Mamlaka iliyomteua Sabaya na kutomtumbua, inahusika pia na hukumu hii

Mindi

JF-Expert Member
Apr 5, 2008
3,523
4,991
Sabaya amehukumiwa kifungo cha miaka 30 kwa ujambazi wa kutumia silaha. Katika kujitetea, mara nyingi amesema kwamba alikuwa anatekeleza maagizo ya mamlaka iliyomteua.
Kwa maoni yangu, hata bila utetezi wake huo, kitendo cha mamlaka ya uteuzi kunyamazia vitendo vyake vya ujambazi, ni kuhusika moja kwa moja. Angalau tunaweza kumwondolea uhusika Rais Samia, kwa kuwa aliamua kuchukua hatua.
Najua kwamba Sabaya ni mbuzi wa kafara tu. Magufuli na idadi kubwa ya wateule wake, sio tu wamehusika na ujambazi, wizi, uporaji wa mali na hata binadamu, na wizi wa kura, lakini wamehusika pia na utekaji, utesaji na mauaji ya wanasiasa ambao walikuwa na msimamo tofauti na Magufuli.

Hata kama Magufuli hayupo hai, ipo haja ya kufungua kesi dhidi yake, na dhidi ya wateule wengine, kutumia ushahidi na hukumu dhidi ya Sabaya, ili angalau haki itendeke kwa wengine kama Ben Saanane, Alfons Mawazo, Tundu Lissu, Azory Gwanda, na maelfu ya waliovunjiwa nyumba zao, nk.
 
Huyu Sabaya atatoka kwa msamaha wa Raisi na si ajabu katika kuazimisha sherehe za uhuru mwaka huu mwezi December.

CCM ni ile ile ila uzuri kaenda jela na mpaka hapo ana la kujutia.
 
Kwahiyo uko sahihi kabisa kwa sababu kwa namna kesi ilivyoendeshwa nimegundua kuna viongozi wengi wakati wa magufuli walikuwa ni wezi na nikikumbuka issue ya Uvamizi wa clouds , majigambo ya Musiba , Mambosasa , ,Makonda nadiriki kusema ipo haja watu wakamtwe wahokjiwe inawezeka wapo watu wanajua au wamepitia madhila Kutoka kwa watu hawa
 
Huyu Sabaya atatoka kwa msamaha wa Raisi na si ajabu katika kuazimisha sherehe za uhuru mwaka huu mwezi December.

CCM ni ile ile ila uzuri kaenda jela na mpaka hapo ana la kujutia.
Makosa ya unyanganyi wa kutumia silaha, ujangili, ubakaji na mauaji huwa hayamo ktk msamaha wa wafungwa. Kwa hukumu ya kifo kwa mfano, msamaha pekee huwa ni kubatilisha hukumu ya kunyongwa na kuwa kifungo cha maisha

Vv
 
Makosa ya unyanganyi wa kutumia silaha, ujangili, ubakaji na mauaji huwa hayamo ktk msamaha wa wafungwa. Kwa hukumu ya kifo kwa mfano, msamaha pekee huwa ni kubatilisha hukumu ya kunyongwa na kuwa kifungo cha maisha

Vv
Kina Babu Seya waliofungwa kwa kuingilia watoto wadogo tena wa shule mbona waliachiwa kwa msamaha wa Raisi ?
 
Sabaya amehukumiwa kifungo cha miaka 30 kwa ujambazi wa kutumia silaha. Katika kujitetea, mara nyingi amesema kwamba alikuwa anatekeleza maagizo ya mamlaka iliyomteua.
Kwa maoni yangu, hata bila utetezi wake huo, kitendo cha mamlaka ya uteuzi kunyamazia vitendo vyake vya ujambazi, ni kuhusika moja kwa moja. Angalau tunaweza kumwondolea uhusika Rais Samia, kwa kuwa aliamua kuchukua hatua.
Najua kwamba Sabaya ni mbuzi wa kafara tu. Magufuli na idadi kubwa ya wateule wake, sio tu wamehusika na ujambazi, wizi, uporaji wa mali na hata binadamu, na wizi wa kura, lakini wamehusika pia na utekaji, utesaji na mauaji ya wanasiasa ambao walikuwa na msimamo tofauti na Magufuli.

Hata kama Magufuli hayupo hai, ipo haja ya kufungua kesi dhidi yake, na dhidi ya wateule wengine, kutumia ushahidi na hukumu dhidi ya Sabaya, ili angalau haki itendeke kwa wengine kama Ben Saanane, Alfons Mawazo, Tundu Lissu, Azory Gwanda, na maelfu ya waliovunjiwa nyumba zao, nk.
Tulia bwa mdogo..unapoapa unachukua mamlaka bmya kulinda katiba na sheria za nchi....huapi kumsukiliza Rais... dogo mshamba tu huyo wacha atumikie ujana wake jela...atapiga punye hadi akome..shenzi tu

Ndiyo maana nimelwambia hayo mengime yanakuja..mdogo mdogo.. PGO
 
Tulia bwa mdogo..unapoapa unachukua mamlaka bmya kulinda katiba na sheria za nchi....huapi kumsukiliza Rais... dogo mshamba tu huyo wacha atumikie ujana wake jela...atapiga punye hadi akome..shenzi tu

Ndiyo maana nimelwambia hayo mengime yanakuja..mdogo mdogo.. PGO
Mmmhhh.....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom