Manabii wa uongo na vita dhidi ya ufisadi

DoubleOSeven

JF-Expert Member
Jul 5, 2008
661
143
:pound:

•Wako wapi wale manabii wawaliotufanyisha kwata kwa muda wa miaka mitatu mfululizo bila mafao yoyote?
•Wako wapi wale manabii waliotusadikisha kuwa nchi iko vitani?
•Wako wapi wale waliohubiri katika nchi na bungeni, wakipanda jukwaa moja baada ya jingine wakipigana vita dhidi ya ufisadi?
•Wameonekana kule Dodoma wakila na kunywa huku wakiruka majoka na wale wale tulioambiwa ni mafisadi..
•Ilitarajiwa na wengi kuwa baada ya Bunge kumaliza muda wake, Manabii wale wangekuwa mstari wa mbele kupambana na wenzao wachafu ambao tuliambiwa kuwa ni mafisadi ili kuinusuru nchi.


Dhambi kubwa ya watu hawa itakayodumu milele katika kumbukumbu za wananchi ni ile ya KUVAMIA hoja njema ya Wanawema juu ya ufisadi na KUIFANYA YAO NA KISHA WAKAIUA KIHUNI.

Somo limeeleweka?

(Jarida la Siasa, Tanzania Daima ya leo)
 
Mwalimu Mkuu wa watu upeo wake na ufunuo wake wa mambo ni unabiiiiii....makala nimeisomaa ni ukweli mtupuuuuuuuu....

kibaya binadamu hasa watanzania hatukubalii ukwelii
 
Kupambana na fisadi sio kazi rahisi kama kupambana na mbu, kwa kulala kwenye net. Rostam na syndicate yake wanajitahidi kuwapa wakati mgumu wapiganaji kwenye majimbo yao, lakini naamini Mungu atawawezesha katika vita hiyo...
 
Tatizo ni sisi watanganyika wenyewe, hatuungi mkono vya kutosha wanaharakati ,mwishowe wanakata tamaa na mafisadi wanapotaka kuwatoa roho mtu huona cha kufia ni nini ???????! Ikiwa wenyewe anaowapigania wako usingizini, wenzetu wakisikia neno tu wote utawaona mitaani lakini sisi sera za ccm "chukua chako mapema ndiyo imekuwa dira yetu"
 
Kupambana na fisadi sio kazi rahisi kama kupambana na mbu, kwa kulala kwenye net. Rostam na syndicate yake wanajitahidi kuwapa wakati mgumu wapiganaji kwenye majimbo yao, lakini naamini Mungu atawawezesha katika vita hiyo...

... Mwanahalisi ya Leo: Mzee Ndimara kaandika hii...MSIMU WA MASHUSHUSHU HUU HAPA....Waliomwona Mrema (Mzee wa Kiraracha) akicheza ngoma na kutupiwa sisenti kwenye mkutano Mkuu wa CCM wiki mbili zilizopita; huku akitetea cham hicho kuliko makada wake, watakuwa WAMEGUNDUA kuwa hakuwa Mwanamageuzi bali ALIKUZWA na MFUMO unaoendesha vitaarifa dhalili vya kishushushu..
NAONGEZA: MFUMO pia unahusishwa na UVUMI mkali unaovumishwa kila mara ku-disinform na ku-destabilize DEMOCRACY ya kweli hapa TZ
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom