CCM tu bali kwa wananchi wote, isipokuwa kama wanasiasa watapendelea tatizo la rushwa na ufisadi lisifikie kikomo kwa faida zao za kisiasa; Kwa maana nyingine – iwapo kuna wanasiasa ambao wanaopenda tatizo la rushwa liendelee ili walitumie kama Political Assest, na kulifanya liwe Political Liability kwa mahasimu wao kuelekea uchaguzi mkuu wa 2015; Hapa nazungumzia viongozi wa vyama vyote yani CCM ambao mtaji wao wa siasa ni uwepo wa rushwa na ufisadi, lakini vile vile viongozi wa Chadema ambao wamewekeza zaidi kwenye suala la rushwa na Ufisadi, kama njia ya kuelekea ikulu 2015; Pia ningependa kusema kwamba inavunja sana moyo kuona kwamba matumaini ya watanzania katika kutokomeza ufisadi yanawekwa kwa Kinana na Mangula badala ya vyombo vilivyoundwa na vinavyoendeshwa na fedha za walipa kodi, hasa TAKUKURU;
Majibizano ya hivi karibuni baina ya Katibu Mkuu wa Chadema Dr. Slaa na Makamu Mwenyekiti wa CCM Taifa (Bara) Philip Mangula juu ya rushwa nchini, kwa bahati mbaya sana, yameegemea zaidi juu ya rushwa katika siasa na sio rushwa kwa ujumla; Pia, ni bahati mbaya kwamba majibizano baina ya viongozi hawa yanalenga zaidi juu ya nani na chama gani kina Moral Authority zaidi ya kuzungumzia vita dhidi ya Rushwa na Ufisadi, badala ya mjadala wao kuonyesha angalau dalili kwamba consensus baina ya vyama hivi viwili inaweza kupatikana ili ufumbuzi upatikane, na ushindani wa siasa uendelee katika maeneo mengine muhimu ambayo bado yanasubiri kutatuliwa; Kwa sasa ni kama vile kila upande unamwombea mwenzake asifanikiwe katika vita dhidi ya ufisadi; Kama baadhi yenu mtakubaliana na mimi katika hili, basi kuna ulakini kwamba vyama vyote viwili vinapigana dhidi ya vita hivi kwa maslahi ya taifa;
Kinachozidi kuwa dhahiri ni kwamba, kwa sasa, kila upande unaweka jitiada kuhakikisha kwamba kuelekea 2015, suala la Rushwa linakuwa more of POLITICAL ASSET kwa upande mmoja, na kwa upande mwingine, suala la rushwa liwe more of POLITICAL LIABILITY, bila ya kujali sana juu ya equilibrium kwa wananchi; Huku sio kutatua tatizo la rushwa bali kulitumia kwa madhumuni ya Kisiasa; Ni muhimu tujikumbushe kwamba Rushwa ni suala la Kijamii, na inapoingia Siasa, ni katika kulitatua tu, vinginevyo katika kulielewa, hatuhitaji siasa au itikadi za vyama bali mchakato unaoanza Kijamii;
Mjadala wangu umegawanyika katika sehemu kuu TANO kama ifuatavyo:
Sehemu ya KWANZA ni Hotuba ya Mwalimu Nyerere (1962) juu ya "Rushwa ni Adui wa WATU"; Hii ni tofauti na dhana ya Rushwa ni Adui wa HAKI; Hotuba hii ya Mwalimu itatusaidia kuweka mjadala wetu katika muktadha husika;
Sehemu ya PILI, nitajadili dhana ya ‘STATE', na kufanya uchambuzi juu ya chimbuko lake, madhumuni yake, changamoto zake, na masuala mengine muhimu ambayo yamechangia Tanzania kuwa a Problematic State; Ni kutokana na kuwa a Problematic State, tatizo la rushwa na ufisadi limeota mizizi mirefu nchini;
Sehemu ya TATU, nitajadili aina kuu mbili za rushwa Tanzania – ya kwanza ikiwa ni ile itokanayo na rogue individuals na aina ya pili ikiwa ni ile ya kimfumo; Aina hii ya pili ndio tatizo kubwa kwa maana ya kwamba ndio inayozaa UFISADI; Na rushwa ya kimfumo Tanzania ni suala ambalo jamii inalikubali (ingawa not officially); Nitalifafanua hili huko mbeleni;
Sehemu ya NNE, nitajadili kwa undani zaidi kwanini nasema Ufisadi Tanzania unakubalika, hasa kwa kujadili na kufafanua hoja yangu kwa kutumia framework ya ECONOMY OF AFFECTION/Uchumi wa Mahaba, ambao Kiuchumi, ndio mfumo mkubwa na ulio rasmi Tanzania kuliko UCHUMI Unaofuata RATIONAL BEHAVIOUR AND CHOICE; Pia katika muktadha huu, nitajadili masuala ya Social and Economic Exchanges/Mfumo wa ubadilishanaji Kiuchumi na Kijamii nchini, ambao umetawaliwa zaidi na informal processes and institutions, na jinsi gani masuala haya kwa pamoja yanachochea na ku ‘entertain' rushwa na ufisadi;
Sehemu ya TANO NA MWISHO, nitajadili mapendekezo juu ya nini kifanyike kutatua tatizo la Ufisadi Tanzania, pamoja na changamoko zilizopo; Ni imani yangu kwamba mwisho wa siku, tutapata angalau mwanga kidogo juu ya jinsi gani Rushwa na Ufisadi ni masuala yasiyokuwa na Itikadi, lakini muhimu zaidi, kwanini itakuwa ni kwa manufaa ya wananchi iwapo tutafanikiwa kuacha kutumia suala la Ufisadi kama mtaji wa Kisiasa; Nina amini kabisa kwamba kama kuna POLITICAL WILL ambayo inaweka UZALENDO KWANZA, SIASA BAADAE, Suala la Ufisadi linaweza kutatuliwa na Chadema na CCM amicably; Vinginevyo kwa chama kimoja kung'ang'ania Ufisadi kama agenda yake kuu katika ushindani ndani wa demokrasia ya uliberali ni ushahidi tosha jinsi gani chama husika kwanza kipo vulnerable lakini pia immature in political competition;
Hoja ya msingi hapa ni kwamba, inabidi tukifie sehemu tumalize tatizo la rushwa amicably na tuhamishie ushindani wetu wa kisiasa kwenye masuala mengine muhimu kama inavyotokea katika demokrasia zilizokomaa; Hivyo ndivyo Chadema kwa mfano itaendelea kuwa relevant katika Siasa za Tanzania kwani, Bila Chadema Madhubuti, CCM Makini Haiwezekani; Huu ni ukweli ambao hautabadilika, at least not in the short to medium term;
Mtaniwia radhi kwamba kuna baadhi ya sehemu nitatumia lugha ya kiingereza, lakini nia yangu ni kujaribu nisipoteze maana na uzito halisi wa neno, maneno au ujumbe husika; Kwa vile wadau wengi huwa wanashauri nisiandike makala ndefu sana, bandiko langu la kwanza litahusiana na Hotuba ya Mwalimu Nyerere, halafu sehemu nyingine za mjadala zitafuata katika mabandiko mengine;
Mwalimu Nyerere (1962): Uhuru na Umoja, Sura ya 17
["…there is another enemy which we must add on the list of these enemies poverty, disease and ignorance; I think we must add another enemy; Let us face it, we can talk of all this idealistic nonsense about the right of the people to govern themselves and all that; You establish a Government of the People; They have Hopes, and during the whole struggle of the nationalist movement we have been raising the expectations of our people; They have been expecting a Government which is going to lift their standard of living; How? Raising Taxes, using them to wage this war; they expect they are going to have a Government which is going to be determined to see that Justice is done in this country;
What is the enemy of that? What is the enemy of this expectation? Not Merely Poverty; We can do something about poverty; Not Disease, we can do something about Diseases as long as honest men are carrying out the job; Not ignorance, we know that enemy too, we know we don't want people who are ignorant; But if our people cannot have Absolute Confidence in their Government, in the people to who they have entrusted their welfare, how sir are you going to wage this silly war against poverty, disease and ignorance? You have got to have people with confidence in their own government and when I say in their own government I don't mean in a few Ministers sitting somewhere around a Council of ministers, I mean every man and woman in the country who is in the position of responsibility, in local government, in the trade unions, in the cooperative unions, in the political movement, and in the central government itself;
Now Sir, I think we should be less than honest if I said that all is well, because it is not; There is corruption; Now Sir, I think corruption must be treated with ruthless because I believe myself corruption and bribery is a greater enemy to the welfare of a people in peacetime than war; I believe myself corruption is a country should be treated as a treason; If people cannot have confidence in their own government, if people can feel that justice can be bought, then what hope are you leaving with the people? The only thing they can do is to take up arms and remove that silly government; They have no other hope; I feel sir, as we move, as we move forward, and we are going to wage this war against poverty, disease and ignorance, we have got to have the confidence of the people; We have got to have people in local government, in the trade unions, in the cooperative movement, in political organizations, in the Civil service and in the government itself, in whom our own people have absolute confidence; If we can't have it then I cannot see how the people of Tanganyika are going to get the true benefits of independence for which they have been struggling;"].
Hapa ningependa kujadili kidogo hoja ya mbili za Mwalimu ambazo nadhani ni muhimu; Ya Kwanza:
"You have got to have people with confidence in their own Government and when I say in their own government I don't mean in a few Ministers sitting somewhere around a Council of ministers";
Hapa Mwalimu anatukumbusha kwamba, iwapo CCM inadhania mtaji wake wa kisiasa 2015 ni kusimisha Waziri fulani kwa imani kwamba jamii inaona hana madoa ya Ufisadi, hivyo kufaa kupeperusha bendera ya CCM Uchaguzi Mkuu 2015, kufanya hivyo ni kujidanganya kwani mafanikio ya mkakati huo yatakuwa ni ya muda mfupi sana, kwani bado tatizo la msingi litakuwa limebadkia intact;Nitajadili hili na mengine mengi kwa undani zaidi baadae;
Hoja ya Pili muhimu ya Mwalimu:
"If people cannot have confidence in their own government, if people can feel that justice can be bought, then what hope are you leaving with the people? The only thing they can do is to take up arms and remove that silly government"
Umuhimu wa hoja hii ni kwamba, bila ya umakini wa Chadema, hata ikiingia Ikulu 2015, haitakuwa ajabu kwa serikali yake kujikuta katika mazingira ya kuwa a 'silly government' anayozungumzia Mwalimu; Hii ni kutokana na jinsi suala la Ufisadi linavyoendeshwa katika muktadha wa POLITICAL ASSET & LIABILITY baina ya CCM na Chadema, bila ya vyama vyote viwili kujali sana juu ya EQUILIBRIUM kwa umma, from the process; Hili ni moja ya maeneo ya msingi katika hoja yangu ambalo pia nitalijadili kwa undani zaidi baadae...
SEHEMU YA PILI INAENDELEA HAPA - https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...angamoto-za-ufisadi-tanzania.html#post5141440