Rais Samia awasili Marekani leo Sept 19, 2021 kuhudhuria Mkutano wa 76 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UN)

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,802
11,961
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa JF Kenedi Jijini New York Marekani leo Sept 19,2021 kwa ajili ya kuhudhuria mkutano wa 76 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa UN unaotarajiwa kufanyika tarehe 23 Sept 2021.

RAIS Samia Suluhu Hassan yupo New York nchini Marekani kuhudhuria Mkutano wa 76 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UN).

Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu ilisema pia kwamba Septemba 23, mwaka huu Rais Samia anatarajiwa kulihutubia Baraza hilo la UN.

Pamoja na mkutano huo, taarifa ilisema kwamba Rais Samia pia atahudhuria mikutano ya kilele ya kujadili masuala ya mabadiliko ya tabianchi, usalama wa chakula na utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs).

Aidha, Rais Samia anatarajiwa pia kukutana na wakuu wa nchi nyingine na viongozi wa mashirika ya kimataifa kwa lengo la kuimarisha ushirikiano na uhusiano baina ya Tanzania na nchi hizo pamoja na mashirika hayo.

1632065617705_3.jpg
1632065619611_4.jpg
 
Mbona hatujaonyeshwa akishuka kweny ndege tujue ameenda na dreamliner yetu au amekodi nyingn
 
Mwanampotevu akiamua kurejea ni vyema kumpokea kwani atakuwa amejutia kwa aliyoyafanya maana hata passport hajapata mpaka leo, ni ngumu kushindana na serikali.
 
Mange alikua anaandamana ama alipanga kukutana?

Naona wote waliokua wanampinga na kumtukana Magufuli sasa wanajipendekeza kwa mama wapate kuteuliwa, tusubiri tuone.

Hivi polisi wa New York wanaruhusiwa kumsogelea rais wetu kiasi hicho na Bunduki nje nje?
 
Mange alimshambulia sana Magufuli hadi kuutweza utu wake leo anatambulishwa kama mtoto wa Mama.

Mama alituambia yeye na Magufuli ni kitu kimoja, mimi nasema kwa haya Mama na Magufuli sio kitu kimoja tusidanganyane.

Tutaona rangi ya kila mmoja muda si mrefu



Sent from my TECNO P704a using JamiiForums mobile app
 
Ulinzi kwa Rais wetu haujaniridhisha, Mange is like a stranger how comes anamsogelea Rais karibu kiasi hicho? japo nimeuona mkono wa askari ukimzuia na Samia alivyoweka mikono yake pia ni kama anajilinda, lakini hiyo pekee kwangu haitoshi, next time ulinzi wa Rais wa nchi uimarishwe asisogelewe sana na raia wa kawaida.
 
Back
Top Bottom