Maneno mazito kutoka kada wa CCM ndugu Bollen Ngetti

COARTEM

JF-Expert Member
Nov 26, 2013
3,596
3,639
Ameandika Kada wa CCM #Bollen_Ngetti

KAMA madai ya Lissu yatathibitika pasipo kuacha shaka nitahitimisha kwa imani kwamba Makao Makuu ya Mamlaka ya Shetani yako Tanzania na mawakala wake! Nitaamini kuwa Mhimili wa Ibilisi unafanya kazi duniani kutokea Tanzania. Lakini pia nitatamatisha maandiko haya kwa kuamini kuwa Tanzania si sehemu salama tena kuishi binadamu wanaomcha Mungu.

Ni hivi: Tundu Lisu anasema anajua waliomshambulia kwa mabunduki. Anajua walioketi kitako na kujadili, kutafakari, kupanga, kuratibu na kugharamia "mauaji" yake September 7, 2017 saa Saba mchana.

Lissu anasema mpango uliokuwepo ni kwamba baada ya kuuawa kwa risasi ilitakiwa mwili wake ukimbizwe kijijini Ikungi-Singida kwa maziko ya haraka maana "mwili umeharibika sana" na ndio sababu ya kumshambulia kwa risasi nyingi ili mwili uharibike.

Mradi huo wa mauti ulipangwa mwili wa Lissu usipewe heshima yoyote ya kibunge Dodoma na wala usipelekwe Dar kwenye makazi yake. Lissu anasema hata watoto wake (twins) wasingeuona mwili wa baba yao maana "umeharibika sana."

Haya maneno ya Lissu ni mazito mno. Yanaonesha jinsi wauaji walivyokuwa na chuki iliyovuka mawingu. Chuki mpaka na mwili wa marehemu. Hii si chuki na hasira ya kawaida.

Mtu pekee aliyewahi kukutana na chuki ya aina hii ni Samwel Doe wa Liberia (naweza kusahihishwa) aliyepigwa risasi 32 na Kisha kuvuliwa nguo zake na mwili wake kukokotwa na ng'ombe huku kamba ikiwa imefungwa kwenye uume wake zoezi iliyoisha baada ya uume huo kukatika! Kwa maelezo ya Lissu ni kwamba "wasiojulikana" walikuwa tayari kudhalilisha mwili wa Lissu maana risasi 38 za nini? Ndio maana hata DC Sarah Msafiri wa Kigamboni anashangaa!

Ni matumaini Lissu hatimaye apate nafasi ya kuthibitisha maneno yake haya ili tujue uongo na ukweli wake. Hii ni chuki isiyo ya kawaida kiasi cha kujiuliza kwa nini "wasiojulikana" wasiwe na "Plan B?" Ni kwa namna gani Lissu amehakikishiwa usalama wake dhidi ya watu waliokuwa na chuki kiwango hiki? Wanaosema "Lissu Rudi nyumbani" mbona hawasemi kuhusu usalama wake? Hivi tunajua kaburi lake lingeota nyasi na kusahaulika? Kwa tumpoteze mtu muhimu kama huyu katika medani ya sheria?

Kila ninapotafakari "kifo" cha Lissu napata taabu sana kuamini kama kweli kilipangwa na Watanzania wenzetu hawa wanaokwenda kanisani na msikitini au ni mashetani yaliyoletwa mawimbi ya bahari kutoka nchi za mbali? Ni dhahiri ndio sababu Mungu aliacha kuwatuma malaika kumuokoa Lissu na badala yake akaingilia Kati yeye mwenyewe mzima mzima. Hakika Mungu yupo na Yu Hai!

Ndio maana kila hoja inayoletwa dhidi yake hupotea na kuyeyuka kama umande na hatujiulizi kwa nini? Jibu ni moja tu, Lissu yuko mikononi mwa Allah! Ilianza ushoga ikapotea, ikaja anatumiwa na mabeberu ikapotea, ikaja anachafua nchi ikapotea, ikaja anahaini Serikali ikapotea, ikaja anaomba-omba Ulaya ikapotea, sasa eti ni mzembe na mzururaji hivyo akamatwe nayo imeshapita kushoto. Lisu ana nini? Mungu!

Kwa kuwa ni Mungu amekataa Lissu asife ni vizuri tukasubiri kuona nini makusudi ya Mungu kwake hadi amtake kuwa hai? Mbona wengine risasi moja tu mguuni hufa?

Tumpe Mungu nafasi ashughulike na Lissu inaweza akawa ni Joshua wa kutuvusha ng'ambo! Tumuombee afya njema anaporudi kufanyiwa operesheni ya mwisho. Mungu ni mwema!

#AchaWoga2020
@Bngetti2019

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ameandika Kada wa CCM #Bollen_Ngetti

KAMA madai ya Lissu yatathibitika pasipo kuacha shaka nitahitimisha kwa imani kwamba Makao Makuu ya Mamlaka ya Shetani yako Tanzania na mawakala wake! Nitaamini kuwa Mhimili wa Ibilisi unafanya kazi duniani kutokea Tanzania. Lakini pia nitatamatisha maandiko haya kwa kuamini kuwa Tanzania si sehemu salama tena kuishi binadamu wanaomcha Mungu.

Ni hivi: Tundu Lisu anasema anajua waliomshambulia kwa mabunduki. Anajua walioketi kitako na kujadili, kutafakari, kupanga, kuratibu na kugharamia "mauaji" yake September 7, 2017 saa Saba mchana.

Lissu anasema mpango uliokuwepo ni kwamba baada ya kuuawa kwa risasi ilitakiwa mwili wake ukimbizwe kijijini Ikungi-Singida kwa maziko ya haraka maana "mwili umeharibika sana" na ndio sababu ya kumshambulia kwa risasi nyingi ili mwili uharibike.

Mradi huo wa mauti ulipangwa mwili wa Lissu usipewe heshima yoyote ya kibunge Dodoma na wala usipelekwe Dar kwenye makazi yake. Lissu anasema hata watoto wake (twins) wasingeuona mwili wa baba yao maana "umeharibika sana."

Haya maneno ya Lissu ni mazito mno. Yanaonesha jinsi wauaji walivyokuwa na chuki iliyovuka mawingu. Chuki mpaka na mwili wa marehemu. Hii si chuki na hasira ya kawaida.

Mtu pekee aliyewahi kukutana na chuki ya aina hii ni Samwel Doe wa Liberia (naweza kusahihishwa) aliyepigwa risasi 32 na Kisha kuvuliwa nguo zake na mwili wake kukokotwa na ng'ombe huku kamba ikiwa imefungwa kwenye uume wake zoezi iliyoisha baada ya uume huo kukatika! Kwa maelezo ya Lissu ni kwamba "wasiojulikana" walikuwa tayari kudhalilisha mwili wa Lissu maana risasi 38 za nini? Ndio maana hata DC Sarah Msafiri wa Kigamboni anashangaa!

Ni matumaini Lissu hatimaye apate nafasi ya kuthibitisha maneno yake haya ili tujue uongo na ukweli wake. Hii ni chuki isiyo ya kawaida kiasi cha kujiuliza kwa nini "wasiojulikana" wasiwe na "Plan B?" Ni kwa namna gani Lissu amehakikishiwa usalama wake dhidi ya watu waliokuwa na chuki kiwango hiki? Wanaosema "Lissu Rudi nyumbani" mbona hawasemi kuhusu usalama wake? Hivi tunajua kaburi lake lingeota nyasi na kusahaulika? Kwa tumpoteze mtu muhimu kama huyu katika medani ya sheria?

Kila ninapotafakari "kifo" cha Lissu napata taabu sana kuamini kama kweli kilipangwa na Watanzania wenzetu hawa wanaokwenda kanisani na msikitini au ni mashetani yaliyoletwa mawimbi ya bahari kutoka nchi za mbali? Ni dhahiri ndio sababu Mungu aliacha kuwatuma malaika kumuokoa Lissu na badala yake akaingilia Kati yeye mwenyewe mzima mzima. Hakika Mungu yupo na Yu Hai!

Ndio maana kila hoja inayoletwa dhidi yake hupotea na kuyeyuka kama umande na hatujiulizi kwa nini? Jibu ni moja tu, Lissu yuko mikononi mwa Allah! Ilianza ushoga ikapotea, ikaja anatumiwa na mabeberu ikapotea, ikaja anachafua nchi ikapotea, ikaja anahaini Serikali ikapotea, ikaja anaomba-omba Ulaya ikapotea, sasa eti ni mzembe na mzururaji hivyo akamatwe nayo imeshapita kushoto. Lisu ana nini? Mungu!

Kwa kuwa ni Mungu amekataa Lissu asife ni vizuri tukasubiri kuona nini makusudi ya Mungu kwake hadi amtake kuwa hai? Mbona wengine risasi moja tu mguuni hufa?

Tumpe Mungu nafasi ashughulike na Lissu inaweza akawa ni Joshua wa kutuvusha ng'ambo! Tumuombee afya njema anaporudi kufanyiwa operesheni ya mwisho. Mungu ni mwema!

#AchaWoga2020
@Bngetti2019

Sent using Jamii Forums mobile app
Mmmh ayaa ngoja miungu ya baali ije tuskie na wao wanasemaje

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ameandika Kada wa CCM #Bollen_Ngetti

KAMA madai ya Lissu yatathibitika pasipo kuacha shaka nitahitimisha kwa imani kwamba Makao Makuu ya Mamlaka ya Shetani yako Tanzania na mawakala wake! Nitaamini kuwa Mhimili wa Ibilisi unafanya kazi duniani kutokea Tanzania. Lakini pia nitatamatisha maandiko haya kwa kuamini kuwa Tanzania si sehemu salama tena kuishi binadamu wanaomcha Mungu.

Ni hivi: Tundu Lisu anasema anajua waliomshambulia kwa mabunduki. Anajua walioketi kitako na kujadili, kutafakari, kupanga, kuratibu na kugharamia "mauaji" yake September 7, 2017 saa Saba mchana.

Lissu anasema mpango uliokuwepo ni kwamba baada ya kuuawa kwa risasi ilitakiwa mwili wake ukimbizwe kijijini Ikungi-Singida kwa maziko ya haraka maana "mwili umeharibika sana" na ndio sababu ya kumshambulia kwa risasi nyingi ili mwili uharibike.

Mradi huo wa mauti ulipangwa mwili wa Lissu usipewe heshima yoyote ya kibunge Dodoma na wala usipelekwe Dar kwenye makazi yake. Lissu anasema hata watoto wake (twins) wasingeuona mwili wa baba yao maana "umeharibika sana."

Haya maneno ya Lissu ni mazito mno. Yanaonesha jinsi wauaji walivyokuwa na chuki iliyovuka mawingu. Chuki mpaka na mwili wa marehemu. Hii si chuki na hasira ya kawaida.

Mtu pekee aliyewahi kukutana na chuki ya aina hii ni Samwel Doe wa Liberia (naweza kusahihishwa) aliyepigwa risasi 32 na Kisha kuvuliwa nguo zake na mwili wake kukokotwa na ng'ombe huku kamba ikiwa imefungwa kwenye uume wake zoezi iliyoisha baada ya uume huo kukatika! Kwa maelezo ya Lissu ni kwamba "wasiojulikana" walikuwa tayari kudhalilisha mwili wa Lissu maana risasi 38 za nini? Ndio maana hata DC Sarah Msafiri wa Kigamboni anashangaa!

Ni matumaini Lissu hatimaye apate nafasi ya kuthibitisha maneno yake haya ili tujue uongo na ukweli wake. Hii ni chuki isiyo ya kawaida kiasi cha kujiuliza kwa nini "wasiojulikana" wasiwe na "Plan B?" Ni kwa namna gani Lissu amehakikishiwa usalama wake dhidi ya watu waliokuwa na chuki kiwango hiki? Wanaosema "Lissu Rudi nyumbani" mbona hawasemi kuhusu usalama wake? Hivi tunajua kaburi lake lingeota nyasi na kusahaulika? Kwa tumpoteze mtu muhimu kama huyu katika medani ya sheria?

Kila ninapotafakari "kifo" cha Lissu napata taabu sana kuamini kama kweli kilipangwa na Watanzania wenzetu hawa wanaokwenda kanisani na msikitini au ni mashetani yaliyoletwa mawimbi ya bahari kutoka nchi za mbali? Ni dhahiri ndio sababu Mungu aliacha kuwatuma malaika kumuokoa Lissu na badala yake akaingilia Kati yeye mwenyewe mzima mzima. Hakika Mungu yupo na Yu Hai!

Ndio maana kila hoja inayoletwa dhidi yake hupotea na kuyeyuka kama umande na hatujiulizi kwa nini? Jibu ni moja tu, Lissu yuko mikononi mwa Allah! Ilianza ushoga ikapotea, ikaja anatumiwa na mabeberu ikapotea, ikaja anachafua nchi ikapotea, ikaja anahaini Serikali ikapotea, ikaja anaomba-omba Ulaya ikapotea, sasa eti ni mzembe na mzururaji hivyo akamatwe nayo imeshapita kushoto. Lisu ana nini? Mungu!

Kwa kuwa ni Mungu amekataa Lissu asife ni vizuri tukasubiri kuona nini makusudi ya Mungu kwake hadi amtake kuwa hai? Mbona wengine risasi moja tu mguuni hufa?

Tumpe Mungu nafasi ashughulike na Lissu inaweza akawa ni Joshua wa kutuvusha ng'ambo! Tumuombee afya njema anaporudi kufanyiwa operesheni ya mwisho. Mungu ni mwema!

#AchaWoga2020
@Bngetti2019

Sent using Jamii Forums mobile app
Inauma Sana kuona binadamu anamchukia mwenzake Tena kwa kiwango Cha kumuua kifo Cha mateso na ukatili hivi
Humo wapo Wakristu pia wapo Waislamu hao ndo watu waendao msikitini na kanisani kila siku za ibada zifikapo
Daaaaah, Mungu tusaidie tuishi kwa wema, haki na usdilifu daima!!! TU MAVUMBI NA MAVUMBINI TUTARUDI!!!

Daima toa bila kukumbuka na Pokea bila kusahau
 
Ameandika Kada wa CCM #Bollen_Ngetti

KAMA madai ya Lissu yatathibitika pasipo kuacha shaka nitahitimisha kwa imani kwamba Makao Makuu ya Mamlaka ya Shetani yako Tanzania na mawakala wake! Nitaamini kuwa Mhimili wa Ibilisi unafanya kazi duniani kutokea Tanzania. Lakini pia nitatamatisha maandiko haya kwa kuamini kuwa Tanzania si sehemu salama tena kuishi binadamu wanaomcha Mungu.

Ni hivi: Tundu Lisu anasema anajua waliomshambulia kwa mabunduki. Anajua walioketi kitako na kujadili, kutafakari, kupanga, kuratibu na kugharamia "mauaji" yake September 7, 2017 saa Saba mchana.

Lissu anasema mpango uliokuwepo ni kwamba baada ya kuuawa kwa risasi ilitakiwa mwili wake ukimbizwe kijijini Ikungi-Singida kwa maziko ya haraka maana "mwili umeharibika sana" na ndio sababu ya kumshambulia kwa risasi nyingi ili mwili uharibike.

Mradi huo wa mauti ulipangwa mwili wa Lissu usipewe heshima yoyote ya kibunge Dodoma na wala usipelekwe Dar kwenye makazi yake. Lissu anasema hata watoto wake (twins) wasingeuona mwili wa baba yao maana "umeharibika sana."

Haya maneno ya Lissu ni mazito mno. Yanaonesha jinsi wauaji walivyokuwa na chuki iliyovuka mawingu. Chuki mpaka na mwili wa marehemu. Hii si chuki na hasira ya kawaida.

Mtu pekee aliyewahi kukutana na chuki ya aina hii ni Samwel Doe wa Liberia (naweza kusahihishwa) aliyepigwa risasi 32 na Kisha kuvuliwa nguo zake na mwili wake kukokotwa na ng'ombe huku kamba ikiwa imefungwa kwenye uume wake zoezi iliyoisha baada ya uume huo kukatika! Kwa maelezo ya Lissu ni kwamba "wasiojulikana" walikuwa tayari kudhalilisha mwili wa Lissu maana risasi 38 za nini? Ndio maana hata DC Sarah Msafiri wa Kigamboni anashangaa!

Ni matumaini Lissu hatimaye apate nafasi ya kuthibitisha maneno yake haya ili tujue uongo na ukweli wake. Hii ni chuki isiyo ya kawaida kiasi cha kujiuliza kwa nini "wasiojulikana" wasiwe na "Plan B?" Ni kwa namna gani Lissu amehakikishiwa usalama wake dhidi ya watu waliokuwa na chuki kiwango hiki? Wanaosema "Lissu Rudi nyumbani" mbona hawasemi kuhusu usalama wake? Hivi tunajua kaburi lake lingeota nyasi na kusahaulika? Kwa tumpoteze mtu muhimu kama huyu katika medani ya sheria?

Kila ninapotafakari "kifo" cha Lissu napata taabu sana kuamini kama kweli kilipangwa na Watanzania wenzetu hawa wanaokwenda kanisani na msikitini au ni mashetani yaliyoletwa mawimbi ya bahari kutoka nchi za mbali? Ni dhahiri ndio sababu Mungu aliacha kuwatuma malaika kumuokoa Lissu na badala yake akaingilia Kati yeye mwenyewe mzima mzima. Hakika Mungu yupo na Yu Hai!

Ndio maana kila hoja inayoletwa dhidi yake hupotea na kuyeyuka kama umande na hatujiulizi kwa nini? Jibu ni moja tu, Lissu yuko mikononi mwa Allah! Ilianza ushoga ikapotea, ikaja anatumiwa na mabeberu ikapotea, ikaja anachafua nchi ikapotea, ikaja anahaini Serikali ikapotea, ikaja anaomba-omba Ulaya ikapotea, sasa eti ni mzembe na mzururaji hivyo akamatwe nayo imeshapita kushoto. Lisu ana nini? Mungu!

Kwa kuwa ni Mungu amekataa Lissu asife ni vizuri tukasubiri kuona nini makusudi ya Mungu kwake hadi amtake kuwa hai? Mbona wengine risasi moja tu mguuni hufa?

Tumpe Mungu nafasi ashughulike na Lissu inaweza akawa ni Joshua wa kutuvusha ng'ambo! Tumuombee afya njema anaporudi kufanyiwa operesheni ya mwisho. Mungu ni mwema!

#AchaWoga2020
@Bngetti2019

Sent using Jamii Forums mobile app
A very touching article! Huyu ni ccm?
 

Similar Discussions

38 Reactions
Reply
Back
Top Bottom