BungelaKatiba2014tz
JF-Expert Member
- Feb 18, 2014
- 1,231
- 648
Maneno mbofumbofu kuhusu Dangote Cement yanaandikwa na watu wenye matatizo na serikali.
Hayo yamesemwa na Mwakilishi Mkazi wa Dangote nchini Tanzania, Bi Esther Baruti wakati akihojiwa na Radio Sauti ya Amerika.
Amefafanua kuwa kiwanda hakijafungwa, bali kimesimamisha uzalishaji kwa muda. Na kwamba hii si mara ya kwanza kwa kiwanda hicho kusimamisha uzalishaji.
Amesema kuwa Dangote alipewa kila kitu alichoomba. Alipewa ardhi bure, msamaha wa kodi kwa kila kitu alicholeta kwa ajili ya kiwanda; ana msamaha wa kodi kwa mafuta ya dizeli. Na amepewa vibali vya kutosha kuajiri wataalam wa kigeni.
Anasema pia Dangote Cement ina mwakilishi katika kamati ya kitaifa ya gesi na makaa ya mawe. Na kwamba kampuni hiyo imenunua tani milioni tano za makaa ya mawe ya Tanzania.
Amesema uzalishaji umesimama kutokana na matatizo ya kiufundi ambayo yanashughulikiwa. Na kwamba wanaosambaza maneno mabaya ni watu wa kati ambao wanataka kuizuia Dangote Cement gesi badala ya TPDC. C&P
Hayo yamesemwa na Mwakilishi Mkazi wa Dangote nchini Tanzania, Bi Esther Baruti wakati akihojiwa na Radio Sauti ya Amerika.
Amefafanua kuwa kiwanda hakijafungwa, bali kimesimamisha uzalishaji kwa muda. Na kwamba hii si mara ya kwanza kwa kiwanda hicho kusimamisha uzalishaji.
Amesema kuwa Dangote alipewa kila kitu alichoomba. Alipewa ardhi bure, msamaha wa kodi kwa kila kitu alicholeta kwa ajili ya kiwanda; ana msamaha wa kodi kwa mafuta ya dizeli. Na amepewa vibali vya kutosha kuajiri wataalam wa kigeni.
Anasema pia Dangote Cement ina mwakilishi katika kamati ya kitaifa ya gesi na makaa ya mawe. Na kwamba kampuni hiyo imenunua tani milioni tano za makaa ya mawe ya Tanzania.
Amesema uzalishaji umesimama kutokana na matatizo ya kiufundi ambayo yanashughulikiwa. Na kwamba wanaosambaza maneno mabaya ni watu wa kati ambao wanataka kuizuia Dangote Cement gesi badala ya TPDC. C&P