Mapango ya Amboni
Senior Member
- Apr 12, 2013
- 104
- 108
Katika kupitia rasimu ya katiba mpya nimeona kuwa katika mambo yanayoelezwa kuwa ni ya Muungano ni "Mambo ya Nje". Wakati huo huo, katika ibara ya 62 (2) ya rasimu hiyo kunaelezwa hivi (nanukuu)
Sasa kwa mujibu wa kifungu hicho bila shaka mshirika (yani Zanzibar au Tanzania Bara kama ilivyotumika humo) anaweza kuanzisha mahusiano na jumuiya au taasisi ya kimataifa bila pingamizi mfano kujiunga na jumuiya kama COMESA au hata kuzipa bendera meli za nchi za nje (ship flagging) hasa Zanzibar ambayo nadhani bendera wanayo. Je hapa hakuna kukinzana? Yani upande unaambiwa mambo ya nje ni ya Muungano, wakati huo huo unaruhusiwa kuwa na mahusiano/ushirikiano na taasisi za kimataifa! Wajuzi mkinielewesha nitashukuru.
"(2) Bila ya kuathiri mipaka iliyowekwa na Katiba hii, kila Mshirika waMuungano atakuwa na uwezo na uhuru wa kuanzisha mahusiano auushirikiano na jumuiya au taasisi yoyote ya kikanda au kimataifa kwa mamboyaliyo chini ya mamlaka yake kwa mujibu wa Katiba ya Mshirika wa
Muungano". (mwisho wa kunukuu)Sasa kwa mujibu wa kifungu hicho bila shaka mshirika (yani Zanzibar au Tanzania Bara kama ilivyotumika humo) anaweza kuanzisha mahusiano na jumuiya au taasisi ya kimataifa bila pingamizi mfano kujiunga na jumuiya kama COMESA au hata kuzipa bendera meli za nchi za nje (ship flagging) hasa Zanzibar ambayo nadhani bendera wanayo. Je hapa hakuna kukinzana? Yani upande unaambiwa mambo ya nje ni ya Muungano, wakati huo huo unaruhusiwa kuwa na mahusiano/ushirikiano na taasisi za kimataifa! Wajuzi mkinielewesha nitashukuru.