Boss Man
JF-Expert Member
- Feb 10, 2022
- 458
- 991
Ndugu Watanganyika Mungu ni Mwema, sifa kwake kwa kutujalia Uhai
Ikiwa una Mpango wa kwenda nchi yeyote Ile Duniani hasa Nje ya bara la Afrika jitahidi kuijua nchi hiyo japo kwa machache mambo ya kuzingatia ukiwa huko pamoja na tamaduni zao, kufanya hivyo itakusaidia sana kuishi kwa amani na kuepuka matatizo ambayo siyo ya lazima.
Naenda kuelezea mambo ya kuzingatia na ambayo hutakiwi kufanya pindi unapokua MAREKANI. nitakuelezea baadhi ya nchi nyingine pia kwa uchache
MAREKANI
Ndugu Mtanzania ukiwa marekani peana mikono (handshake ) kama salamu ya kawaida, japokuwa hii kwangu sio lazima sana kwasababu tu ya ngozi yangu nyeusi, nikiwa Marekani Mimi Binafsi kwenye hili swala la handshake mm Nina principal zangu huwa siwi wa kwanza kutoa mkono nasubiri mwenzangu aanze lakini pia hii nai apply sana hapa Bongo, maana mswahili hakawii kusema nataka kumuibia nyota
Ukisalimiwa "How are you" take it as if they are saying “You good?” na ujibu "Good" au "Good thank" jibu hivyo hata kama unahisi kufa sekunde zijazo, Marekani salamu haimaanishi kumjulia mtu hali, ni changamsha genge tu. Sasa wewe salimiwa halafu jichanganye kwa kutoa maelezo marefu.
Pia usisahau kuonesha katabasamu kwa mbali unaposalimia au unapojibu salamu. Marekani tabasamu ni ishara ya ukarimu, ndugu Mtanganyika usije ukafika Marekani watoto wa kizungu wakawa wanakutabasamia ukazani wanakutaka na wewe ukajimix kuwatongoza, utaharibu kila kitu, chonde chonde hizo hisia ziache Bongo.
Ndugu Mtanzania ukifika Marekani usifanye mazungumzo moja kwa moja na watoto usiowajua. Watoto wa Marekani wanafundishwa tangu wakiwa wadogo kuogopa wageni, na ukianza kuzungumza na mtoto asiyekujua utamtia kiwewe mtoto wa watu, na kama kuna mtu aliye karibu atafikia hitimisho lisilo sahihi kuhusu nia yako. Ikiwa una kitu cha kumwambia mtoto, mwambie mtu mzima aliye naye.
Ndugu Mtanzania ukifika Marekani usitoe maoni ya kudhalilisha kuhusu serikali au jeshi lao. Wamarekani wanathamini uhuru wao wenyewe wa kukosoa serikali na jeshi lao, lakini hawataki kusikia wageni wakikosoa nchi yao.
Ndugu Mtanzania hii point ninayoenda kueleza ni Muhimu sana, haswa ikiwa wewe sio Mzungu: Unaposimamishwa na polisi, USITOKE NDANI YA GARI LAKO NA KUMFUATA ASKARI. Kaa ndani ya gari lako na askari anapokaribia gari lako, weka mikono yako mahali ambapo askari anaweza kuiona.
Tatizo ni kwamba katika nchi nyingine au hapa Tanzania inachukuliwa kuwa ni adabu kumfuata police pale alipo, Kwa Marekani ni kosa kubwa sana askari anaweza kuwa na wasiwasi haraka sana ukifa hivyo, na hiyo inaweza kusababisha madhara makubwa, shuka kwenye gari pale tu atakapokuamlisha
VITU VYA KUFANYA UTAKAPOSHIKWA NA POLICE MAREKANI
(1) Zima injini ya gari lako
(2) Washa taa za ndani ikiwa nje ni giza (usiku)
(3) Teremsha kioo Cha mlango wa gari lako kama kipo juu
(4) Weka mikono yako kwenye usukani ambapo afisa wa polisi anaweza kuiona kwa urahisi
(5) Ukifuatisha hayo yote hapo juu then fuata kwa upole maagizo ya polisi (isipokuwa kwa maagizo ambayo hayafai, kama vile ombi la kupekua gari bila hati au sababu inayowezekana)
Ndugu Mtanzania narudia tena, Usitoke kwenye gari hadi uamliwe kufanya hivyo. Sasa jichanganye utoke kwenye gari utafurahia show.
Vivyo hivyo, usiguse pochi yako au kitambulisho hadi uulize. Ukianza kujigusagusa Police atadhani una bastora unataka kumdhuru, kwasababu Marekani kuwa na Bastola ni kitu cha kawaida na Sheria inawaruhusu yani ni kama wewe tu kuwa na namba za NIDA.
Inatosha kwa Marekani Wacha nikupe hints fupi fupi kwa nchi tofauti tofauti
ITALY
Italy: usivae nguo za Kiitaliano.
JAPAN
Japani: Ukifurahia huduma Nzuri iwe hotelini au mahala popote pale ndani japani usijidai Mshua saana ukatoa tip (Usitoe tip) ni ishara mbaya kwao, hawatachukulia kama wewe unavyoichukulia
UTURUKI
Ndugu Mtanzania ukifika Uturuki ukipewa chai usikatae kubali na inywe kwa amani ya moyo
INDIA
Ndugu Mtanzania ukifika India na Ukiona madume mawili wameshikana mikono huku wanatembea ni sawa kwao, inakubalika kijamii, usidhani kuwa wao ni mashoga. Nyingine kwa India ni kwamba usikanyage pesa, pesa inachukuliwa kuwa toleo la mungu wa kike katika dini ya Kihindu.
Hayo ni mambo baadhi kwa nchi ya Marekani na baadhi ya nchi nyingine kwa uchache pia unaweza nitajia nchi ambayo unataka kwenda au unataka kujua vitu gani havitakiwi kufanywa huko au ni mambo gani ya kuzingatia unapokuwa katika nchi ngeni na nitakujibu nikishindwa Watanganyika wenzangu watanisaidia
Huu uzi ni wa kila mtu, kuwa huru kueleza chochote kile unachokijua ili kutusaidia sisi Watanganyika wenzako
NB: Swala la kwamba utafikaje huko hilo ni juu yako Sina msaada wowote katika jambo hilo we niambie ushafika au unatarajia kwenda kwa namna unayoijua wewe then Mimi nitakupa hits.
MUNGU NI MWEMA
Ikiwa una Mpango wa kwenda nchi yeyote Ile Duniani hasa Nje ya bara la Afrika jitahidi kuijua nchi hiyo japo kwa machache mambo ya kuzingatia ukiwa huko pamoja na tamaduni zao, kufanya hivyo itakusaidia sana kuishi kwa amani na kuepuka matatizo ambayo siyo ya lazima.
Naenda kuelezea mambo ya kuzingatia na ambayo hutakiwi kufanya pindi unapokua MAREKANI. nitakuelezea baadhi ya nchi nyingine pia kwa uchache
MAREKANI
Ndugu Mtanzania ukiwa marekani peana mikono (handshake ) kama salamu ya kawaida, japokuwa hii kwangu sio lazima sana kwasababu tu ya ngozi yangu nyeusi, nikiwa Marekani Mimi Binafsi kwenye hili swala la handshake mm Nina principal zangu huwa siwi wa kwanza kutoa mkono nasubiri mwenzangu aanze lakini pia hii nai apply sana hapa Bongo, maana mswahili hakawii kusema nataka kumuibia nyota
Ukisalimiwa "How are you" take it as if they are saying “You good?” na ujibu "Good" au "Good thank" jibu hivyo hata kama unahisi kufa sekunde zijazo, Marekani salamu haimaanishi kumjulia mtu hali, ni changamsha genge tu. Sasa wewe salimiwa halafu jichanganye kwa kutoa maelezo marefu.
Pia usisahau kuonesha katabasamu kwa mbali unaposalimia au unapojibu salamu. Marekani tabasamu ni ishara ya ukarimu, ndugu Mtanganyika usije ukafika Marekani watoto wa kizungu wakawa wanakutabasamia ukazani wanakutaka na wewe ukajimix kuwatongoza, utaharibu kila kitu, chonde chonde hizo hisia ziache Bongo.
Ndugu Mtanzania ukifika Marekani usifanye mazungumzo moja kwa moja na watoto usiowajua. Watoto wa Marekani wanafundishwa tangu wakiwa wadogo kuogopa wageni, na ukianza kuzungumza na mtoto asiyekujua utamtia kiwewe mtoto wa watu, na kama kuna mtu aliye karibu atafikia hitimisho lisilo sahihi kuhusu nia yako. Ikiwa una kitu cha kumwambia mtoto, mwambie mtu mzima aliye naye.
Ndugu Mtanzania ukifika Marekani usitoe maoni ya kudhalilisha kuhusu serikali au jeshi lao. Wamarekani wanathamini uhuru wao wenyewe wa kukosoa serikali na jeshi lao, lakini hawataki kusikia wageni wakikosoa nchi yao.
Ndugu Mtanzania hii point ninayoenda kueleza ni Muhimu sana, haswa ikiwa wewe sio Mzungu: Unaposimamishwa na polisi, USITOKE NDANI YA GARI LAKO NA KUMFUATA ASKARI. Kaa ndani ya gari lako na askari anapokaribia gari lako, weka mikono yako mahali ambapo askari anaweza kuiona.
Tatizo ni kwamba katika nchi nyingine au hapa Tanzania inachukuliwa kuwa ni adabu kumfuata police pale alipo, Kwa Marekani ni kosa kubwa sana askari anaweza kuwa na wasiwasi haraka sana ukifa hivyo, na hiyo inaweza kusababisha madhara makubwa, shuka kwenye gari pale tu atakapokuamlisha
VITU VYA KUFANYA UTAKAPOSHIKWA NA POLICE MAREKANI
(1) Zima injini ya gari lako
(2) Washa taa za ndani ikiwa nje ni giza (usiku)
(3) Teremsha kioo Cha mlango wa gari lako kama kipo juu
(4) Weka mikono yako kwenye usukani ambapo afisa wa polisi anaweza kuiona kwa urahisi
(5) Ukifuatisha hayo yote hapo juu then fuata kwa upole maagizo ya polisi (isipokuwa kwa maagizo ambayo hayafai, kama vile ombi la kupekua gari bila hati au sababu inayowezekana)
Ndugu Mtanzania narudia tena, Usitoke kwenye gari hadi uamliwe kufanya hivyo. Sasa jichanganye utoke kwenye gari utafurahia show.
Vivyo hivyo, usiguse pochi yako au kitambulisho hadi uulize. Ukianza kujigusagusa Police atadhani una bastora unataka kumdhuru, kwasababu Marekani kuwa na Bastola ni kitu cha kawaida na Sheria inawaruhusu yani ni kama wewe tu kuwa na namba za NIDA.
Inatosha kwa Marekani Wacha nikupe hints fupi fupi kwa nchi tofauti tofauti
ITALY
Italy: usivae nguo za Kiitaliano.
JAPAN
Japani: Ukifurahia huduma Nzuri iwe hotelini au mahala popote pale ndani japani usijidai Mshua saana ukatoa tip (Usitoe tip) ni ishara mbaya kwao, hawatachukulia kama wewe unavyoichukulia
UTURUKI
Ndugu Mtanzania ukifika Uturuki ukipewa chai usikatae kubali na inywe kwa amani ya moyo
INDIA
Ndugu Mtanzania ukifika India na Ukiona madume mawili wameshikana mikono huku wanatembea ni sawa kwao, inakubalika kijamii, usidhani kuwa wao ni mashoga. Nyingine kwa India ni kwamba usikanyage pesa, pesa inachukuliwa kuwa toleo la mungu wa kike katika dini ya Kihindu.
Hayo ni mambo baadhi kwa nchi ya Marekani na baadhi ya nchi nyingine kwa uchache pia unaweza nitajia nchi ambayo unataka kwenda au unataka kujua vitu gani havitakiwi kufanywa huko au ni mambo gani ya kuzingatia unapokuwa katika nchi ngeni na nitakujibu nikishindwa Watanganyika wenzangu watanisaidia
Huu uzi ni wa kila mtu, kuwa huru kueleza chochote kile unachokijua ili kutusaidia sisi Watanganyika wenzako
NB: Swala la kwamba utafikaje huko hilo ni juu yako Sina msaada wowote katika jambo hilo we niambie ushafika au unatarajia kwenda kwa namna unayoijua wewe then Mimi nitakupa hits.
MUNGU NI MWEMA