Mangula: CCM haitakiwi kutoa maoni

R.B

JF-Expert Member
May 10, 2012
6,296
2,573
[h=1]
mangula.jpg
[/h]
Philip Mangula.





Makamu Mwenyekiti wa CCM Taifa, Philip Mangula amesema viongozi wa chama hicho hawatakiwi kuichambua rasimu ya katiba mpya na kutoa maoni binafsi na badala yake wataitembeza rasimu hiyo kwa wanachama ili waikosoe.

“Unajua sisi ni viongozi na hatutakiwi kutoa maoni binafsi, sisi tunawawakilisha wananchi ambao ni wanachama wa CCM, tutawaplekea hao ili watoe maoni yao” alisema Mangula.

Alisema ni vigumu kwa kikao kimoja cha Kamati Kuu ya CCM kutoa maoni kwa sababu hao ni wawakilishi tu wa chama, hivyo wanachama wote wa chama hicho watapelekewa rasimu wakaichambue ndipo chama kitatoa msimamo wake.

“Sisi viongozi hatutoi maoni tutaipeleka rasimu kwa wanachama wetu zaidi ya 6,000 tuyasikie wanayosema, kwa sababu hao ndiyo wananchi” alisema Mangula Waziri wa Sheria na Katiba, Mathias Chikawe alizungumza na gazeti hili na kusema kuwa ni vyema kama wananchi ambao CCM inawawakilisha wakatoa maoni kuhusu rasimu hiyo, ingawa nao viongozi wanaweza kuchangia maoni yao kama wananchi wa kawaida.

Akichambua baadhi ya vipengele vya rasimu hiyo, Chikawe alisema haoni kama ni vyema katiba kuruhusu wananchi kumvua ubunge, mbunge ambaye hajatimiza wajibu wake kwani hali hiyo itazua vurugu na fitina. Alisema kwa kuwa siasa unafananishwa na mchezo mchafu, wapinzani wa ndani ya chama wanaweza kufanya fitina na mbunge aliye madarakani kung’olewa pengine bila hata makosa.
 
Kuweka madarakani iwe poa ...na kumvua madaraka iwe fitina!!!??? hapo sijamwelewa huyu kiombee,
 
Ni kweli CCM haitakiwi kutoa maoni kwa sababu suala la katiba mpya halipo ndani ya ilani yenu ya uchaguzi wala si sera ya CCM kuwa na serikali tatu!
 
Na kwanini waipeleke kwa mtazamo wa kichama? Mi nadhani waipeleke kwa WANANCHI wote kwani hiyo si rasimu ya katiba ya chama ni ya Taifa! Kama ndiyo hivyo, basi kila chama kipeleke kwa wanachama wake ili waipitie na kutoa maoni.

Mangula amepoteza mwelekeo baada ya kukuta magamba yamekwisha kuwa magumu kuyang'oa sasa anatafuta pa kushika!
 
Aden Rage mbunge wa Tabora mjini siyo lazima kabisa amalize mda wake anabebwa tu na katiba ya sasa.
 
Viongozi wa ccm wameigiwa na hofu katika katiba mpya kwanza ni hili la kuzowea kuona na kujisahau kuhisi ccm ndio Serekali na ndio yenye mamuzi yote hata mtu akifuja basi hufunikwa na mwevuli wa Chama.Sasa hivi sasa wameshtuka katika usingizi mnono bada kumuona Mh Warioba Kaja na Nyundo . Lakwanza ni hili la kuzowea kuichezea chezea Serekali watakavyo ccm a. b. ni hili la Mbunge akifuja katika jimbo lake wananchi wana haki ya kumngowa asiendelee kufuja. Mimi nashangazwa na hawa ccm?. Ni chama chao tu kilicho kata haya na Hata kuweko kwa serekali ya Tanganyika wamekataa sasa tuwafahamu vipi hawa mafisadi?
 
Huyo dingi hana jipya, bora aendelee kula Honeymoon yake.
WanaCCM wengi walidhani ana jipya kumbe ni mwepesi kuliko Mukama.
Alisema atawafukuza mafisadi wote ndani ya miezi sita, muda umekwisha na hakuna aliyefukuzwa wala kuonywa.
Namshauri aende akawape Feedback wanaCCM kuhusu mpango wake wa kuwafukuza mafisadi umefikia wapi ndani ya CCM.

Poor Mangula, Poor CCM!!!
 
Je umewahi kusikia, timu yenu, kiwanja chenu, refa wenu, washabiki wenu, lakini bado kombe likachukuliwa mikononi mwenu? Mtajisikiaje. Tume wachague wajumbe wao wenyewe, Hoja ya Katiba Mpya haikuwa yao wakachakachua kutoka kwa CHADEMA, Tume imetoa maoni kutoka kwa wananchi sasa iweje CCM inalia na kuweweseka hivyo? Kwani zile pongezi, majivuno na mbwembwe za kuwa CCM ina wajumbe kwenye mabaraza ya kata zaidi ya asilimia 90% zimepotelea wapi?

Kama alivyotwambia NAPE kwamba chama chao kina wanachama zaidi ya milioni 6 na ambao ndio wametoa maoni ya serikali tatu sasa wasiwasi wa Kinana unatoka wapi?
 
One cannot dare to cut down a tree on which s/he sits on unless demonstrates a planned suicide!
 
Back
Top Bottom