Mambo Ya Sata

Yona F. Maro

R I P
Nov 2, 2006
4,202
218
Mwaka Jana nilikumbana na Computer moja aina ya Acer , ilikuwa ina matatizo kidogo kwahiyo nikatakiwa nirekebishe , matatizo yenyewe yalihusu Operating system , nami nilitaka kufanya repair tu .

Nikaingiza Cd yangu , na kuboot hiyo computer , nikafuata njia zote zinazotumika mwisho nikaambiwa Hard drive bado haijatambuliwa , nikaamua kuangalia setting upya katika bios na kukuta kila kitu kiko sawa , nikaenda kuload Default Settings ambazo ndio zilikwepo mwanzo .

Kwa mara ya pili nikaingiza cd yangu , kuboot na ikakataa , basi nikaamua kwenda katika tovuti ya acer , nikaangalia aina ya hii computer ndio nikaona driver moja ambayo ni maalumu kwa ajili ya SATA na ni maalumu kwa aina hizo za Acer Pekee .

Hivyo driver una download halafu unafanya exraction inaenda katika floppy disk , kisha ndio unaenda kutumia katika hivyo computer ya acer , na mimi ndio nilifanya mtindo huu huu .

Maelezo mengine ni mafupi , ni wakati una boot na cd , unabonyeza f6 ili hizo driver ziweze kuingia katika hdd yako ili iweze kutambulika na computer yako wakati unapotaka kufanya installation upya au wakati unapotaka kurepair

Sasa ni miezi imepita na juzi tu hapa nikapata computer yenye tatizo kama hilo nikatakiwa kudownload hizo driver za SATA ,nilistajabishwa kwamba katika tovuti ya sata hawajafanya mabadiliko yoyote au maendeleo yoyote katika muundo wa aina hizi za Computer , mtu unalazimika tena kutumia floppy disk kuboot na kufanya shuguli zingine .

Hii ni tofauti na unapokuwa na Dell au HP Compaq ambazo zinatambua SATA moja kwa moja na wakati unapotaka kufanya shuguli zako hauhitaji driver za ziada .

Lakini tofauti iko katika Hp Compaq zingine ambazo ni laptop , hizi kama unataka kufanya installation kuna sehemu katika Bios unatakiwa kubadilisha Enable na Disable Native Sata , sasa hivi unachagua Enable Native sata na hivyo HDD yako itatambulika .

Matatizo ya Kudisable na Enable Native sana moja ni kwamba unaweza kupoteza vitu vyako kama ukifanya kwa makosa kwa sababu inaweza kufuta partition ya HDD yako , au inaweza kuleta ukorofi mwingine .

USHAURI

Mfano computer yako imecorrupt na unataka kufanya reinstallation , au repair ni vizuri ukahifadhi data zako nje , siku hizi kuna external cases ambazo unaweza kufanya HDD na kuweza kuchukuwa data zako na kuhifadhi kisha unaweza kuifanyia HDD yako chochote unachotaka lakini umehakikisha Data zako Ziko Safi .

Kuna wakati , kuna kuwa na matatizo kadhaa , mfano hiyo computer ilikuwa ina password wakati wa kulogin na ulifanya account hiyo iwe private , maana yake ukiifunga katika external case hautaweza kuchukuwa data zako utapata ujumba mmoja ACCESS DENIED , je ufanyaje ?

Unatakiwa uifunge katika Windows 2000 au 2003 au Windows NT , usifunge katika Windows xp au 98 au millennium kwa sababu haziwezi kukupa ruhusa ya kubadilisha Permission na kufanya kitu kimoja kinaitwa Taking Ownership , lakini Windows 2000 , 03 au NT zinaweza kufanya hivi bila matatizo yoyote .

Kwahiyo kama unadata zako na umeweka pwd usihofu windows 2000 au windows 2003 ziko maalumu kwa ajili ya kutake owner ship , na hapa ndipo Microsoft walipochemsha kwa mara nyingine ukiwa na windows xp huwezi kutake ownership ya account ingine mambo kama hayo

Hizi ndio baadhi ya changamoto ambazo ziko katika SATA na windows naamini siku zinavyozidi kwenda mbele wataalamu watazidi kuboresha huduma hizi na kuzifanya ziweze kutumika kwa urahisi zaidi na watumiaji wengi zaidi
 
hivi shy kama computer imecorrupt na data hazina backup na unataka kuformat upya hiyo computer je kuna uwezekano wa kuzipata data zako from the corrupt disk?
 
hivi shy kama computer imecorrupt na data hazina backup na unataka kuformat upya hiyo computer je kuna uwezekano wa kuzipata data zako from the corrupt disk?

..shy,mbona hujamjibu jamaa?au?

..anyways,kinyau,kama ulivyouliza[je,kuna uwezekano]!ndio upo!

..ila,kazi hizo zina wataalam wake kulingana na level of corruption au damage done to the hdd!
 
shy
computer yangu inachora mstari ktk screen. mstari upo wima puande wa kushoto na unonekana nikiiwasha. je kuna fault yeyote ktk system??
 
shy
computer yangu inachora mstari ktk screen. mstari upo wima puande wa kushoto na unonekana nikiiwasha. je kuna fault yeyote ktk system??

HELLO MSANII

HIYO MISTARI HUJASEMA IKOJE

INAKATA KATA KAMA VIBOXI AU NI MSITARI UMENYOOKA MMOJA NA RANGI NYINGI NYINGI ?

1 ) KAMA NI RANGI ZENYE VIBOX MARA NYINGI NI HARDDRIVE YAKO IKO NJIANI KWENDA KUHANI

2 ) KAMA NI MSITARI ULIONYOOKA , INAWEZEKANA MONITOR YAKO NI MBOVU , HORIZONTAL CIRCULT NDIO INA MATATIZO HIYO MPAKA KUFUNGUA IANGALIWE KAMA KUNA KITU KIMELEGEA UREKEBISHWE .

AHSANTE SIKUKUU NJEMA
 
hivi shy kama computer imecorrupt na data hazina backup na unataka kuformat upya hiyo computer je kuna uwezekano wa kuzipata data zako from the corrupt disk?

Hi Kinyau

Habari zako .

Samahani kwa kuchelewa kujibu swali lako ni kutokana na majukumu ya hapa na pale ambayo yanatuzuia hata kuchungulia forums mbali mbali haswa katika suala zima na kuandika na utoaji maoni .

Kinyau kuna njia nyingi za kutoa data zako

Kama umefanya formatting kuna software za kunformat hata kama ulifanya partition kuna software za kurudisha data zako lakini hazina uhakika wa asilimia 100 wakati mwingine unaweza kufanikisha zoezi lako hilo

1 ) weka hiyo hdd yako katika external case halafu utaweza kuiaccess na kutoa data zako

2 ) kama hiyo hdd yako ilikuwa na windows xp na uliweka pwd basi funga katika mashine yenye windows 2000 au 2003 ili iweze kuover take ownership ya hizo files halafu uhamishe

3 ) njia ingine ni kufanya reinstall katika directory ingine unatakiwa urename badala ya windows weka winx na mengine kisha unaweza kuhamisha data zako

4 ) siku ingine unapokuwa na computer weka partition ili uweze kuhifadha data sehemu zingine ambazo unaweza kuhamisha kwa urahisi zaidi unapopata corrupton .

Ahsante siku zingine ukiwa na swali unaweza kuniandikia email hollymaro@gmail.com au piga simu 0784 360204 hizo ndio njia rahisi zaidi kwa sababu sio saa zote naingia forum au kushiriki forums na pia kuna sehemu nikiwepo siwezi kuingia katika forums kwa sababu za kiusalama

Karibu tena
 
Mwaka Jana nilikumbana na Computer moja aina ya Acer , ilikuwa ina matatizo kidogo kwahiyo nikatakiwa nirekebishe , matatizo yenyewe yalihusu Operating system , nami nilitaka kufanya repair tu .

Nikaingiza Cd yangu , na kuboot hiyo computer , nikafuata njia zote zinazotumika mwisho nikaambiwa Hard drive bado haijatambuliwa , nikaamua kuangalia setting upya katika bios na kukuta kila kitu kiko sawa , nikaenda kuload Default Settings ambazo ndio zilikwepo mwanzo .

Kwa mara ya pili nikaingiza cd yangu , kuboot na ikakataa , basi nikaamua kwenda katika tovuti ya acer , nikaangalia aina ya hii computer ndio nikaona driver moja ambayo ni maalumu kwa ajili ya SATA na ni maalumu kwa aina hizo za Acer Pekee .

Hivyo driver una download halafu unafanya exraction inaenda katika floppy disk , kisha ndio unaenda kutumia katika hivyo computer ya acer , na mimi ndio nilifanya mtindo huu huu .

Maelezo mengine ni mafupi , ni wakati una boot na cd , unabonyeza f6 ili hizo driver ziweze kuingia katika hdd yako ili iweze kutambulika na computer yako wakati unapotaka kufanya installation upya au wakati unapotaka kurepair

Sasa ni miezi imepita na juzi tu hapa nikapata computer yenye tatizo kama hilo nikatakiwa kudownload hizo driver za SATA ,nilistajabishwa kwamba katika tovuti ya sata hawajafanya mabadiliko yoyote au maendeleo yoyote katika muundo wa aina hizi za Computer , mtu unalazimika tena kutumia floppy disk kuboot na kufanya shuguli zingine .

Hii ni tofauti na unapokuwa na Dell au HP Compaq ambazo zinatambua SATA moja kwa moja na wakati unapotaka kufanya shuguli zako hauhitaji driver za ziada .

Lakini tofauti iko katika Hp Compaq zingine ambazo ni laptop , hizi kama unataka kufanya installation kuna sehemu katika Bios unatakiwa kubadilisha Enable na Disable Native Sata , sasa hivi unachagua Enable Native sata na hivyo HDD yako itatambulika .

Matatizo ya Kudisable na Enable Native sana moja ni kwamba unaweza kupoteza vitu vyako kama ukifanya kwa makosa kwa sababu inaweza kufuta partition ya HDD yako , au inaweza kuleta ukorofi mwingine .

USHAURI

Mfano computer yako imecorrupt na unataka kufanya reinstallation , au repair ni vizuri ukahifadhi data zako nje , siku hizi kuna external cases ambazo unaweza kufanya HDD na kuweza kuchukuwa data zako na kuhifadhi kisha unaweza kuifanyia HDD yako chochote unachotaka lakini umehakikisha Data zako Ziko Safi .

Kuna wakati , kuna kuwa na matatizo kadhaa , mfano hiyo computer ilikuwa ina password wakati wa kulogin na ulifanya account hiyo iwe private , maana yake ukiifunga katika external case hautaweza kuchukuwa data zako utapata ujumba mmoja ACCESS DENIED , je ufanyaje ?

Unatakiwa uifunge katika Windows 2000 au 2003 au Windows NT , usifunge katika Windows xp au 98 au millennium kwa sababu haziwezi kukupa ruhusa ya kubadilisha Permission na kufanya kitu kimoja kinaitwa Taking Ownership , lakini Windows 2000 , 03 au NT zinaweza kufanya hivi bila matatizo yoyote .

Kwahiyo kama unadata zako na umeweka pwd usihofu windows 2000 au windows 2003 ziko maalumu kwa ajili ya kutake owner ship , na hapa ndipo Microsoft walipochemsha kwa mara nyingine ukiwa na windows xp huwezi kutake ownership ya account ingine mambo kama hayo

Hizi ndio baadhi ya changamoto ambazo ziko katika SATA na windows naamini siku zinavyozidi kwenda mbele wataalamu watazidi kuboresha huduma hizi na kuzifanya ziweze kutumika kwa urahisi zaidi na watumiaji wengi zaidi

NITAWEZAJE KUPATA DATA ZANGU KATIKA SATA KAMA UMESEMA HAINA SLAVE ?
 
shy
computer yangu inachora mstari ktk screen. mstari upo wima puande wa kushoto na unonekana nikiiwasha. je kuna fault yeyote ktk system??

Samahani Msanii, najua umeelekeza swali kwa Shy, naomba tu kuuliza; je computer hiyo ni laptop aina ya Toshiba?!

Kuna takwimu zangu nakusanya ndiyo maana nimeuliza. Ahsante. (btw, apologies for a leading question)

SteveD.
 
Back
Top Bottom