Mamlaka itafakari na kuwaonea huruma askari wa chini wa Magereza kwani ndio wahanga wa maamuzi ya leo na kutoa vibali vya ajira kwa jeshi la Magereza

Masamila

JF-Expert Member
Jun 22, 2014
6,411
7,306
Miaka ya 2011 au 2012 mimi binafsi bila kuhadithiwa nilishuhudia askari mmoja wa jeshi la Magereza kijana mdogo asie na cheo (rank yake inaitwa Warder) akihangaika kumuulizia mitaani pale Mpwapwa mjini mfungwa alie mtoroka.

Askari yule akiwa peke yake alikuwa akiliswaga na kulilinda kundi la wafungwa kama 10 hivi akipita na lile kundi la wafungwa mitaa ya Mpwapwa mjini karibu na Gereza lake ambalo ni gereza la wilaya ya Mpwapwa na wafungwa wale wakiwa wameshika viboko wakimfuatilia yule mfungwa alietoroka.

Hii ni jinsi gani askari wa hilo Jeshi walivyo na mazingira magumu ya kazi , nilimshuhudia askari yule akitembea kwa miguu huku akiwa ana silaha/bunduki inayobeba risasi 10 tu Bunduki aina ya S.A.R huku akiliswaga kundi hilo kubwa la wafungwa peke yake na niliwashudia pia wale wafungwa baadhi yao wakimkashifu kwa kuwa nyuma.

Jeshi la Magereza wana mazingira magumu ya kazi ,hawana magari ya kutosha wanatembeaga kwa miguu wafungwa kwa askari , sijawahi kuona jeshi hilo likimiliki wanyama aina ya farasi au ndege aina ya Helikopta kama mojawapo ya vitendea kazi.

Askari huyo nina uhakika kama taratibu za jeshi hilo zinavuokuwa kwa askari anaepoteza mfungwa alikuja kuzuiwa kupanda cheo kwa miaka kadhaa na hivyo kubaki chini na rank ya Warder.

Naisihi mamlaka itengue maamuzi yake ya kulinyima jeshi la Magereza kibali cha kuajiri ,kwani kwa hakika maamuzi haya yanawaumiza zaidi askari ambao hawana vyeo na wenye cheo cha chini cha koplo kwani hao ndio hushika silaha kushinda na wafungwa (waliowahi kuwa majeshini wanajua uhalisia wa majeshi askari wa ngazi mbili za mwisho chini huwa ndio wanapitia msoto/mzigo mkubwa wa majukumu ya jeshi).

Askari hawa wa vyeo vya chini wataendelea kupata kazi changamoto ya kuswaga na kulinda makundi makubwa ya wafungwa maporini na vichakani na kuendelea kuadhibiwa pindi wanapotorokewa.

Na pia wanapata changamoto kwa kuwa wachache, waliofikisha wakati wa kustaafu wakistaafu na ilhali magereza mengi kama sio yote yamejaza watu kuliko uwezo wake , na mazingira ya kazi ni magumu.

Mamlaka na sisi wananchi kiujumla tungetambua kwamba askari magereza kiujumla ni watumishi wazalendo,wachapakazi na wakakamavu kwelikweli hivyo tunakuwa na deni la kiungwana la kuwathamini na kuwajali.

Nimalizie kwa wito kwa Mheshimiwa kutafakari upya mtazamo wake na pia atafakari pia na kuwasaidia jeshi hilo kwa kuwanunulia vitendea kazi kama farasi na magari na pia bila kusahau kujenga zaidi magereza mengine sababu taifa letu idadi ya wanachi inaongezeka kwa kasi na idadi ya wafungwa na mahabusu nayo inaendelea na itaendelea kuongezeka.
 
Magereza na wao wanahusika kuwalinda CCM?

Kama na wao wanahusika acha tu waendelee kula msoto, na wengi wao pombe kali na bangi ndio faraja yao kwa kuwa wanakaa sana juani.

Askari Magereza ni mfungwa aliye na jezi na bunduki.
 
Tuendelee kuwahimiza walimu jaman
Walimu wa watoto wetu wapo mashakani kimaslai na hata mishahara duni na maslai yao
Taifa letu la kesho lipo kwa watoto wetu na sio kwa wafungwa wa nchi hii
Tupambane kuona maslai ya walimu yanaboreshwa na walimu wanatoa elimu bora kwa watoto wetu
Nadhani umenielewa
 
Magereza na wao wanahusika kuwalinda CCM?

Kama na wao wanahusika acha tu waendelee kula msoto, na wengi wao pombe kali na bangi ndio faraja yao kwa kuwa wanakaa sana juani.

Askari Magereza ni mfungwa aliye na jezi na bunduki.

Ni jeshi ambalo halina muingiliano mkubwa na wanasiasa

Maamuzi ya mheshimiwa rais yatawaathiri askari kapera na wanyonge waliokuwa wanasubiri kupandishwa cheo kutoka ukoplo hadi usajini kwani kwani kwa kunyimwa kibali cha kuajiri jeshi itabidi liwazuie waliokuwa kwenye mbavu mbili wasipande ,askari hawa ambao wanasubiri kwa hamu,shauku na subira kupata motisha hiyo ya kupandishwa cheo
 
Tuendelee kuwahimiza walimu jaman
Walimu wa watoto wetu wapo mashakani kimaslai na hata mishahara duni na maslai yao
Taifa letu la kesho lipo kwa watoto wetu na sio kwa wafungwa wa nchi hii
Tupambane kuona maslai ya walimu yanaboreshwa na walimu wanatoa elimu bora kwa watoto wetu
Nadhani umenielewa

Waalimu mbona mna mazingira mazuri kama utalinganisha na askari jela mkuu

Askari jela kwa amzingira hayo magumu ya kazi ,akitorokewa na mfungwa huwa anapigwa adhabu ya kutopanda cheo na seniority yake kwa miaka mitano , waalimu nyie miaka mitatu tu unapandishwa cheo kizingatio ni OPRAS tu
 
Miaka hyo.Enz za Jk!!! Mkwele!!!

Huko Jkt ajira zilikua nyingi......Majeshin mfano mwenye elimu kuanzia form four.... Service men!!! Alikua na uwezo wa kuchagua kwenda!!!

Jwtz/Tiss/Tpa/Tanapa/police/Migration/.......

Yaani kiufupi Magereza na Fire watu walikua wanazikimbia!!!!na kujifichaaa

Lakin sasa hiv hata hizo zilizokimbiwa zimekua almas!!!!...

Oooh Bado Minne
 
mimo sijaona huo ugumu unaosemea uko wapi hapo.

una bunduki ya risasi 30,maana yake atakayeleta ujuaji vunja mguu.
halafu si huwa mnapewa kutoka na wafungwa waliokaribia kumaliza kifungo!!!hizo bangi za kutoroka zinawapandia wapi???

kwanza nikajua ukitorokwa na mfungwa unafungwa wewe,kumbe unanyimwa cheo ambacho nacho ni kama hakina faida,maana maslahi ni mbuzi.
 
Manyumbu lini tutaanza kutoka mashimoni?mtoa hoja elewa mfungwa anapotoroka jela au kwingineko inakuwa ni polisi case wao ndio unakua wajibu wao na wao wanaweza omba msaada wa tiss au kitengo maalum katika kumsaka fugitive sio kazi ya warder!!
 
Magereza na wao wanahusika kuwalinda CCM?

Kama na wao wanahusika acha tu waendelee kula msoto, na wengi wao pombe kali na bangi ndio faraja yao kwa kuwa wanakaa sana juani.

Askari Magereza ni mfungwa aliye na jezi na bunduki.
Mwaka jana kwenye uchaguzi gari lao lilitumika kusambaza na kubandika mabango ya CCM Dodoma.

Hata hivyo ni vyema kuwatetea, wanafanya kazi katika mazingira magumu sana, mara nyingi hata wao wanaambukizwa magonjwa kama kifua kikuu kwasababu ya mazingira ya kazi, WaTz tusichoke kuteteana, infact tuwatete hata buku 7 sababu zimepunguzwa na kuwa buku 5, kila mtu anaisoma namba isipokuwa wale wa Chamwino, labda.... labda na Kebbys 😀😀😀

Usipoisoma namba kwa kukosa pesa utaisoma kwa kusimangwa na mkulu kila siku hadi ukose hamu na kazi/Cheo.
 
Miaka hyo.Enz za Jk!!! Mkwele!!!

Huko Jkt ajira zilikua nyingi......Majeshin mfano mwenye elimu kuanzia form four.... Service men!!! Alikua na uwezo wa kuchagua kwenda!!!

Jwtz/Tiss/Tpa/Tanapa/police/Migration/.......

Yaani kiufupi Magereza na Fire watu walikua wanazikimbia!!!!na kujifichaaa

Lakin sasa hiv hata hizo zilizokimbiwa zimekua almas!!!!...

Oooh Bado Minne
ata enzi za Jk. tofauti ni kuwa haya majeshi yameondolewa dhamana ya kuajiri.
sikukz mpaka kibali kitoke ikulu.

zaman wao wenyewe walikuwa na uwezo wa kuajiri.
wao kama wao.
 
Ila kota zao aisee. Serikali itazame hilo.
Swala la kota mimi huwa nawalaumu viongozi wa magereza wenyewe labda kama takuwa sijui taratibu za serikali, hivi inakuwaje magereza wanaishi nyumba zilizochoka wakati wananguvukazi ya kutosha kufyetua matofali ya kutosha na kujenga nyumba, tena za kisasa kwa kuwatukia hao hao wafungwa, bila serikali kuweka hata senti tano. Wanachopaswa kufanya wafyetue tofali za kutosha zingine wajengee nyumba zao,, zingine wauze kwa ajili ya kupata pesa za bati, mbao madirisha na milango.

Ni maajabu sana kuona askari. magereza wanaishi kwenye makazi duni, mimi huwa nahisi pengine kuna sheria zinawazuia kuishi au kujenga makazi bora. Na haya maajabu pia yapo kwenye shule za ufundii, waalimu wanakosa nyumba za kuishi ilhali shule ina eneo kubwa ambalo wanafunzi wangejenga nyumba za waalimu kama sehemu ya mafuzo yao kwa vitendo. Ki ukweli haya ni maajabu makubwa na siamini kama serikali inazuia haya mambo yasifanyike, nahisi tatizo lipo kwa watendaji na wasimamizi waliopewa dhamana, ni kama bado wanaishi kwenye kale ka usemi cha lack of capital.
 
Mkuu tangia lini SAR ikabeba risasi 30 ? Yule Warder alikuwa na SAR akiwa peke yake na wafungwa kama 10

Ila sio fair Uhamiaji wawe wanapewa vibali halafu mnawanyima Magereza Mkuu

mimo sijaona huo ugumu unaosemea uko wapi hapo.

una bunduki ya risasi 30,maana yake atakayeleta ujuaji vunja mguu.
halafu si huwa mnapewa kutoka na wafungwa waliokaribia kumaliza kifungo!!!hizo bangi za kutoroka zinawapandia wapi???

kwanza nikajua ukitorokwa na mfungwa unafungwa wewe,kumbe unanyimwa cheo ambacho nacho ni kama hakina faida,maana maslahi ni mbuzi.
 
Haya Order imetoka kwamba jeshi lilime sana ,Je watalima kwa kutumia hao Wafungwa wachache wanaokaribia kumaliza vifungo ?

mimo sijaona huo ugumu unaosemea uko wapi hapo.

una bunduki ya risasi 30,maana yake atakayeleta ujuaji vunja mguu.
halafu si huwa mnapewa kutoka na wafungwa waliokaribia kumaliza kifungo!!!hizo bangi za kutoroka zinawapandia wapi???

kwanza nikajua ukitorokwa na mfungwa unafungwa wewe,kumbe unanyimwa cheo ambacho nacho ni kama hakina faida,maana maslahi ni mbuzi.
 
Back
Top Bottom