Manara aipa sifa tele Simba na kuidhihaki Yanga

Rajab_Omar

JF-Expert Member
May 15, 2016
16,449
27,099
hajji-manara-msemaji-wa-simba_131vd8g49943p1xtl3wanj4hwq.jpg



Simba inamaliza mwaka ikiwa kileleni mwa msimamo baada ya takribani miaka 4 kuwahi kufanya hivyo huko nyuma


Msemaji wa klabu ya Wekundu wa Msimbazi Haji Sunday Manara amewakashifu watani wao wa jadi klabu ya Yanga kwa kitendo chao cha kutowalipa mishahara na posho wachezaji wake hivyo kuishi kwa kutanga tanga tanga tu


Kupitia akaunti yake ya instagram Haji Manara amewapiga kijembe Wana Jangwani kwa kitendo chao cha kujiita wa kimataifa wakati ili hali wana shindwa kuwalipa wachezaji mishahara na posho zao kwa wakati


Haji Sunday Manara ameandika " Timu inayojiita ya kimataifa wachezaji wake hawajalipwa mishahara mpaka sasa wanaish kwa vifurushi vya siku huku wakilia njaa"


Hali kadhalika msemaji huyo wa Msimbazi Haji Manara amezungumzia bahati waliyo kuwa nayo klabu ya Simba kuwa ndiyo timu pekee duniani kushabikiwa na Raisi wa nchi pamoja na Waziri Mkuu wake katika awamu mmoja ya uongozi Serikalini ".Tanzaniani nchi pekee ambayo ina Rais na Waziri Mkuu wote mashabiki wa Simba"


Kwa muda mrefu Yanga kupitia msemaji wao aliye fungiwa na TFF Jerry Muro, wamekuwa wakiwatania wapinzani wao klabu ya Simba kwa kuwaita wa mchangani huku wao wakiji nasibu ni kimataifa, hasa kutokana na ushiriki wao wa mara kwa mara kwenye michuano ya kimataifa kama klabu bingwa Afrika au Shirikisho.


Tunapomaliza mwaka 2016 1.Simba inaongoza ligi 2.Trump ni mwanaume pekee katika historia ambaye ameshinda ubishi na mwanamke 3.Tanzaniani nchi pekee ambayo ina Rais na Waziri Mkuu wote mashabiki wa Simba. 4.Neno Simba limetajwa zaidi kuliko wanyama wote. 5.Timu inayojiita ya kimataifa wachezaji wake hawajalipwa mishahara mpaka sasa wanaish kwa vifurushi vya siku huku wakilia njaa 2017 Tutaona mengi.
:D:D:D
 
Hahaha.. Huu mwaka raha sana.. Sijui hata kwanini unaisha haraka hivi?? Ila ni bora uishe tu ili tuweze kukabidhiwa mwali wetu mapemaaaa.
 
Sijawahi sikia mtukufu wetu akishabikia hii timu uchwara ila najua kuwa yule mstaafu ni yanga dam dama

Mikia kwa kujikwezaaa
 
Sijawahi sikia mtukufu wetu akishabikia hii timu uchwara ila najua kuwa yule mstaafu ni yanga dam dama

Mikia kwa kujikwezaaa
Alishaapa kuwa ni heri atazame ndondo cup kuliko kutazama wang'oa vitu
 
Afadhali JPM ni shabiki wa Simba maana nilikiwa siamini kama kwa anayo yafanya ana weza kuwa shabiki wa wa kimataifa.

Na ningegundua JPM shabik wa Yanga ningehama timu
 
Miaka mitano bila ya kombe la VPL.... Wanalikosa msimu huu... Msimu ujao watakuwa Waning'ang'ana wasishuke daraja kama 1987,1988
 
Back
Top Bottom