Elections 2015 Mambo yenye kufikirisha juu ya Hatma ya Taifa letu TANZANIA... Nakubali kuna tatizo kwenye elimu yetu

Kwanza kabisa wewe ndio watu waliosababisha tukadharau wasomi. Hivi unaposema tuheshimu mambo yaliyofanywa na wasomi unatufanya sisi ni wajinga wa kiasi hicho. Mikataba yote hii mibovu inayotufanya kila siku tulie imeingiwa na hao watu unaowadharau wa kariakoo? Kwa hiyo wewe baadhi ya wasomi ambao huna shaka nao ni Zitto!!? Ukiona hivyo ujue kwamba hapa tulipofikia tumeona mambo mengi yakuongopea wananchi yakifanywa kwa kigezo cha usomi, zamani tulikuwa tukisikia mtu ni msomi tulikuwa tunampa mpaka akili zetu atushikie. Leo hii mashirika na taasisi nyingi zinazoendeshwa na wasomi ziko taabani kwani hakuna wasomi bali watu waliohudhuria vyuo vikuu. Baada ya sisi wananchi wa wa kawaida kuwastukia nyie mnaojifanya wasomi tumeamua kufanya kivyetu na hakika sasa tunaoana mambo yananyooka. Jaribu kuangalia shughuli nyingi zinazofanywa na watu wachapa kazi fananisha na za wasomi jinsi utakavyoona tofauti kubwa. Ama nikupe mfano mrahisi, leo msomi na asiye msomi wape biashara wafanye halafu njoo ndani ya mwaka utakuta ile ya asiye msomi ndio imefanya kwa ufanisi kuliko inayoongozwa na msomi.

Kwani nyie mnaojifanya wasomi zaidi ya kuzunguka na bahasha kwenda kuomba kazi za kuajiriwa ni kipi kikubwa mnachofanya? Sana sana mkipata kazi ndio mnaoishia kuiba hela za wananchi wavuja jasho kwa kutengeneza receipt fake ili kujipatia hela kwa njia ya uwizi. Kwa mfano wewe mwenyewe zaidi ya kujipendekeza ili upate madaraka ni mradi gani wenye tija umewahi kusimamia na ukatoa matokeo chanya? Jipime kwa dhamira yako kama kuna chochote tangible unaweza kutuonyesha zaidi ya kujipendekeza ukae ofisini.

mkuu huyu Juliana tulikua nae mbozi magharibi kwa silinde mwaka 2010,hela tuliyoandaliwa ya chakula na posho kidogo huyu dada na mwenzake mkaka alikua anasoma RUAHA walituibia........leo hapa anajifanya msomi na yeye.............km huyu ataingia bungeni basi ni kwa kigezo cha kuuza mwili na sio utendaj
 
Bavicha hamna jema..leo July amewapa kick ya Elimu kwanza bado mnamshughulikia..mmetisha.
 
Wewe UTAKUWA MBUGE KUPITIA CHAMA KIPI? WEWE NAHISI NI WALE WALE, SO MVUTA KAMBA HUVUTIA UPANDE WAKE! WEWE BORA UNGEENDA KUPEKUA HAYO MAKALABRASHA YAKO BADALA YA KUJA HUKU KUANDIKA VITU AMBAVYO HATA HAVIELEWEKI
 
Wewe UTAKUWA MBUGE KUPITIA CHAMA KIPI? WEWE NAHISI NI WALE WALE, SO MVUTA KAMBA HUVUTIA UPANDE WAKE! WEWE BORA UNGEENDA KUPEKUA HAYO MAKALABRASHA YAKO BADALA YA KUJA HUKU KUANDIKA VITU AMBAVYO HATA HAVIELEWEKI
Wewe unaishi Dunia gani...yaani Haujui Juliana yuko Chama gani..sasa tukusaidiaje..?
 
Eti ni siku ya kujisomea maktaba,.. huna hata aibuna elimu yako ya kujitungia stori za pwagu na pwaguzi!!!
 
Leo sikupanga kuandika jambo lolote sehemu yeyote kwani kwa kawaida leo ni siku yangu ya kujiongezea maarifa kwa maana ni siku yangu ya kuingia Maktaba kujisomea, lakini nimekuta mjadala unaendelea katika sehemu ambayo ninanunua magazeti kila asubuhi, kundi la watu wanajadili kuhusu TAFITI.

Kilichonifanya niandike ni muelekeo wa mjadala huo unaohusu tafiti zilizotoa matokeo yake hivi karibuni..Kila mmoja anajua TWAWEZA wametoa matokeo ya tafiti yao na kuonyesha kuwa MAGUFULI atashinda kwa asilimia 65 na LOWASSA 25%, na kisha Taasisi ya Kimataifa Synovate nayo imetoa matokeo ya tafiti yake na kuonyesha Magufuli atashinda kwa asilimia 62 na Lowassa 26%. Matokeo haya yameleta ukakasi mkubwa kwa Upinzani hasa CHADEMA maana watu kama Zitto ambao ni wapinzani wasomi na wanafanya siasa za mahesabu wamekubali..

12063814_984103881656012_2081695128803102450_n.jpg
Nimeshangazwa na Kundi la Watu ambao wanaonekana kuwa wameenda shule lakini abaa-manthura hakuna kitu kichwani ambao walikuwa wanapinga matokeo ya tafiti hizo kwa kutumia "Eti wanaouita UTAFITI wa Kkoo" na mmoja anatokwa povu anasema nina Digrii lakini sikubali matokeo ya Twaweza ila wale jamaa wa kariakoo wako sahihi kwa sababu wamefanya utafiti kwenye ground kabisa." sikutaka hata kuchangia nikanunua magazeti yangu na kuondoka eneo hilo kwa masikitiko makubwa.

Nikajiuliza hivi hawa watu wanajua maana ya Utafiti..? wanajua maana ya MTAFITI..? na ikiwa mtu mwenye digrii tena anayeishi Dar es salaam bado hajajua maana ya Utafiti na nani mtafiti, hali ya Taifa hili ikoje kwa waliokosa elimu na wanaoishi vijijini..? Sikutegemea kuwa anaweza kuwepo Mtu mwenye akili Timamu tena aliyeenda shule ambae ataamini Utafiti wa Kkoo unaosema LOWASSA atashinda kwa 98% na kupinga tena "serious" kabisa tafiti za TWAWEZA na SYNOVATE..nasikia hata kwenye baadhi ya maofisi mjadala huu uko katika sura hii pia.

Elimu yetu BADO HAIJATUKOMBOA...katika Serikali ijayo na kwa kuwa nitakuwa Bungeni, nitapeleka muswada binafsi ama nitaomba kupitia Chama Serikali ilete Muswada "Maalum" Bungeni wa kujadili ELIMU na HATMA ya Taifa, tufanye Overall reform and rebranding..bado elimu yetu inazalisha MAMBUMBUMBU kupindukia...
Kiukweli tulikuwa tunaidharau jf, lakini amini usiamini, mabandiko kama haya, yamesaidia saidia, huwezi jua!. Zamani nilikuwa napitia mabandiko yako kwa dharau na kujibu kwa kejeli, lakini baada ya uteuzi, sasa napitia mabandiko yako yote kwa makini zaidi, heshima na adabu haswa kwa kuzingatia wewe sasa ndio bosi wangu kwenye tasnia ya habari.

Karibu Boss, Mheshimiwa saba, Bi Juliana Shonza.

Paskali.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom