#COVID19 Mambo ya kuzingatia unapotumia Barakoa

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Aug 7, 2018
625
938
20210226_112832_0000.png


Barakoa hufanya kazi ya kunasa matone yaliyo na virusi tunayotoa tunapoongea, kukohoa au kupiga chafya. Husaidia katika kujilinda wewe na wanaokuzunguka dhidi ya virusi

Ikiwa unaona barakoa inakukosesha amani usiache kuvaa bali badilisha aina tafuta nyingine mpaka utakapopata inayokufaa

Barakoa zinaweza kuleta unyevunyevu lakini katika hali hiyo, vaa ya kitambaa cha pamba ambayo itarahisisha kupumua kuliko polyester.

Ni kweli zinaweza kukuumiza masikio. Katika hali hiyo pata barakoa yenye kamba inayozunguka masikio iliyofunikwa kwa kitambaa laini ambacho hakitasumbua ngozi yako

20210226_114223_0000.png


Barakoa inaweza kuweka ukungu kwenye miwani kama wewe ni mvaaji wa miwani. Katika hali hiyo, vaa miwani yako ya macho juu ya barakoa ili kushikilia barakoa vizuri na miwani kutoingia ukungu
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom