Akii nahisi hii timu imelogwa ... hakuna kocha anae itaka hii timu !!
Mimi nakomalia kwenye DNA tusiipotezee DNA ya timu yetu .. na mwelekeo sahihi uko kwa Brendan Rodgers.. naamini sana mfumo wake wa kupress ... cha muhimu si mpira wa kupress? mbinu anazo ..
Akishindwa tutajaribu msimu unao fata !! Tuwe tunajaribu jaribu makocha mpaka rooney atapo komaa kuifunza timu yetu

DNA ni jambo la muhimu sana kwa timu yetu .. na hawa malejendarii ushauri wao ni wa kuzingatiwa sana maana wanaijua timu yetu nje ndani
 
Akii nahisi hii timu imelogwa ... hakuna kocha anae itaka hii timu !!
Mimi nakomalia kwenye DNA tusiipotezee DNA ya timu yetu .. na mwelekeo sahihi uko kwa Brendan Rodgers.. naamini sana mfumo wake wa kupress ... cha muhimu si mpira wa kupress? mbinu anazo ..
Akishindwa tutajaribu msimu unao fata !! Tuwe tunajaribu jaribu makocha mpaka rooney atapo komaa kuifunza timu yetu

DNA ni jambo la muhimu sana kwa timu yetu .. na hawa malejendarii ushauri wao ni wa kuzingatiwa sana maana wanaijua timu yetu nje ndani
DNA lazima ifatwe

Rooney au wamrudishe tu mwenyewe Ole sosha

 
Mchezaji wa zamani wa United Patrice Evra amemshukuru Ole Gunnar Solskjaer kwa kazi yake na amewapa kitisho wachezaji wa Manchester United akisema "ninakuja nyuma yenu"

Evra ameandika katika mtandao wa instagram "
" Asante rafiki yangu kwa kutufanya tuiamini tena Manchester United. Kwa bahati mbaya usipopata matokeo watu husahau mazuri uliyoyafanya. Kwa wachezaji wote wa Manchester United ninakuja, tuonane katika mechi na Arsenal ". Evra alikuwa mchezaji mwenzake na Solskjaer wakati wa msimu wa mwisho wa Ole akichezea Manchester United. Wote kwa pamoja walikuwa chini ya Sir Alex Ferguson.

#KitengeSports
 
Manchester United Legends with Coaching Licences.
1. Steve Bruce
2. Mark Hughes
3. Paul Ince
4. Garry Neville
5. Michael Carrick
6. Jap Stam
7. Roy Keane
8. Phil Neville
9. Patrice Evra
10. Nick But
11. Ole Gunar Solkjaer
12. Wayne Rooney
13. Diego Forlan
14. Mike Phelan
Katika orodha hiyo amekosekana hata legend mmoja wa kuvaa viatu vya Ole ?
Umpe timu evra kweli timu yetu imekuwa Kama Namungo
 
Hapo hamna kocha anaeweza kufundisha man u hata sosha ilikuwa nafasi ya upendeleo hakustahili maana hakuwahi kuprove chochote kwenye soka la ushindani kimbinu na kimafanikio maana amefundisha Cardiff akaishusha daraja...na iyo molde kwahy hawa sijui malegend wanatuharibia timu wanaongea sana wanatetea upande wao mfano mzuri ni kushindwa kumtimua sosha ni kama ilikuwa ngumu sana mbaka tumemuacha conte ameenda spurs
Pamoja na yote ila kajitahidi sana kutengeneza kikosi hata ile kuingia top four consecutive two season ilikuwa imeanza kusahaulika.

Atleast kocha mpya sasa atakuwa na sehemu ya kuanzia.
 
Tujikumbushe japo kidogo mazuri na mabaya yake:

Safari ya Ole Gunnar Solskjaer ndani ya manchester united
Yawezekana utawala wa Ole Gunnar Solskjaer akiwa kama ni kocha wa muda pale mitaa ya carrington (interim manager)umeshasahaulika baada ya miaka mitatu kupita tokea ateuliwe kuwa kocha mkuu wa manchester united, lakini sidhani kama kuna mshabiki wa manchester united atasahau tukio la comeback lililofanywa na man utd dhidi ya PSG kwenye hatua ya mtoano ya michuano ya champions league huku Ole akiwa bado ni kocha wa muda (man utd walipata ushindi wa magoli 3 dhidi ya 1). Hapo ndipo ulipozaliwa ule wimbo wa "Ole at the wheel"

Baada ya takribani miaka mitatu kupita hatimaye utawala wake umemalizika kwa kufukuzwa kazi baada ya kuendelea kupata matokeo yasioridhisha huku yale yote alioyazungumza kupitia mahojiano yake ya mwanzo juu ya style ya kiuchezaji akishindwa kuyasimamia ipasavyo kwa mtazamo wangu Mimi.

furaha na dhoruba kwa wakati mmoja
Baada ya kumalizika kwa mechi dhidi ya PSG, Ole gunnar alihudumu mechi mbili tu akiwa na nyadhifa ya ukocha wa muda (caretaker) wa manchester united na mechi hizo ziliishia kwa man utd kuambulia vipigo ikiwemo mechi ya Barcelona na baada ya hapo bodi ikaendekea kumuamini na hatimaye akateuliwa kuwa kocha mkuu wa manchester united.

kiuhalisia ulimwengu wa bwana Ole kwa upande wa mfumo rasmi wa kiuchezaji, fikra, na mipango aliyokuja nayo tokea mechi ya kwanza (tactical perspective) uliishia usiku ule tuliofungwa magoli 2 dhidi ya PSG ndani ya Old trafford na baada ya hapo kila kitu kikabadilika (wengine wakasema honeymoon imeisha) kwa sababu tofauti ikiwemo majeruhi ya wachezaji muhimu.

Ole alirithi timu iliokosa umoja ndani na nje ya uwanja, licha ya kuwepo kwa mazingira mabaya ndani ya kikosi Ole pia alirithi timu iliokwisha poteza pattern ya kiuchezaji na identity. Ole pia alirithi timu iliokwisha onyesha madhaifu makubwa sana kwenye safu ya ulinzi baada ya kuruhusu magoli 29 kwenye mechi 17.

Jose anafukuzwa, Ole anaanza kazi rasmi:
mechi ya kwanza chini ya utawala wa Ole tulianza na mfumo wa 4-3-3 na high pressing system , mechi ya kwanza tulianza na midfield ya matic, herrera na pogba huku safu ya ushambuliaji tulianza na martial, rashford na lingard.

Kwa aliyesikiliza mahojiano ya ole atakuwa anayakumbuka maneno matamu aliyoyaongea, alisema anataka kuona wachezaji wake wanakimbia sana, pressing ya hali ya juu (chini ya ole, pressing intensity ilikuwa ni 8 ukilinganisha na 10 ya jose mourinho, kwa ufupi tuliimarika zaidi na zaidi chini ya ole ukilinganisha na jose chini ya miaka yake miwili), pasi za haraka za kwenda mbele ndio maana si ajabu alianza na watu watatu hao safu ya mbele na hapo katikati akifaidika na uwepo wa pumzi ya ander herrera aliye kwenye ubora, pogba akitokea upande wa kushoto kama alivyokuwa juventus.

Jesse lingard alikuwa ndiye mzungukaji mkuu wa ndani ya uwanja akiongeza work rate hapo juu na chini, kwa ufupi jesse alisimama kama ni kiunganishi kikuu cha safu ya kiungo na ushambuliaji. Uwepo wa jesse, herrera na matic kiulinzi kulimzawadia uhuru wa kiuchezaji paul pogba kwa mara ya kwanza.

Uhuru huo aliutumia vizuri sana paul pogba kwani alifunga magoli matano (non penalty) ndani mechi 9 za mwanzo za ole gunnar, pia aliweza kuongeza assist nne ndani ya hizo mechi 9, kiwango cha kupiga mashuti kiliongezeka kutoka 2.93 chini ya mourinho hadi 4.08

marcus rashford naye kiwango chake cha kupiga mashuti kiliongezeka kutoka 2.0 chini ya mourinho kwa dakika 90 hadi 4.8 huku pia akifunga magoli 6 ndani ya hizo mechi 9 za mwanzo za Ole gunnar. pia ndani ya mechi 10 tulishuhudia mabadiliko makubwa sana ya kiuchezaji, kitakwimu na kimatokeo,
  • kwa mfano non-penalty xG ( expected goal) per game tulipanda sana kutoka 1.41 chini ya jose hadi 1.90 chini ya Ole.
  • non-penalty xG against tulishuka kutoka 1.43 chini ya jose kwenda 1.07(safu yetu ya ulinzi iliimarika, hatukuwa tunakaribisha mashambulizi ya mara kwa mara)
================
Inaendelea
Makombe mengi - Jose

Points nyingi - Jose

Least goals conceded - Jose

Highest xG - Jose

Higher winning rate - Jose

Kutopoteza ugenini mechi nyingi - Jose

Kwanini media zinamlabel Jose kama destroyer wa United hiyo ni siri yao
 
Makocha wengi waliohusishwa na united wameitolea nje isipokua Pochettino.

Tuchel alisema ni ngumu sana kumanage PSG kwa sababu siyo tu unatakiwa kuwa mlezi wa mastar wa pale bali unatakiwa kuwalea na ndugu na marafiki zao.

Nafikiri hilo linamkumba Pochettino pia. So haondoki kwakua mkewe yupo London anaondoka kwakua kuisimamia timu yenye mastar wengi vile ni mzigo. Kingine ni namna PSG inapata ushindi wake huku inashindwa kupata clean sheet.
 
Back
Top Bottom