Uchaguzi 2020 Mambo ya kuzingatia ili usipate usumbufu siku ya kupiga kura

Status
Not open for further replies.

JamiiTalks

JF Advocacy Team
Aug 7, 2018
625
938
photo_2020-10-07_16-49-12.jpg


Ibara ya 5 (1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imempa haki kila raia aliyetimiza umri wa miaka kumi na minane kupiga kura.Kwa mujibu wa vifungu vya 13(1), 13 (2), 35C, 61 (3)(a) na 63(1) vya Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343 pamoja na kifungu cha 38 (1) cha Sheria ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa (Madiwani), Sura ya 292,Ili mtu aweze kupiga kura anatakiwa kuwa na sifa zifuatazo:-

(i) Awe amejiandikisha katika Daftari la kudumu la wapiga kura:

(ii) Awe ana Kadi ya Mpiga Kura iliyotolewa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi;

(iii) Awe katika kituo alichojiandikisha kupiga kura

Sheria ya Taifa ya uchaguzi inamruhusu mtu kupiga kura kwa kufuata utaratibu ufautao:

(i) Mpiga Kura anatakiwa kwenda kwenye kituo cha kupigia kura alichojiandikisha akiwa na kadi yake ya kupigia kura.

(ii) Mpiga kura anatakiwa kupanga mstari akiwa kituo cha kupigia kura na kusubiri hadi zamu yake ya kupiga kura itakapowadia.

(iii) Mpiga kura anatakiwa afuate maelekezo yote atakayopewa na msimamizi wa kituo muda wote akiwa kituoni.

(iv) Baada ya kumaliza kupiga kura, mpiga kura anatakiwa kurudi nyumbani.
 
Kumbe ile ya kupakwa wino ukimaliza kupiga kura haipooo kesho hawanipaki
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom