Mandela alipewa sifa aliyostahili Nyerere! So sad!

NI kweli, Nyerere kafanya mambo makubwa sana tena sana ukilinganisha na Mandela!!

Wakati Nyerere alikuwa ni mpigania uhuru wa Afrika Mandela hakupata fursa ya kuonesha kwamba alikuwa ni mpigania uhuru wa Afrika na kwahiyo kilichopo kwenye kumbukumbu ni upiganaji wake dhidi ya nchi yake!

Hata hivyo, kwa wakati ule hakuwa na namna zaidi ya kuipigania nchi yake ambayo bado ilikuwa kwenye minyororo ya makaburu!!

Lakini pamoja na yote hayo suala la kuunda Truth & Reconciliation Commission si jambo la kupuuza hata kidogo na sina shaka hili ndilo lililompa sifa nyingi Mandella!!!

Hata kama Msumbiji walikuwa na kitu kama hicho bado Mandella hakulazimika kufuata nyayo za Msumbiji!!!

Hata kama angehubiri akuanzae mmalize bado Mandela angepata support kubwa sana kutoka kwa wananchi wa Afrika Kusini! Hawa wananchi bado walikuwa na madonda mabichi ya moyoni yaliyotokana na udhalimu wa Makaburu!!!

Ingekuwa ni rahisi sana kwa sababu suppression kubwa ya Makaburu ilikuwa mijini; tena kwa kiasi kikubwa ni kutoka jiji lile lile kubwa kuliko yote!! Hapa Mandela angepata support kubwa sana kama angeamua "akuanzae mmalize!"

Kwanza kuna tofauti kati ya Truth & Reconciliation Commission ya Msumbiji na ile ya South Africa!

Kwa kumbukumbu zangu, Tume ya Mapatano Msumbiji iliundwa baada ya vita vya wenyewe kwa wenyewe kati ya RENAMO & FRELIMO! Kwavile sina uhakika sana am ready to be corrected with evidence lakini naweza kutumia logical argument ku-support madai yangu!!!

FRELIMO hawakuwa na sababu ya kuunda Tume ya Mapatano ya kuwasuluhisha na Wareno kwa sababu Mreno Msumbiji hapakuwa kwake na alitakiwa kuondoka na yule atakayebaki abaki huku akijua Msumbiji halikuwa koloni la Wareno tena!!!

Na kweli, Wareno waliondoka na kurudi Ulaya haidhuru hata kama wapo waliokuwa wamebakia!!!

Sasa kama ni Tume ya Mapatano kati ya RENAMO na FRELIMO pamoja na wafuasi wao; katu huwezi kuilinganisha na ile tume ya Afrika Kusini!

Wakati tume ya Msumbiji ilikuwa ni kuwapatanisha ndugu... Waafrika kwa Waafrika wasahau waliyofanyiana wao kwa wao, ile ya Mandela ndani ya Afrika ya Kusini kimsingi ilikuwa ni kuwafanya Waafrika wasahau unyama wote waliofanyiwa na wageni... Makaburu kutoka Ulaya!

Si jambo dogo hili hata kidogo!!!!

Wakati pasingekuwepo ile tume ya Msumbiji basi Waafrika wangeendelea kuuana wao kwa wao!! Lakini kama isingekuwepo ile ya Afrika Kusini; ambao wangeathirika zaidi ni Makaburu kwa sababu walikuwa outnumbered kwa kiasi kikubwa.

Hata Kibaraka wao Chief Mangosuthu Buthelezi asingeweza kuwasadia kwa sababu wafuasi wa Inkatha Freedom Party
ambao walikuwa tu Durban nao walikuwa outnumbered kwa mbali sana na wafuasi wa ANC!

Lakini pamoja na yote hayo... Mandela akasema let bygone be bygone na kuamua kuunda Tume ya Mapatano ambayo kimsingi ni kwa ajili ya kupatana na wale wale waliomweka korokoroni kwa miaka 27!!!!!

Si jambo dogo hilo hata kidogo!!!!

Pamoja na yote hayo, Mandela anaamua kushirikiana serikalini na wale wale waliomweka ndani kwa miaka 27... si jambo dogo hili!!

Pamoja na yote hayo, Mandela anampa cheo cha Uwaziri wa Mambo ya Ndani (mnaweza kunisahihisha kwa sababu sikutaka ku-verify) Chief Mangosuthu Buthelezi, kiumbe wa Kiafrika ambae wazi wazi alikuwa akiihujumu ANC... si jambo dogo hili!!!

Na ile ilikuwa ni truth commission kweli kweli manake kila kitu kilikuwa wazi!

Bado nakumbuka na Kiingereza changu cha Form I nilivyokuwa namfuatilia Winnie Mandela Live wakati akihojiwa hadi akanifanya nitafute dictionary kufahamu neno "ridiculous" ambalo Winnie alikuwa akilitumia mara kwa mara wakati amekalishwa kitimoto!!!

Si jambo dogo kumwacha mke wako nae awekwe kitimoto tena mbele ya kamera za televisheni!!!

Kwahiyo alichokuwa amefanya Mandella is more than kufanya kile ambacho kilifanywa na Msumbiji bali alifanya jambo ambalo lilihitaji kitu kingine la ziada!!!!

To sum up, ingawaje nakiri Nyerere amefanya mambo makubwa kwa Afrika kuliko Mandela lakini bado Mandela nae ana-deserve heshima anayopata na wala hajapata kwa upendeleo!!

NI bahati mbaya sana dunia haifahamu mchango wa Mwalimu ingawaje kwa dunia siwezi kushangaa kwa sababu Mwalimu alikuwa anawasaidia waafrika wenzake na nje ya Afrika it's none of their business!!! Uchungu wangu ni pale ambapo hata Afrika yenyewe inapoonekana kutofahamu mchango huu wa Mwalimu!!!

Lakini ngoja niweke kumbukumbu sawa kwa manufaa ya vizazi vyetu manake wengi huwa hatulizungumzii vizuri hili jambo!!

Pamoja na kwamba tangu mwanzo Mwalimu alionesha kusaidia harakati za ukombozi, lakini mengine mengi yaliyofuata alikuwa anatekeleza kazi aliyokuwa amepewa na OAU.

Baada ya OAU kuundwa, pia ziliundwa kamati mbalimbali kwa ajili ya kufanikisha na kutatua changamoto mbalimbali barani Afrika! Kwa mfano, kulikuwa na Kamati ya Viwanda (and something) ambayo Makao Makuu yake yalikuwa Gaborone, Botswana!!!

Tanzania tukatwishwa zigo la ukombozi ambapo Kamati ya Ukombozi ilikuwa na makao yake makuu Dar es salaam!!!

Main goal ya Kamati ya Ukombozi ilikuwa ni moja: kuhakikisha nchi zote zilizokuwa chini ya ukoloni nazo zinapata uhuru! By the time, nchi hizo zilikuwa Msumbiji, Angola na Guinea Bissau!!

Na kweli, Mwalimu Nyerere aliifanya kazi hiyo kwa moyo mmoja na mara kadhaa kutumia raslimali za taifa ili mradi tu kuhakikisha lengo hilo linafikiwa na kweli likafikiwa!!

Nadhani Kamati ya Ukombozi ndie kamati pekee ya OAU iliyokuwa imefanikiwa malengo yake miongoni mwa kamati zingine zote!!!

Remember, Afrika Kusini haikuwa considered kama ilikuwa inatawaliwa! Ni kama Zanzibar... Zanzibar haiwi considered kwamba ilitawaliwa na Sultan at least baada ya ujio wa wakoloni wa Ulaya!!!
Chile, nimependa maelezo yako. Ningeweza kuchangia mengine hapo ila muda wangu hautoshi kwa sasa. Ila nitaeleza kidogo mawazo yangu kuhusu OAU kugawa kamati zake na TZ kupata ile ya Ukombozi. Ukweli ni kwamba si nchi zote wanachama wa OAU walitaka hii kamati iundwe. Kamati hii iliundwa kutokana na ushauri na msukumo wa Mwalimu. Bila Mwalimu hiyo Kamati, hata kama ingeundwa, isingefika popote. Mwalimu aliamini kwa dhati kabisa ya moyo wake kwamba Afrika ilikuwa na jukumu la kuikomboa sehemu ya Afrika iliyokuwa bado inatawaliwa. Nchi nyingine nyingi ziliamini kwamba hilo ni jukumu pekee la wananchi wa nchi hizo! Hata Kenya na Malawi, kwa mfano tu, viongozi wao waliamini hivyo. Hata kama OAU ingekataa kuanzisha Kamati ya Ukombozi, Mwalimu na viongozi wengine kama Obote, Kaunda, Sekou Toure, Haile Selasie, yule aliyekuwa Rais wa Misri, etc wangeanzisha kamati kama hiyo kwa nia hiyo hiyo. Tanzania kuwa Mwenyekiti wa Kamati hiyo kulitokana na juhudi za Mwalimu za kuianzisha kamati hiyo na siyo kwa sababu tu kwamba ilipendekezwa na OAU.
 
Sisi waafrika wenyewe kwa wenyewe hatupendani ndio maana viongozi wengi hawataki kumuenzi mwalimu.kiki nyingi kwa Mandela zimetoka nchi za ulaya baada ya kuwasmehe wazungu wezao.Jambo ambalo linaniuma sana.SA watu wengi hawamjui hata Nyerere .Ni baadhi sana.,haswa wale Mkhonto we sizwe.Historia yao mashuleni haiongelei Afrika kwa ujumla.Bali historia yao inaongelea nchi yao pekee.watu wengi SA hawajui nini mchango uliofanywa na viongozi wengi wa Afrika hasa Nyerere kipindj cha ubaguzi wa rangi.Yote hii imesababishwa na ubinafsi wa waafika.
 
WASWAHILI WANASEMA KHASIDI HANA SABABU.
WAZUNGU NI MAKHASIDI WA AFRIKA.
HAWAWEZI KUMKUMBUKA NYERERE KWA SABABU ALIFANYA VITU VYA KIPEKEE DUNIANI NA HASA AFRICA.
HAKUPENDA FALSAFA YA UTAWALA WA KIZUNGU KWANI ULIKUWA WA KINYONYAJI.
TUKUMBUKE INCHI YETU ILIPOVAMIWA NA IDD AMIN HAKUNA INCHI ILIIKEA UGANDA ILA TANZANIA ILIPOANZA KUICHAPA UGANDA WAZUNGU WALIPIGA KELELE.
HISTORIA ITAWEKA MAMBO SAWA NA NYERERE BAADAYE ATAKUMBUKWA KULIKO MANDELA.
MANDELA ANAKUMBUKWA NA DUNIA NZIMA KWA SABABU MBILI KUU.
1. ALIKAA JELA MIAKA 27
2. HAKULIPIZA KISASI KWA WAZUNGU AU MAKABURI NA PIA HAKUBADILI SANA MFUMO WA UTAWALA NA PIA UCHUMI WA INCHI.
 
Na
No Vita vya Renamo Vilianzwa 1983 Na vilimalizika na Makubaliano ya Nkomati ya 1985. Kabla ya Kufa kwa Samora. Truth and Reconciliation ilianza tangu 1976 na hapo 1981 ilikuwa ni siku ya Kukamilisha tume. Pili ungesikiliza hiyo video iko Wazi there is nothing to do with Renamo.
Rejea upya historia ya Msumbiji!!! Vita vya wenyewe kwa wenyewe kati ya RENAMO na FRELIMO vilianza mara baada ya Msumbiji kupata uhuru. The same happened to Angola kati ya MPLA na UNITA.

Vita kati ya RENAMO na FRELIMO viliisha in early 1990's (ama 1991 au 1992) mara baada ya Utawala wa Makaburu kuonesha nia ya kumaliza siasa zao za kibaguzi Afrika Kusini! Similar situation happened to Angola na Namibia ambako bado SWAPO walikuwa msituni!!!

Hapo ndipo watu walipo-conclude kwamba civil wars ndani ya Msumbiji na Angola ilikuwa inachochewa na utawala wa makaburu!!!!

Tume ya Mapatano Msumbiji iliundwa around 1992.

Lakini hata nikitumia dhana yako kwamba hiyo tume iliundwa 1976, still haiwezi kuwa ni tume iliyotaka kuleta suluhu kati ya Waafrika wa Msumbiji na Wareno kwa sababu by 1976 tayari Msumbiji walikuwa wameshapata uhuru wake na Wareno walishakusanya virago vyao!!!
 
Chile, nimependa maelezo yako. Ningeweza kuchangia mengine hapo ila muda wangu hautoshi kwa sasa. Ila nitaeleza kidogo mawazo yangu kuhusu OAU kugawa kamati zake na TZ kupata ile ya Ukombozi. Ukweli ni kwamba si nchi zote wanachama wa OAU walitaka hii kamati iundwe. Kamati hii iliundwa kutokana na ushauri na msukumo wa Mwalimu. Bila Mwalimu hiyo Kamati, hata kama ingeundwa, isingefika popote. Mwalimu aliamini kwa dhati kabisa ya moyo wake kwamba Afrika ilikuwa na jukumu la kuikomboa sehemu ya Afrika iliyokuwa bado inatawaliwa. Nchi nyingine nyingi ziliamini kwamba hilo ni jukumu pekee la wananchi wa nchi hizo! Hata Kenya na Malawi, kwa mfano tu, viongozi wao waliamini hivyo. Hata kama OAU ingekataa kuanzisha Kamati ya Ukombozi, Mwalimu na viongozi wengine kama Obote, Kaunda, Sekou Toure, Haile Selasie, yule aliyekuwa Rais wa Misri, etc wangeanzisha kamati kama hiyo kwa nia hiyo hiyo. Tanzania kuwa Mwenyekiti wa Kamati hiyo kulitokana na juhudi za Mwalimu za kuianzisha kamati hiyo na siyo kwa sababu tu kwamba ilipendekezwa na OAU.
Nakubaliana na maelezo yako kwa 100%.

Kwa yeyote ambae angeshauri uanzishwaji wake bado am very sure majukumu ya kuongoza kamati ile yangekuja Tanganyika kwa sababu hizo hizo ulizosema... tayari Mwalimu alishaonesha kwa kauli na vitendo lengo la kutaka kuhakikisha Afrika yote inakuwa huru!!!
 
Mandela jela miaka 27 alipoachiwa akawasamahe wazungu.

Je Nyerere angefungwa hiyo miaka 27 halafu angeachiwa je angewasamahe wazungu?


*Long Walk For Freedom*
 
Hivi huko south Africa kuna nyerere road,kama IPO basi inatosha.Malipo mengine Mungu aliziona jitihada za sir Nyerere atamlipa mwenyewe na malipo mengine tumelipwa watz taifa lenye kila aina ya utajiri
 
Mwalimu Nyerere Muda Mfupi Baada ya Uhuru alipata Ugeni wa Siri, Ugeni wa Nelson Mandela. Mandela alikuwa akitaka Msaada kwa Nyerere wa Kuanzisha Jeshi la Kupigania Haki la Umkoto We Skzwe yaani Mkuki wa Bwana au Mkuki wa Mfalme.

Kulingana Na Kitabu cha Mandela cha Long Walk to Freedom, Nyerere alionyesha Kusita, alimshauri asubiri asifanye jitihada za Kijeshi mpaka Walter Sisulu aachiliwe. Wakaagana Nelson akamwambia Mwalimu atarudi Tena na Akaenda Ethiopia ambako alikutana na Haile Selassie, Haile Selassie alimwelewa Mandela Kwa haraka na Akampa Pesa nyingi sana tu. Mandela akasafiri kurudi SA. Kufika huko muda Mchache akakamatwa hivyo hakuweza Tena kuonana na Nyerere.

Baada ya Mandela Kukamatwa na Nyerere Kuona kwa Undani Uonevu wa Ukoloni Nchi za Kusini Mwa Afrika na Ubaguzi wa Rangi SA, basi akaamua Kujitwisha Mzigo wa Kusaidia Majeshi ya nchi zote zile na Pia sio tu hivyo Bali kiwazi wazi akazunguka Dunia Nzima Kupiga Kelele na Pia Kutafuta fedha za kusaidia Majeshi yale. Na mara nyingi akatumia hata Majeshi ya Tanzania kusaidi. Hii ilimhatarisha binafsi na nchi kwa ujumla!




Msumbiji ilipopata Uhuru Nyerere ndiye aliyewakalisha Akina Samora na Kuwaambia wasilipize Visasi kwa Wazungu au Collaborators (Waliokuwa wakiwasaidia wazungu) na kwa Mwongozo wa Moja kwa moja wa Nyerere Ikaanzishwa Tume ya Ukweli na Usuluhishi (Truth and Reconciliation) ambapo waliofanya uhalifu wa kinyama walikuwa wakikiri na Kuomba Msamaha.



South Afrika ilipokuwa Democratic 1994 Mandela Akafuata Mfano huo nukta kwa Nukta. Lakini Dunia Nzima ikamwenzi sana Mandela, Mandela alizikwa na Viongozi wote Wa dunia, Ila Nyerere hakupewa heshima wala shukurani anayoistahili na Dunia wakati wa Kifo chake.

Kila uendapo Duniani Unakuta Sanamu za Mandela, Ila Nyerere hata AU ilibidi Mugabe aseme ikiwa Afrika haitaki Kumkumbuka Nyerere Zimbabwe itafanya Kivyake!

Nyerere ni juu kuliko Mandela kwa sababu kuu zifuatazo;
1. Nyerere amehudumu kama Rais kwa miaka 23 ukilinganisha Nandela miaka 4.
2.Nyerere ameshiriki ktk Ukombozi wa nchi zote za Afrika kwa 100% na hata kuihatarishia nchi yake naslahi yake. Kuliko Mandela ambaye amehangaika na kufungwa kwa ajili ya watu wake tu na siyo wwtu wote wa Afrika.
 
Niliwahi kusoma short course chuo alichosomea Mandela cha Grahamtown. Wazungu wapale walikuwa wanamsifia Mandela kwa jambo moja kubwa tena kiunafiki nafiki hasa pale wanapokuwa na waafrika weusi, kwamba ni shujaa wa kuleta umoja kwa mantiki ya kwamba amewaridhia wazungu na kuwafanya na kuwaona ni wa afrika kusini wote. Ila bado hao hao wazungu tena wanafunzi ,pamoja na wahindi walikuwa wanaundani na kejeli ya ndani kwa ndani na watu weusi. Hivyo basi japo kweli Mandela amefanya mengi ila ngoma yake ilipigiwa chapuo zaidi na mataifa ya kizungu ili waendelee kukwapua mali kule S.A. Bwana Nyerere yeye ni kweli hakuvuma kwa sababu aliwakandia wazungu katika hutuba zake. Lakini pia alipenda wazungu popote pale walipo Afrika wasiteswe tofauti kabisa na aliamrisha kuuliwa kwa mtu yeyote mwenye damu ya kiarabu hapa Zanzibar ule mwaka 1964 katika uvamizi wa Zanzibar.
 
Kuna vitu viwili muhimu sana ambavyo mnatakiwa kuvielewa;

1. Kujiita Mjamaa ni kosa kubwa kwa nchi za Wazungu maybe ujiite Mjaa kinadharia tu kama tunavyojiita kwa sasa lakini kimatendo wewe uko kwao na misaada unakimbilia kuwa omba wao na masharti yao uyakubali.

2. Nelson Mandela kwa nini anapendwa na Wazungu, baada ya kutoka gerezani, hakuwa na misimamo mikali kama alivyokuwa anaingia gerezani. Ukisoma Hotuba yake akijijitetea alisema kuwa Amejiandaa Kufa akiwa anawatetea watu wa Afrika ya Kusini alisema; I am prepared to Die. Baada ya kutoka, alikuwa kwanza ameishiwa nguvu sana, nadhani humo gerezani alipata muda mwingi sana wa kutafakari maisha yake binafsi na pia akimwomba Mwenyezi Mungu....hasa akisisitiza maneno ya Yesu kwamba; Bwana Wasamehe Maana Hawajui Walitendalo. Baada ya kutoka alianza kuongea lugha ya Kiliberali na aliwahahakikishia kutolipiza......hili ndo Wazungu wanamuona ni hero zaidi.
 
Yule Mzee Mungu alimpa uwezo mkubwa sana wa kutoa hotuba zenye mambo mengi ya msingi sana kwa wakati aliokuwa hai kuhusu nchi yetu na dunia pia na hotuba zake nyingi ziko valid mpaka leo hii.
Kuna hotuba za Viongozi wa Leo hata Miaka ya 67 haziwezi kuwa applicable ni Utombo!
 
Rejea upya historia ya Msumbiji!!! Vita vya wenyewe kwa wenyewe kati ya RENAMO na FRELIMO vilianza mara baada ya Msumbiji kupata uhuru. The same happened to Angola kati ya MPLA na UNITA.

Vita kati ya RENAMO na FRELIMO viliisha in early 1990's (ama 1991 au 1992) mara baada ya Utawala wa Makaburu kuonesha nia ya kumaliza siasa zao za kibaguzi Afrika Kusini! Similar situation happened to Angola na Namibia ambako bado SWAPO walikuwa msituni!!!

Hapo ndipo watu walipo-conclude kwamba civil wars ndani ya Msumbiji na Angola ilikuwa inachochewa na utawala wa makaburu!!!!

Tume ya Mapatano Msumbiji iliundwa around 1992.

Lakini hata nikitumia dhana yako kwamba hiyo tume iliundwa 1976, still haiwezi kuwa ni tume iliyotaka kuleta suluhu kati ya Waafrika wa Msumbiji na Wareno kwa sababu by 1976 tayari Msumbiji walikuwa wameshapata uhuru wake na Wareno walishakusanya virago vyao!!!
Unabishana Na Video? Angalia Video ya Mkutano wa TRC Mozambique uliokuwa na Kilele chake 1981-2.

Hayo ya Renamo ni Maswala amengine! Makaburu wa South Africa pamoja na Old colonial Powers zilitaka kuwa na control juu ya nchi ambazo mara zilipata Uhuru, Mfano Angola walimtumia Savimbi aliyekuwa na Uwezo mkubwa wa Kusema! Mozambique wakamtumia Alfonzo Dlakama, Zimbabwe Joshua Nkomo, Congo wakamtumia Kasavubu, Tshombe na Baadaye Mobutu, shamefully hata Uganda ndio waliomsaidia Idi Amini ila walishindwa Kumcontol!
 
Tatizo sio sifa inshu hapo ilikua kufanya kitu kifanikiwe hata bila misifa.,, Huo ndo uzalendo
 
Unabishana Na Video? Angalia Video ya Mkutano wa TRC Mozambique uliokuwa na Kilele chake 1981-2.
Hayo ya Renamo ni Maswala amengine! Makaburu wa South Africa pamoja na Old colonial Powers zilitaka kuwa na control juu ya nchi ambazo mara zilipata Uhuru, Mfano Angola walimtumia Savimbi aliyekuwa na Uwezo mkubwa wa Kusema! Mozambique wakamtumia Alfonzo Dlakama, Zimbabwe Joshua Nkomo, Congo wakamtumia Kasavubu, Tshombe na Baadaye Mobutu, shamefully hata Uganda ndio waliomsaidia Idi Amini ila walishindwa Kumcontol!
Sasa mimi na wewe ni nani anaebishana na hiyo video?! Kumbuka hiki ndicho umesema:
Msumbiji ilipopata Uhuru Nyerere ndiye aliyewakalisha Akina Samora na Kuwaambia wasilipize Visasi kwa Wazungu au Collaborators (Waliokuwa wakiwasaidia wazungu) na kwa Mwongozo wa Moja kwa moja wa Nyerere Ikaanzishwa Tume ya Ukweli na Usuluhishi (Truth and Reconciliation).

South Afrika ilipokuwa Democratic 1994 Mandela Akafuata Mfano huo nukta kwa Nukta.
Ndipo nami nikasema:

Kwanza kuna tofauti kati ya Truth & Reconciliation Commission ya Msumbiji na ile ya South Africa!

Kwa kumbukumbu zangu, Tume ya Mapatano Msumbiji iliundwa baada ya vita vya wenyewe kwa wenyewe kati ya RENAMO & FRELIMO! Kwavile sina uhakika sana am ready to be corrected with evidence lakini naweza kutumia logical argument ku-support madai yangu!!!

FRELIMO hawakuwa na sababu ya kuunda Tume ya Mapatano ya kuwasuluhisha na Wareno kwa sababu Mreno Msumbiji hapakuwa kwake na alitakiwa kuondoka na yule atakayebaki abaki huku akijua Msumbiji halikuwa koloni la Wareno tena!!!

Na kweli, Wareno waliondoka na kurudi Ulaya haidhuru hata kama wapo waliokuwa wamebakia!!!

Sasa kama ni Tume ya Mapatano kati ya RENAMO na FRELIMO pamoja na wafuasi wao; katu huwezi kuilinganisha na ile tume ya Afrika Kusini!

Wakati tume ya Msumbiji ilikuwa ni kuwapatanisha ndugu... Waafrika kwa Waafrika wasahau waliyofanyiana wao kwa wao, ile ya Mandela ndani ya Afrika ya Kusini kimsingi ilikuwa ni kuwafanya Waafrika wasahau unyama wote waliofanyiwa na wageni... Makaburu kutoka Ulaya!
Hiyo video uliyoweka, kuanzia Dakika 1:41, Narrator anatuhabarisha:
FRELIMO proves to have have enough popular support. And after a period of transition, they come into power. In 1975 Mozambique becomes independent. The Portugueses pool out on mass (1). What remains is the problem of those Mozambicans who were in league with the Portuguees. FRELIMO believes everyone has the possibility to change. And therefore is willing to forgive those who betrayed the country (2). But first, they had to denounce themselves, so that the people would know who they were. Face up the past, suffer the shame. This rehabilitation meeting does a way with the old contradiction between collaboration and resistance. 1982, the socialist government of Mozambique, a young independent country in southern Africa organized a meeting of great political importance. President Samora Machel and his government leaders held a week long session with some thousand collaborators who'd worked by order of Portugal at the time of its colonial domination of Mozambique (3). People who betrayed their compatriots, sometimes even tortured or killed them (4).
Kauli hiyo hapo juu ipo sawa na maelezo yangu.

Note #(1) in RED inathibitisha kwamba baada uhuru 1975, Wareno wakaondoka.

Note # (2) in RED, inazungumzia forgiveness in favor of those who betrayed the country. Mkoloni wa Kireno hawezi kuwa kwenye kundi la watu waliosaliti Msumbiji kwa sababu, wao Msumbiji sio kwao! Mtu anayepewa sifa ya usaliti ni mshirika wako, na kwa context ya mjadala huu, ni raia wa nchi husika alieamua kushirikiana na adui wa nchi.

Note # (3) in RED inaonesha Samora Machel anafanya mkutano na wale waliokuwa wanashirikiana na Wareno wakati Msumbiji ikiwa koloni la Kireno. Hapo juu, tumeshaona Wareno walishaondoka, which means, huo ulikuwa ni mkutano wa wa ujenzi wa Msumbiji mpya kati ya patriots na traitors.

Note # 4 in BLUE ina-conclude ni nani hasa hao wahusika... Narrator anasema "...people who betrayed their compatriots." Mreno hawezi kuwa COMPATRIOTS.

So, to sum up, maelezo hayo yanaonesha kile kile nilichosema mimi kwamba Truth & Reconciliation Commission of South Africa is completely different na hiyo Rehabilitation Meeting.

Wakati ile ya South Africa ilikuwa ni kutengeneza mapatano kati Oppressors & Traitors in one hand and patriots in another hand... which meant to forgive even Makaburu, ile ya Mozambique ilikuwa ni ya kutengeneza suluhu na mapatano among brothers... all black brothers!!!

Narudia, rejea upya historia yako kuhusu Msumbiji kwa sababu, ulifikia hata kusema kwamba:

No Vita vya Renamo Vilianzwa 1983 Na vilimalizika na Makubaliano ya Nkomati ya 1985. Kabla ya Kufa kwa Samora. Truth and Reconciliation ilianza tangu 1976 na hapo 1981 ilikuwa ni siku ya Kukamilisha tume. Pili ungesikiliza hiyo video iko Wazi there is nothing to do with Renamo.
BBC wanatoa timeline ya Mozambique History:
RENAMO.png

Hicho unachoita Vita na RENAMO vilimalizika na Makubaliano ya Nkomati, source ya hapo juu inasema:
1984 - Under Nkomati Accord, Mozambique drops support for African National Congress (ANC) in return for South African withdrawal of backing for Renamo. Short-lived ceasefire fails and Renamo continues its offensives.
WHY Inkomat? Kama hiyo quote inavyo-highlight inavyosema, ilikuwa ni makubaliano kati ya FRELIMO kuacha kui-support ANC ili hatimae Afrika Kusini ya Makaburu iache kui-support RENAMO.

Baada ya uhuru wa Msumbiji, Walowezi wa Zimbabwe wanaanza kui-support RENAMO na ndipo vilipoanza Vita vya Wenyewe 1976 or 1977 kati ya RENAMO & FRELIMO na sio 1983 kama ulivyosema.

Baada ya utawala wa Walowezi kuondolewa Zimbabwe in 1981, ilimaanisha RENAMO hawatakuwa na backup.Hapo ndipo Makaburu walipojitosa na kuanza kuwa-support RENAMO na hatimae ndipo ikazaliwa Nkomati!.

Foreign Policy nao wanaandika:
The horrific discoveries add to a growing body of evidence that, almost a quarter century after the end of a 16-year civil war that killed a million people, Mozambique is once again mired in conflict.......

Mozambique’s civil war was noted for its brutality, meted out in particular by Renamo, a rebel group that was founded, financed, and armed by foreigners bent on destabilizing the country: first by white Rhodesia, then apartheid South Africa. A peace agreement ended the war in 1992 and led to multi-party elections in which Renamo came second, as it has done in every election since.
Uki-connect hizo highlights in RED unapata vita vya wenyewe kwa vilidume kwa miaka 16 na vilimaliza in 1992! Ukifanya subtraction hapo utaona kumbe vita vilianza 1976 kama ilivyoripotiwa na BBC hapo juu au kama ambavyo nilisema:
Rejea upya historia ya Msumbiji!!! Vita vya wenyewe kwa wenyewe kati ya RENAMO na FRELIMO vilianza mara baada ya Msumbiji kupata uhuru. The same happened to Angola kati ya MPLA na UNITA.

Vita kati ya RENAMO na FRELIMO viliisha in early 1990's (ama 1991 au 1992) mara baada ya Utawala wa Makaburu kuonesha nia ya kumaliza siasa zao za kibaguzi Afrika Kusini! Similar situation happened to Angola na Namibia ambako bado SWAPO walikuwa msituni!!!
 
Niliwahi kusoma short course chuo alichosomea Mandela cha Grahamtown. Wazungu wapale walikuwa wanamsifia Mandela kwa jambo moja kubwa tena kiunafiki nafiki hasa pale wanapokuwa na waafrika weusi, kwamba ni shujaa wa kuleta umoja kwa mantiki ya kwamba amewaridhia wazungu na kuwafanya na kuwaona ni wa afrika kusini wote. Ila bado hao hao wazungu tena wanafunzi ,pamoja na wahindi walikuwa wanaundani na kejeli ya ndani kwa ndani na watu weusi. Hivyo basi japo kweli Mandela amefanya mengi ila ngoma yake ilipigiwa chapuo zaidi na mataifa ya kizungu ili waendelee kukwapua mali kule S.A. Bwana Nyerere yeye ni kweli hakuvuma kwa sababu aliwakandia wazungu katika hutuba zake. Lakini pia alipenda wazungu popote pale walipo Afrika wasiteswe tofauti kabisa na aliamrisha kuuliwa kwa mtu yeyote mwenye damu ya kiarabu hapa Zanzibar ule mwaka 1964 katika uvamizi wa Zanzibar.
Khamisiya bila shaka wewe ni Muarabu au una damu ya Sultan Muarabu! Kama ni hivyo, tatizo lako linajulikana
 
Niliwahi kusoma short course chuo alichosomea Mandela cha Grahamtown. Wazungu wapale walikuwa wanamsifia Mandela kwa jambo moja kubwa tena kiunafiki nafiki hasa pale wanapokuwa na waafrika weusi, kwamba ni shujaa wa kuleta umoja kwa mantiki ya kwamba amewaridhia wazungu na kuwafanya na kuwaona ni wa afrika kusini wote. Ila bado hao hao wazungu tena wanafunzi ,pamoja na wahindi walikuwa wanaundani na kejeli ya ndani kwa ndani na watu weusi. Hivyo basi japo kweli Mandela amefanya mengi ila ngoma yake ilipigiwa chapuo zaidi na mataifa ya kizungu ili waendelee kukwapua mali kule S.A. Bwana Nyerere yeye ni kweli hakuvuma kwa sababu aliwakandia wazungu katika hutuba zake. Lakini pia alipenda wazungu popote pale walipo Afrika wasiteswe tofauti kabisa na aliamrisha kuuliwa kwa mtu yeyote mwenye damu ya kiarabu hapa Zanzibar ule mwaka 1964 katika uvamizi wa Zanzibar.
Uvamizi wa Zanzibar? Ulifanywa na nani sasa na nani aliyeuongoza huo uvamizi Karume au Nyerere? Hii itikadi ndo iliyowajaa mioyoni mwenu na ndiyo itakayo wasambaratisha wazanzibar.... So wamoja ninyi. Kuna upemba na uunguja, uafrika na uarabu.

Hata kama ingekuwa ni kweli amewaua, kuna kosa gani kuliondoa tawi lisilozaa mtini ili yenye kutoa matunda mazuri yamee?
 
Back
Top Bottom