Singida ndio home
JF-Expert Member
- Feb 23, 2012
- 3,192
- 3,353
Man Water ni miongoni mwa ma producer hodari aliewatoa wasanii wengi kama kina 20% ila baada ya kutoelewana 20% akapotea.
Katika mahojiano na Azam TV, amesema kuwa kuna nyimbo kadhaa alizofanya na msanii Ali Kiba lakini hawajazirelease kwa sababu hazijalipiwa.
Anasema kuwa licha ya kwamba alishiriki kupiga promo kuwa kazi nyingi zinakuja lakini walitoa “Seduce Me” na “Mvumo wa Radi” pekee kwa sababu ndizo zilizolipiwa.
“Pamoja na mimi kusubiri malipo ya hizi nyimbo ili nipate maslahi, nazisikia zikiwa zimerudiwa kwingine huko na zimeshatoka hivyo mimi ni kama nimebaki na makapi ilhali ndio nilikuwa source” anazidi kulalamika Man Water
Hadi sasa Man Water amesema hana hamu ya kufanya kazi na Kiba.
My Take:
Kiburi cha Alikiba hadi kwa producer ni aibu tupu, kayumba sana kumkera uyu jamaa ambae ni fundi anaejua.
Kwa sasa Ali Kiba ameamua kuwa na studio yake ya Kings music ila naweza kusema kwamba ni ya kawaida sana.