Mamlaka husika ichunguze uthabiti wa chanjo ya kuku ya Tatu Moja

3 Angels message

JF-Expert Member
Aug 3, 2017
4,877
13,555
Wasalaam wakuu,

Kwa sisi wafugaji hasa wa kuku hivi karibuni tulipata afuheni ya chanjo mara baada ya kuingia sokoni kwa chanjo ya kuku ya tatu moja ambayo kwa maelezo inatoa kinga kwa magonjwa matatu Newcastle, mafua na ndui ambayo hapo awali ilihitajika uingie gharama kununua chanjo hizo tofauti tofauti.

Lakini sasa pamekuwa na malalamiko kadhaa kuwa hii chanjo haipo vizuri kwenye kukinga hayo magonjwa maana kuna baadhi waliochanja kuku wao ila Newcastle ilipowakumba iliwafagia kuku wote na hata mafua kinyume na matarajio na hivyo kuingia hasara kubwa.

Na baadhi ya madaktari wa mifugo wanadai hii chanjo haina nguvu hiyo inayosemwa na wanapendekeza bora utumie chanjo ya Newcastle yenyewe halafu uichanganye na hiyo tatu moja.

Ili kuondoa huu mkanganyiko ni vyema mamlaka husika watusaidie hii chanjo ya 3 moja imefanyiwa utafiti kweli na inafaa au laa ili kutuondolea hasara na huu mkanganyiko uliopo sasa juu ya uimara wake kukabiliana na hayo magonjwa.
 
Unafuga kuku mazingira machafuuuu maranda unabadili mara moja kwa mwezi! Unamwagamwaga maji kunanukaaaa halafu UNATAKA TATU MOJA IKUSAIDIE kukufugia kuku!?

We tafuta mlalamishi hata mmoja mwambie mwende kwake kama atakubali! Kuna wafugaji wapuuzi sana
 
Unafuga kuku mazingira machafuuuu maranda unabadili mara moja kwa mwezi! Unamwagamwaga maji kunanukaaaa halafu UNATAKA TATU MOJA IKUSAIDIE kukufugia kuku!?

We tafuta mlalamishi hata mmoja mwambie mwende kwake kama atakubali! Kuna wafugaji wapuuzi sana
Hayo ya kufundisha usafi kwa wafugaji yaanzishie uzi wake mkuu ila leo ni kutaka kujua ufanisi wa hii chanjo ni wa uhakika kweli maana inalalamikiwa sana kuwa haifanyi vizuri kwenye kukinga
 
Hayo ya kufundisha usafi kwa wafugaji yaanzishie uzi wake mkuu ila leo ni kutaka kujua ufanisi wa hii chanjo ni wa uhakika kweli maana inalalamikiwa sana kuwa haifanyi vizuri kwenye kukinga
nakupa siri ya ufugaji!

mazingira yakiwa safi kuku hata bila chanjo anatoboa! mie nina mwaka wa 3 nafuga bila chanjo sio broiler wala chotara wala kienyeji! we nifuate PM ntakusidia maujuzi na wala hauna gharama!

shida kubwa wafugaji hawafuati masheriti hata Lishe tu shida!
 
Chanjo yoyote ni kama bahati nasibu, uhakika wa matokeo hasi na changya ni 50/50.

Unaweza ukachanja na bado isisaidie!
 
nakupa siri ya ufugaji!

mazingira yakiwa safi kuku hata bila chanjo anatoboa! mie nina mwaka wa 3 nafuga bila chanjo sio broiler wala chotara wala kienyeji! we nifuate PM ntakusidia maujuzi na wala hauna gharama!

shida kubwa wafugaji hawafuati masheriti hata Lishe tu shida!
Naomba uweke hapa maujuzi yako kwa faida na sisi tuonatarajia kuingia kwenye ufungaji wa kuku
 
Naomba uweke hapa maujuzi yako kwa faida na sisi tuonatarajia kuingia kwenye ufungaji wa kuku
Kuku anapitia magonjwa mengi sananje ya hizo chanjo zenu mnazokomaa nazo! kwa anayefuga kuanzia vifaranga atanielewa hapa!

Sasa kama haujui dawa (sio chanjo) za kuanza na kuku kama kinga utateseka sana! malezi ya kuku ni wiki mbili za mwanzo! baada ya hapo wanakuwa wanajielewa
 
nakupa siri ya ufugaji!

mazingira yakiwa safi kuku hata bila chanjo anatoboa! mie nina mwaka wa 3 nafuga bila chanjo sio broiler wala chotara wala kienyeji! we nifuate PM ntakusidia maujuzi na wala hauna gharama!

shida kubwa wafugaji hawafuati masheriti hata Lishe tu shida!
Sawa mkuu
 
Inabidi kujua wizara ina maelezo gani kwenye hili kwa sababu binafsi nimeshasikia malalamiko kama hayo......ugonjwa wa kideri siyo wa kufanyia majaribio ya chanjo ambazo hazijathibitishwa ubora wake ikizingatiwa kwamba taasisi ya chanjo kibaha tayari wanayo chanjo ambayo imetumika miaka mingi sasa kuuthibiti huo ugonjwa hasa kwa kuku wa kienyeji. Kuanza kuingiza na kutumia chanjo zisizo thibitishwa ubora wake kunaenda kurudisha nyuma kabisa jitihada ambazo zilishawekwa kwa miaka mingi kwenye kuthibiti ugonjwa kideri na sidhani kama wizara ipo tayari kuona hili likitokea.............​
 
Wasalaam wakuu,

Kwa sisi wafugaji hasa wa kuku hivi karibuni tulipata afuheni ya chanjo mara baada ya kuingia sokoni kwa chanjo ya kuku ya tatu moja ambayo kwa maelezo inatoa kinga kwa magonjwa matatu Newcastle, mafua na ndui ambayo hapo awali ilihitajika uingie gharama kununua chanjo hizo tofauti tofauti.

Lakini sasa pamekuwa na malalamiko kadhaa kuwa hii chanjo haipo vizuri kwenye kukinga hayo magonjwa maana kuna baadhi waliochanja kuku wao ila Newcastle ilipowakumba iliwafagia kuku wote na hata mafua kinyume na matarajio na hivyo kuingia hasara kubwa. Na baadhi ya madaktari wa mifugo wanadai hii chanjo haina nguvu hiyo inayosemwa na wanapendekeza bora utumie chanjo ya Newcastle yenyewe halafu uichanganye na hiyo tatu moja.

Ili kuondoa huu mkanganyiko ni vyema mamlaka husika watusaidie hii chanjo ya 3 moja imefanyiwa utafiti kweli na inafaa au laa ili kutuondolea hasara na huu mkanganyiko uliopo sasa juu ya uimara wake kukabiliana na hayo magonjwa.

Ww unaongelea chanjo ya kuku haifanyi kazi, unajua chanjo ya binadamu pia haifanyi kazi kwa 100%, wako waliochanja na wamekwenda na maji. Kuku na binadamu yupi ana thamani zaidi. Hizi chanjo lazima iwe imefanyiwa majaribio miaka kadhaa ndio ujue how effective it is.
 
Ww unaongelea chanjo ya kuku haifanyi kazi, unajua chanjo ya binadamu pia haifanyi kazi kwa 100%, wako waliochanja na wamekwenda na maji. Kuku na binadamu yupi ana thamani zaidi. Hizi chanjo lazima iwe imefanyiwa majaribio miaka kadhaa ndio ujue how effective it is.
Nisome hapo juu utaelewa ni nini mleta mada anakiwasilisha hapa.......
 
Inabidi kujua wizara ina maelezo gani kwenye hili kwa sababu binafsi nimeshasikia malalamiko kama hayo......ugonjwa wa kideri siyo wa kufanyia majaribio ya chanjo ambazo hazijathibitishwa ubora wake ikizingatiwa kwamba taasisi ya chanjo kibaha tayari wanayo chanjo ambayo imetumika miaka mingi sasa kuuthibiti huo ugonjwa hasa kwa kuku wa kienyeji. Kuanza kuingiza na kutumia chanjo zisizo thibitishwa ubora wake kunaenda kurudisha nyuma kabisa jitihada ambazo zilishawekwa kwa miaka mingi kwenye kuthibiti ugonjwa kideri na sidhani kama wizara ipo tayari kuona hili likitokea.............​
Kabisa mkuu, huyu Dr ambaye nilikuwa naye jana akiwafanyia uchunguzi kuku waliokufa alisema hii chanjo ya tatu moja wao (maana yupo pale maabara veterinary tmk) hawajaithibitisha hii chanjo na akasisitiza bora kutumia chanjo ya Newcastle ambayo wao ndiyo wanaitengeneza na kuisambaza kwani ndiyo imethibitishwa

Sasa ili kuwasaidia wafugaji wetu ni vyema wizara au mamlaka husika itoe muongozo hii chanjo ya tatu moja ni sahihi maana wengi tunaikimbilia maana pia inasaidia kupunguza gharama lkn ufanisi wake ndiyo una uwalakini
 
nakupa siri ya ufugaji!

mazingira yakiwa safi kuku hata bila chanjo anatoboa! mie nina mwaka wa 3 nafuga bila chanjo sio broiler wala chotara wala kienyeji! we nifuate PM ntakusidia maujuzi na wala hauna gharama!

shida kubwa wafugaji hawafuati masheriti hata Lishe tu shida!
Usafi ndio chanjo ya Magonjwa ?

Nini maana ya Chanjo ?; Kwahio jamaa kama mchafu ndio wauzaji chanjo wasiwajibishwe hata kama chanjo yao haikidhi vigezo
 
Unafuga kuku mazingira machafuuuu maranda unabadili mara moja kwa mwezi! Unamwagamwaga maji kunanukaaaa halafu UNATAKA TATU MOJA IKUSAIDIE kukufugia kuku!?

We tafuta mlalamishi hata mmoja mwambie mwende kwake kama atakubali! Kuna wafugaji wapuuzi sana
Mbona umekua mkali kama mbwa mwenye mimba?
 
Inabidi kujua wizara ina maelezo gani kwenye hili kwa sababu binafsi nimeshasikia malalamiko kama hayo......ugonjwa wa kideri siyo wa kufanyia majaribio ya chanjo ambazo hazijathibitishwa ubora wake ikizingatiwa kwamba taasisi ya chanjo kibaha tayari wanayo chanjo ambayo imetumika miaka mingi sasa kuuthibiti huo ugonjwa hasa kwa kuku wa kienyeji. Kuanza kuingiza na kutumia chanjo zisizo thibitishwa ubora wake kunaenda kurudisha nyuma kabisa jitihada ambazo zilishawekwa kwa miaka mingi kwenye kuthibiti ugonjwa kideri na sidhani kama wizara ipo tayari kuona hili likitokea.............​
Tuna weak systems za kudhibiti ubora wa baadhi ya pembejeo

So concerns za quality ya chanjo ni valid
 
Tuna weak systems za kudhibiti ubora wa baadhi ya pembejeo

So concerns za quality ya chanjo ni valid
Soko limekuwa holela sana mkuu kila mtu anaingiza sokoni kila kitu bila ubora wake kuthibitishwa na hatimaye kuleta hasara kwa watumiaji na wengine kwa nguvu waliyonayo wanaweza kuhakikisha bidhaa yao ndiyo itumike kuliko nyingine hata kama haina uwezo
 
Back
Top Bottom