Mambo ya kuzingatia unapovinjari kwenye Internet ili kulinda usalama wako

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,397
1579527918611.png

Wakati ukivinjari kwenye mtandao wa inteneti unapotembelea tovuti mbalimbali au #MitandaoYaijamii unapaswa kuwa mwangalifu na kutunza usalama wako dhidi ya watu wenye nia ovu: Kumbuka mambo yafuatayo ili kujihakikishia usalama wako

Usifungue kiunganishi au barua pepe kutoka kwa mtu usiyemfahamu: Wadukuzi hutumia mbinu ya kutuma links au viunganishi wanavyoviambatanisha na jumbe za kuvutia. Endapo utafungua kiunganishi hicho basi unampa uwezo mdukuzi wa kuingia mawasiliano yako

Tumia nywila au password iliyoimara na bora zaidi: Jitahidi kuifanya nywila yako kuwa siri na kuitunza kwa njia sahihi, epuka kutoa nywila yako kwa mtu yeyote. Endapo nywila yako itaingia katika mikono ya wahalifu wa mtandaoni basi taarifa na mawasiliano yako yatakuwa shakani

Tumia kivinjari(Browser) inayojali usalama wa watumiaji wake: Wataalamu wengi wa #UsalamaWaKidigitali hushauri watu kutumia vivinjari vifuatavyo, Tor Browser, Firefox, Brave, Yandex Browser, Epic, Freenet na I2P

1579527801572.png

Usikubali urafiki kutoka kwa mtu ambaye unamashaka na akaunti yake: Inashauri wa kuichunguza akaunti iliyokuomba urafiki kabla ya kukubali na kuanza kuwasiliana nayo. Ipo mifano ya watu kutumiwa meseji na kuombwa kutoa barua pepe zao kutoka kwa watu ambao si rafiki zao kwenye mtandao

Wadau naomba mchangie mengine zaidi ili kujenga uelewa mpana...
 
Je kama imetokea umewasiliana na uyo mtu ambae unamashaka na email yake utatakiwa kufanya nn?
 
Back
Top Bottom