NakuliliaTanzania
JF-Expert Member
- Sep 24, 2007
- 555
- 7
Mi nilidhani wangekuwa maelfu, halafu kumbe ni wanachama wa CCM..so ningedhani ingekuwa mamia ya wana CCM....au ndo kujaribu kufunika ishu?
Habari za Kitaifa
Mamia wampokea Kikwete
Mwandishi Wetu
HabariLeo; Monday,October 08, 2007 @00:04
MAMIA ya watu jana walifurika katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kumpokea Rais Jakaya Kikwete aliyerejea nchini baada ya ziara ndefu ya Marekani.
Watu hao akiwamo Waziri Mkuu Edward Lowassa, mawaziri kadhaa na wanachama wa CCM waliokuwa wamevalia mavazi ya njano na kijani walifurika uwanjani tangu saa saba mchana, wakimsubiri Rais Kikwete aliyewasili baada ya saa moja.
Umati huo wa watu ulikuwa ukiburudishwa na nyimbo maarufu za John Komba wa TOT huku wakiwa wameshika mabango ya kumkaribisha nyumbani rais.
Mengi ya mabango yalisomeka Karibu nyumbani Rais Kikwete.
Baada ya kuwasili, Rais Kikwete alitoka nje ya eneo la kupumzika wageni mashuhuri (VIP) na kwenda nje kuwasalimia wananchi hao waliokuwa wamefurika ambao nao walimshangilia kwa makofi na vigelegele kabla ya kuondoka kuelekea Ikulu kwa ajili ya mapumziko.
Ziara hiyo ya rais ya wiki tatu nchini Marekani imeelezwa kuwa na mafanikio kutokana na kuiwezesha Tanzania kupatiwa kiasi kikubwa cha fedha kuliko kilichowahi kutolewa kwa nchi yoyote chini ya Mpango wa Millennium Challenge Corporation(MCC).
Mtendaji Mkuu wa MCC, Balozi Johyn Damilovich alimueleza rais uamuzi wa bodi ya shirika hilo kuidhinisha fedha za kugharamia miradi mikubwa ya uwekezaji nchini. Fedha hizo siyo mkopo.
MCC imeidhinisha dola za Kimarekani milioni 699 (Sh bilioni 881), kiasi ambacho ni kikubwa zaidi kuliko kilichowahi kutolewa kwa nchi yoyote duniani na MCC. Miongoni mwa miradi itakayonufaika na fedha hizo ni ile ya ujenzi wa miundombinu.
Taarifa iliyotolewa na Ikulu juzi ilisema kuwa Marekani iliahidi kuendelea kuisaidia Tanzania katika maeneo mbalimbali ikiwamo eneo la kijeshi.
Katika eneo la uwekezaji kampuni kadhaa zimeonyesha nia ya kujenga viwanja vya mbolea nchini na miradi mingine. Miongoni mwa makampuni hayo ni JP Morgan, Merrill Lynch, Tegris na Gilbraltar Properties.
Wakati wa ziara yake nchini humo aliyoianza Septemba 15, Rais Kikwete alizindua matangazo ya vivutio vya utalii wa Tanzania katika televisheni ya kimataifa ya CNN huku kampuni kadhaa zikionyesha kukubali kuwekeza nchini katika sekta ya utalii ikiwamo kampuni maarufu ya mahoteli ya Global Hyatt Corporation ambayo imekubali kuja nchini kuangalia maeneo ya kujenga mahoteli.
Rais pia alizindua maandalizi ya Tanzania kuwa Mwenyekiti wa Mkutano wa 33 wa Utalii Afrika uliopangwa kufanyika Mei mwakani mjini Arusha.
http://www.dailynews-tsn.com/habarileo/page.php?id=4431
Habari za Kitaifa
Mamia wampokea Kikwete
Mwandishi Wetu
HabariLeo; Monday,October 08, 2007 @00:04
MAMIA ya watu jana walifurika katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kumpokea Rais Jakaya Kikwete aliyerejea nchini baada ya ziara ndefu ya Marekani.
Watu hao akiwamo Waziri Mkuu Edward Lowassa, mawaziri kadhaa na wanachama wa CCM waliokuwa wamevalia mavazi ya njano na kijani walifurika uwanjani tangu saa saba mchana, wakimsubiri Rais Kikwete aliyewasili baada ya saa moja.
Umati huo wa watu ulikuwa ukiburudishwa na nyimbo maarufu za John Komba wa TOT huku wakiwa wameshika mabango ya kumkaribisha nyumbani rais.
Mengi ya mabango yalisomeka Karibu nyumbani Rais Kikwete.
Baada ya kuwasili, Rais Kikwete alitoka nje ya eneo la kupumzika wageni mashuhuri (VIP) na kwenda nje kuwasalimia wananchi hao waliokuwa wamefurika ambao nao walimshangilia kwa makofi na vigelegele kabla ya kuondoka kuelekea Ikulu kwa ajili ya mapumziko.
Ziara hiyo ya rais ya wiki tatu nchini Marekani imeelezwa kuwa na mafanikio kutokana na kuiwezesha Tanzania kupatiwa kiasi kikubwa cha fedha kuliko kilichowahi kutolewa kwa nchi yoyote chini ya Mpango wa Millennium Challenge Corporation(MCC).
Mtendaji Mkuu wa MCC, Balozi Johyn Damilovich alimueleza rais uamuzi wa bodi ya shirika hilo kuidhinisha fedha za kugharamia miradi mikubwa ya uwekezaji nchini. Fedha hizo siyo mkopo.
MCC imeidhinisha dola za Kimarekani milioni 699 (Sh bilioni 881), kiasi ambacho ni kikubwa zaidi kuliko kilichowahi kutolewa kwa nchi yoyote duniani na MCC. Miongoni mwa miradi itakayonufaika na fedha hizo ni ile ya ujenzi wa miundombinu.
Taarifa iliyotolewa na Ikulu juzi ilisema kuwa Marekani iliahidi kuendelea kuisaidia Tanzania katika maeneo mbalimbali ikiwamo eneo la kijeshi.
Katika eneo la uwekezaji kampuni kadhaa zimeonyesha nia ya kujenga viwanja vya mbolea nchini na miradi mingine. Miongoni mwa makampuni hayo ni JP Morgan, Merrill Lynch, Tegris na Gilbraltar Properties.
Wakati wa ziara yake nchini humo aliyoianza Septemba 15, Rais Kikwete alizindua matangazo ya vivutio vya utalii wa Tanzania katika televisheni ya kimataifa ya CNN huku kampuni kadhaa zikionyesha kukubali kuwekeza nchini katika sekta ya utalii ikiwamo kampuni maarufu ya mahoteli ya Global Hyatt Corporation ambayo imekubali kuja nchini kuangalia maeneo ya kujenga mahoteli.
Rais pia alizindua maandalizi ya Tanzania kuwa Mwenyekiti wa Mkutano wa 33 wa Utalii Afrika uliopangwa kufanyika Mei mwakani mjini Arusha.
http://www.dailynews-tsn.com/habarileo/page.php?id=4431