Mambo ya uchawi unavyofanyika katika viungo vya uzazi someni

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,314
33,108
MAMBO YA UCHAWI UNAVYOFANYIKA KATIKA VIUNGO VYA UZAZI SOMENI
Tunapozungumzia uchawi hakuna shaka kuwa ni lugha inayoeleweka katika jamii yoyote.
Hivyo hili ni tatizo linalosababishwa na sayansi ya asili kwa baadhi ya watu
wachache. Sayansi hii hutumika zaidi kwa kutumia mchanganyiko wa miti
ya shamba. Mfano: Mwanamke anaweza kulogwa ili asizae kabisa au
akapata mimba na kutoka au akapata mimba na kukaa nayo kwa muda
mrefu sana halafu asizae. Vipimo vya hospitali huonyesha sawasawa ana
mimba lakini hakuna kuzaa. Hata kwa mwanaume pia anaweza kulogwa na
maumbile yake yakasinyaa yakawa hayana uwezo wa kushiriki tendo la
ndoa tena. Hata pia sayansi hii inaweza kutumiwa na baadhi ya watu ya
kumfanya mwanamme au mwanamke asioe au kuolewa.
Kwa upande wa mwanamke anaweza kuwa anaolewa na kuachwa au
kukosa huduma katika ndoa yake au katika mapenzi. Inawezekana pia akachumbiwa na asiolewe.
Inawezekana kabisa ndoa ya mwanamke ikawepo lakini kukawa hakuna kusikilizana, Amani inatoweka muda wote, vile vile hata kwa mwanamme hali kadhalika.
NINI HUSABABISHA MPAKA MTU MUME AU MTU MKE AKALOGWA?
Mara nyingi sana hali hii hutoka kutokana na wivu au chuki baina ya mtu na mtu au na watu. Chuki hii inayo tabaka nyingi:
Kwa upande wa mwanamke anaweza kuolewa na mwanaume ambaye alivunja ndoa yake ya awali.
Mwanamke anaweza kuolewa na mme mwenye mali nyingi wengine wakaona wivu na kwanini yeye?
Mwanamke anaweza kuolewa na mwanaume mwenye mahusiano na wanawake wengine. (wake wengi/mitara).
Mwanamke anaweza kuolewa na mme mwenye elimu kubwa au mwenye fani ya mvuto kwa UMMA kwa mfano mcheza mpira, mwanamuziki maarufu, biashara kubwa, cheo kikubwa serikalini, kwenye makampuni n.k.
Pia mwanaume anaweza kulogwa kwa sababu zifuatazo
Anaweza kuoa mwanamke aliyeachana na mwanaume mwingine.
Kama ikatokea anagombaniwa na wanawake wengi.
Kama ikatokea mwanaume anabadilisha sana wanawake na kutokuwa mwaminifu.
Kama ikatokea mwanaume anashiriki mapenzi na mwanamke aliyelogwa pia yeye atakuwa na tatizo hilohilo.
DALILI ZA MWANAMKE AU MWANAUME ALIYELOGWA:
Mwanamke
Kuota ndoto za kufanya mapenzi na wanaume asiyewajua nap engine anayewajua, mfano:
Anaweza kutoa ndoto anafanya mapenzi na baba yake wa kumzaa/mzazi.
Kuota kufanya mapenzi na kaka yake.

Anaweza kuota ndoto anafanya mapenzi na mwanaume jalalani au chooni.
Anaweza kuota ndoto anafanya mapenzi kwenye dimbwi la maji.
Anaweza kuota ameolewa na kufanya mapenzi na mwanaume mwenye kipato (Tajiri) lakini mwanaume huyo anakuwa anabadilika badilika mara binadamu mara nyingine nyoka.
Anaweza wakati mwingine kutaka kufanya mapenzi lakini akikosa
mwanaume hujichuwa mwenyewe na kumaliza haja yake.
Anaweza kuota ndoto amepewa pesa nyingi lakini cha ajabu akiomba pesa
kwa mume/ndugu au jamaa zake hawampi.
Wakati mwingine huota ananyonyesha mtoto kwenye chuchu zake wakati
mwingine huota amezaa mtoto lakini mtoto huyo hubadilika badilika mara nyoka, kuku au paka.
Mwanaume
Kutaka kufanya mapenzi na mwanamke lakini uume husinyaa mara
anapomkaribia au kumwingilia mwanamke.
Kutaka kufanya mapenzi au tendo la ndoa na mwanamke na mara mawazo
ya mapenzi huyeyuka na kichwa kujaa mawazo mengine nje ya mapenzi.
 

Attachments

  • nguvu ya giza.jpg
    nguvu ya giza.jpg
    22 KB · Views: 901
Wacha Kudanganya watu wewe.
Ogopa Mungu wako. Na uwache mara moja tabia hizi za Kikafiri.
We nani kakufundisha elimu hizi za SHIRKI km sio Mkafiri?
 
Haya mambo kweli yapo na hakuna dawa Kali yenye uwezo Wa kupambana na uchawi isiyochanganywa na kiungo..na kiungo sii lazima kipatikane kwa MTU aliye hai.hapana hata kwa maiti kama Kule mochuar watu wanaenda kununua..kiukweli dunia hii INA siri kubwa
sana ikiwekwa wazi kila MTU ataogopa
 
Haya mambo kweli yapo na hakuna dawa Kali yenye uwezo Wa kupambana na uchawi isiyochanganywa na kiungo..na kiungo sii lazima kipatikane kwa MTU aliye hai.hapana hata kwa maiti kama Kule mochuar watu wanaenda kununua..kiukweli dunia hii INA siri kubwa
sana ikiwekwa wazi kila MTU ataogopa

Pamoja na hayo yote lkn uzuri ni kwamba sote ni wapitaji tu!!,hata km ungelikuwa Mchawi wa Namna gani huwezi kuishi milele.
 
Kuna vipengele vimetokea ni UKWELI. je! tiba yake nini?? au ATUBU KWA MUNGU NA KUANZA UPYA?....
Kiboko ya wachawi ni Yehova,mkabidhi Yesu maisha yako leo na hawatakuweza kwani yeye akiwa ndani yako,yeye ni mkuu kuliko wao.Tumepewa mamlaka juu ya falme za giza sema kutokujua kunamfanya mwanadamu aendelee kupata shida wakati amepewa mamlaka juu yao.

Umeumbwa kwa mfano wa Mungu.
 
Back
Top Bottom