'Mamia' wampokea Kikwete

NakuliliaTanzania

JF-Expert Member
Sep 24, 2007
555
7
Mi nilidhani wangekuwa maelfu, halafu kumbe ni wanachama wa CCM..so ningedhani ingekuwa mamia ya wana CCM....au ndo kujaribu kufunika ishu?


Habari za Kitaifa

Mamia wampokea Kikwete

Mwandishi Wetu

HabariLeo; Monday,October 08, 2007 @00:04

MAMIA ya watu jana walifurika katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kumpokea Rais Jakaya Kikwete aliyerejea nchini baada ya ziara ndefu ya Marekani.

Watu hao akiwamo Waziri Mkuu Edward Lowassa, mawaziri kadhaa na wanachama wa CCM waliokuwa wamevalia mavazi ya njano na kijani walifurika uwanjani tangu saa saba mchana, wakimsubiri Rais Kikwete aliyewasili baada ya saa moja.

Umati huo wa watu ulikuwa ukiburudishwa na nyimbo maarufu za John Komba wa TOT huku wakiwa wameshika mabango ya kumkaribisha nyumbani rais.

Mengi ya mabango yalisomeka ‘Karibu nyumbani Rais Kikwete.’

Baada ya kuwasili, Rais Kikwete alitoka nje ya eneo la kupumzika wageni mashuhuri (VIP) na kwenda nje kuwasalimia wananchi hao waliokuwa wamefurika ambao nao walimshangilia kwa makofi na vigelegele kabla ya kuondoka kuelekea Ikulu kwa ajili ya mapumziko.

Ziara hiyo ya rais ya wiki tatu nchini Marekani imeelezwa kuwa na mafanikio kutokana na kuiwezesha Tanzania kupatiwa kiasi kikubwa cha fedha kuliko kilichowahi kutolewa kwa nchi yoyote chini ya Mpango wa Millennium Challenge Corporation(MCC).

Mtendaji Mkuu wa MCC, Balozi Johyn Damilovich alimueleza rais uamuzi wa bodi ya shirika hilo kuidhinisha fedha za kugharamia miradi mikubwa ya uwekezaji nchini. Fedha hizo siyo mkopo.

MCC imeidhinisha dola za Kimarekani milioni 699 (Sh bilioni 881), kiasi ambacho ni kikubwa zaidi kuliko kilichowahi kutolewa kwa nchi yoyote duniani na MCC. Miongoni mwa miradi itakayonufaika na fedha hizo ni ile ya ujenzi wa miundombinu.

Taarifa iliyotolewa na Ikulu juzi ilisema kuwa Marekani iliahidi kuendelea kuisaidia Tanzania katika maeneo mbalimbali ikiwamo eneo la kijeshi.

Katika eneo la uwekezaji kampuni kadhaa zimeonyesha nia ya kujenga viwanja vya mbolea nchini na miradi mingine. Miongoni mwa makampuni hayo ni JP Morgan, Merrill Lynch, Tegris na Gilbraltar Properties.

Wakati wa ziara yake nchini humo aliyoianza Septemba 15, Rais Kikwete alizindua matangazo ya vivutio vya utalii wa Tanzania katika televisheni ya kimataifa ya CNN huku kampuni kadhaa zikionyesha kukubali kuwekeza nchini katika sekta ya utalii ikiwamo kampuni maarufu ya mahoteli ya Global Hyatt Corporation ambayo imekubali kuja nchini kuangalia maeneo ya kujenga mahoteli.

Rais pia alizindua maandalizi ya Tanzania kuwa Mwenyekiti wa Mkutano wa 33 wa Utalii Afrika uliopangwa kufanyika Mei mwakani mjini Arusha.
http://www.dailynews-tsn.com/habarileo/page.php?id=4431
 
huyu mwandishi hajui protocal au ndio wanamtandao wamebadili..mnajua aliyeongoza mapokezi ni makamu wa rais shein...mbona wanamfanya kama hayupo??? alafu wale walioenda pale walikusanywa na mabasi na kupewa buku tano kila mmoja kama chai....wengine wasaniii wa mjini wanahojiwa wanajifanya wamesafiri toka tanga maalum kumlaki muhashimiwa....
 
Nafikiri huyu mwandishi anajipendekeza kwa EL kwani aliyempokea JK ni Shein, kwa vile shein sio mwanamtandao basi hakuonekana. Kuna ajenda ya siri ya kumpigia Ndanda Kosovo debe la 2015 na huu ni mpango mahsusi wa mafisadi, ni lazima tusimame kidete kupambana nao
 
huyu mwandishi hajui protocal au ndio wanamtandao wamebadili..mnajua aliyeongoza mapokezi ni makamu wa rais shein...mbona wanamfanya kama hayupo??? alafu wale walioenda pale walikusanywa na mabasi na kupewa buku tano kila mmoja kama chai....wengine wasaniii wa mjini wanahojiwa wanajifanya wamesafiri toka tanga maalum kumlaki muhashimiwa....


OOh poor Shein nadhani historia itamhukumu kuwa 'hakushiriki nao' ndo maana huyu mwandishi wetu hakumwona, na kama unavosema hakujali protokali...
 
hadi jumatatu mchana kwa saa za uingereza na marekani na tanzania, oneni watu wakavyomponda Muungwana kwa kuwa kapokewa na watu wengi ! hapo ndipo utakapojua watengenezaji propaganda !
 
hadi jumatatu mchana kwa saa za uingereza na marekani na tanzania, oneni watu wakavyomponda Muungwana kwa kuwa kapokewa na watu wengi ! hapo ndipo utakapojua watengenezaji propaganda !

Lakini Kaka Kada Embu tuwe wakweli kidogo Muungwana!Hivi kwa nini Jk anapokewa kwa makeke namna hiyo?Kuna nini kinataka kuelezwa hapa?Au safari yake hii ya Marekani imekuwa na Mafanikio kuliko alizowahi kufanya huko mwanzoni?.Au wananchi wamefurahi kwamba amerudi salama kwa sababu Medical check up huko Ufaransa iliwapa wasiwasi labda Jk ana tatizo kubwa?.Na wala sio kweli kwamba watu wapo hapa kumshambulia Muungwana!TUTAMPONGEZA atakapomuondoa Kaka Karamagi katika Cabinet!
 
hadi jumatatu mchana kwa saa za uingereza na marekani na tanzania, oneni watu wakavyomponda Muungwana kwa kuwa kapokewa na watu wengi ! hapo ndipo utakapojua watengenezaji propaganda !


kada acha upenzi..hata wengine ccm lakini ukweli lazima usemwe ...jk kapoteza umaarufu..source za waliokuwa uwanjani zinasema hakuwa na ile kicheko chake cha kawaida ...ana mawazo mengi..na hata katika haliisiyo ya kawaida aliwakwepa waandishiambao siku zote ni marafiki zake...ni wa kumuonea huruma for sure..

tofauti na ule umati unaomlaki kila mara wa jana ulikuwa wa kulazimisha....watu walisombwa na mabasi na nauli juu..na wala hawakuwa wengi ...wapo wachache walioenda kwa moyo na walikereka sana na kitendo cha wengi walopelekwa pale kuvaa magwanda...capt komba alifanya kazi kubwa sana ya kuiimba ili kuendelea kuvutia watu pale uwanjani...it was no as usual....hata jk atakuwa amegundua kuwa ule umati haukuwa wa rohoni kama wakati mwingine...
 
hadi jumatatu mchana kwa saa za uingereza na marekani na tanzania, oneni watu wakavyomponda Muungwana kwa kuwa kapokewa na watu wengi ! hapo ndipo utakapojua watengenezaji propaganda !

KM (kuwadi wa mafisadi) sijakuelewa hata kidogo unachoongea.
 
Mawaziri wote hao wameacha kazi zao, familia zao, ndugu zao, majimbo yao ili tu kwenda kumpokea Muungwana airport?

Tanzania bado tumelala sana. Hayo masaa tunayopoteza airpot si tungetumia kwenye uzalishaji? kwenye kutatua shida za watu? Kwenye kuhimiza mambo ya maendeleo?

Nashangaa kila siku watu wako VIP lounge, eti hata wabunge ni VIP. Hivi mtu kama Zitto akitelemkia kule kwa wananchi wengine kutatokea nini?

Hivi hawa CCM, CHADEMA, TLP, CUF, wanapingana nini? Naona mambo yao yote yanafanana. Kila mmoja anajifanya ni VIP, kila mmoja kakimbilia shangingi badala ya hizo pesa kununua vitabu vya shule, kila mmoja kwenye kura ya kupandisha mishahara yao, anasema ndio.

Sisi kweli tumelala, tunacheza mdundiko wao bila kujua ulikoanzia wala utakako ishia.
 
Mawaziri wote hao wameacha kazi zao, familia zao, ndugu zao, majimbo yao ili tu kwenda kumpokea Muungwana airport?

Tanzania bado tumelala sana. Hayo masaa tunayopoteza airpot si tungetumia kwenye uzalishaji? kwenye kutatua shida za watu? Kwenye kuhimiza mambo ya maendeleo?

Nashangaa kila siku watu wako VIP lounge, eti hata wabunge ni VIP. Hivi mtu kama Zitto akitelemkia kule kwa wananchi wengine kutatokea nini?

Hivi hawa CCM, CHADEMA, TLP, CUF, wanapingana nini? Naona mambo yao yote yanafanana. Kila mmoja anajifanya ni VIP, kila mmoja kakimbilia shangingi badala ya hizo pesa kununua vitabu vya shule, kila mmoja kwenye kura ya kupandisha mishahara yao, anasema ndio.

Sisi kweli tumelala, tunacheza mdundiko wao bila kujua ulikoanzia wala utakako ishia.

Kazi kweli yaani.....tatizo la bongo ni kuwa kila mtu anataka ufalme,huyo kikwete mwenyewe kwanini asiseme kwamba hataki li-umati kuja kumpokea???wanapenda sana hayo mambo ya umungu mtu.......
 
waacheni tu kiama kimefika walipe wasilipe wembe ni ule ule wanaondoka ngoja maandamano yaanze mtaona.

ila msiwe waoga kuonyesha haya maoni yenu kwa maandamano waoga sana CCM wala msihofu.
 
jamani hata mchawi anao wachawi wenzake waache marehemu wana jikokota karamagi si naye alikuwepo?

wezi wanapokea wezi wenzao.hata huyo Lowassa mwizi nitawapa stori zake ngoja nipange mambo vema.
 
Mawaziri wote hao wameacha kazi zao, familia zao, ndugu zao, majimbo yao ili tu kwenda kumpokea Muungwana airport?

Tanzania bado tumelala sana. Hayo masaa tunayopoteza airpot si tungetumia kwenye uzalishaji? kwenye kutatua shida za watu? Kwenye kuhimiza mambo ya maendeleo?

Nashangaa kila siku watu wako VIP lounge, eti hata wabunge ni VIP. Hivi mtu kama Zitto akitelemkia kule kwa wananchi wengine kutatokea nini?

Hivi hawa CCM, CHADEMA, TLP, CUF, wanapingana nini? Naona mambo yao yote yanafanana. Kila mmoja anajifanya ni VIP, kila mmoja kakimbilia shangingi badala ya hizo pesa kununua vitabu vya shule, kila mmoja kwenye kura ya kupandisha mishahara yao, anasema ndio.

Sisi kweli tumelala, tunacheza mdundiko wao bila kujua ulikoanzia wala utakako ishia.

Mtanzania,
Ndio maana tukaitwa maskini,
maskini huwa ni mtu jeuri sana,anapenda sifa sana,haiingii akilini
viongozi wote wanahamia airport eti kumpokea rais,what a hell,hivi akienda mkuu wa mkoa peke yake kutaharibika nini?Watu weusi sijui
hii laana itaondoka lini?Jifunzeni kwa nchi za magharibi hamna upuuzi kama huu,Bush na Brown ni sawa na Tibaigana tu huku majuu.
 
sioni sababu ya kuwa kila rais akisafiri akapokewe na lukuki ya watu. .....ila hii ya safari hii ccm wamefanya kwa makusudi kuonyesha kuwa rais hajapoteza umaarufu wake kama watu wanavyopiga kelele kwa kiingereza wanasema ni image control! na hii image control sio kwa sisi watanzania, maana hatubabaishwi na tarumbeta la john komba, bali n kwa vyombo vya nje visivyojua propaganda ya tz
 
mimi naona haya mapokezi ni kama kupoteza muda vile. Time is money jamani.

kwa wenzetu mlioko majuu hivi George Bush na Gordon Brown na wenyewe hupokewa na umati wa mawaziri na wananchi kama JK?
 
Lakini Kaka Kada Embu tuwe wakweli kidogo Muungwana!Hivi kwa nini Jk anapokewa kwa makeke namna hiyo?Kuna nini kinataka kuelezwa hapa?Au safari yake hii ya Marekani imekuwa na Mafanikio kuliko alizowahi kufanya huko mwanzoni?.Au wananchi wamefurahi kwamba amerudi salama kwa sababu Medical check up huko Ufaransa iliwapa wasiwasi labda Jk ana tatizo kubwa?.Na wala sio kweli kwamba watu wapo hapa kumshambulia Muungwana!TUTAMPONGEZA atakapomuondoa Kaka Karamagi katika Cabinet!

safari zake nyingi tu Muungwana amekuwa akipokewa na watu kede kede, hii sio mara ya kwanza mheshimiwa !
 
Back
Top Bottom