Maneno hapa kazi tu, yaondolewe kwenye ndege za ATCL

Wabongo bana,hapa kazi tu,ilikuwa ni slogan ya JPM kwenye kampeni zake wakati wa kujinadi kuelekea uchaguzi mkuu,ikawaje wakaandija slogan hiyo mpaka kwenye ndege?
 
Serikali ifute maneno ya "hapa kazi tu" kwenye ndege zetu na badala yake ziandikwe jumbe za kutangaza nchi yetu.
Ndege yetu ikitua nje hakuna anaejua maana ya hiyo mineno. Hata kama ni safari za ndani ziwekwe jumbe nzuri na zenye kutangaza taifa letu.
Hayo ni mawazo yangu.

Huna hoja yoyote hapa! Tupe hizo jumbe!
 
'Hapa kazi tu 'ataelewa nani kama ndege ipo china ?
Wenzetu wanaweka slogans zinaeleweka dunia nzima ndege inapokwenda
Quantas the spirit of Australia
Youre the reason we fly
Slogans zinatakiwa zieleweke na kila anayezosoma

Youre the reason we fly ni lugha gani! ‘Youre’ hata sielewi ni neno gani maana hata hilo tangazo kwenye hiyo ndege sijui nani angeelewa!
 
Youre the reason we fly ni lugha gani! ‘Youre’ hata sielewi ni neno gani maana hata hilo tangazo kwenye hiyo ndege sijui nani angeelewa!
Tukianza kufundishana grammar tutaelewana kweli ??
You're the reason we fly, nilitaka kumaanisha hivyo bahati mbaya autospell haikuwa upande nilioutaka
 
Tukianza kufundishana grammar tutaelewana kweli ??
You're the reason we fly, nilitaka kumaanisha hivyo bahati mbaya autospell haikuwa upande nilioutaka

Wewe andika kiswahili tu, sasa hapo umeeleweka kitu gani? Kiingereza cha shule za kata ni shida bwana mdogo!
 
Wewe andika kiswahili tu, sasa hapo umeeleweka kitu gani? Kiingereza cha shule za kata ni shida bwana mdogo!
Unaelewa hata hiyo ni slogan ya nchi gani? Niandike kiswahili wakati wenyewe wameandika hivyo?
Nani shule ya kata kati yangu na wewe?
Slogan ya Liverpool ni 'you'll never walk alone'
Wangeweza kuandika" you will never walk alone " ila kuna swaggs za kunogesha sentence
Nilichoandika kina maana , ya" you are the reason we fly " Quantas airline slogan , wakiwa na maana ya' wewe ndio sababu ya sisi kuruka'
' You are the reason we fly ' ina maana sawa na 'You're the reason we fly'

Uwe na jioni njema
 
Serikali ifute maneno ya "hapa kazi tu" kwenye ndege zetu na badala yake ziandikwe jumbe za kutangaza nchi yetu.
Ndege yetu ikitua nje hakuna anaejua maana ya hiyo mineno. Hata kama ni safari za ndani ziwekwe jumbe nzuri na zenye kutangaza taifa letu.
Hayo ni mawazo yangu.
Kwa kifupi ni kwamba maneno hayo hayana kabisa maana yoyote ile katika ulimwengu wa kujitangaza biashara. Ni kama vile misemo ile iliyopo kwenye khanga ama nyimbo za taarabu, yenye kurusha vijembe kwa watu wengine kwa nia ya kuwananga.

Sasa sijui Wamerakani waandike nini ktk vyombo vyao viendavyo ktk anga za juu, kama sisi tunaona kununua ndege zizizojiendesha kibiashara ni jambo la fahari kiasi cha kufikia kuwananga viongozi wa nchi waliotangulia.
 
Leo hii zimekuwa ndege zenu? Si mlikuwa mnasema tutashitakiwa MIGA na mkawa mnashangilia zikikamatwa?
Kwahiyo hapo umekaa unahisi ni zako peke yako na Sabaya tu?

Hata kama mtoa uzi hakuzihitaji kwa kuwa mlinunua kwa lazima kwa kutumia hela yake nae ni mmiliki mtake msitake
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom