Mambo ya ajabu ayafanyayo mwanadamu

Fredinho

JF-Expert Member
May 18, 2016
969
1,137
1. Unanunua ndizi mbivu halafu unaosha vizuri ganda la nje kisha unalitupa unakula kipande cha ndani,uliosha ganda kwanini?

2. Unanawa mikono vizuri kwa maji ya uvuguvugu kisha unajifuta kwa tissue halafu unakula wali maharage kwa kijiko mwanzo mwisho,ulinawa ili iweje?

3. Unatongoza mwanamke miezi mitatu akikukubalia unafanya nae ngono ukiwa umevaa kondomu kwa nini? kama ulijua huyo mwanamke ni hatari kwa afya yako mpaka anahitaji kinga kwa nini ulipoteza muda wako kumtongoza?

4. Unapelekwa shule kusoma hutaki, utoro mwanzo mwisho,adabu hakuna, kujisomea hujisomei, matokeo ya NECTA yakitoka una ziro unahuzunika, unahuzunikia nini? kwani hukujua utafeli?

5. Unampa mimba binti wa watu akikuambia ana mimba yako, unamuuliza iliingiaje-hebu kuwa siriasi bwana!!!!

Ongezea ya kwako mdau.
 
Unategemea mambo mazur kwenye nchi ambayo Magu ndio rais...... BILA SHAKA KWA HIYO KICHWA YAKO HAIKO BRAIN!!!!
 
tantariiii tantariii too much
umemaliza mshahara wote halafu tar 60 bado mbali sana tantarii what d u expect
 
Hautaki kusuuza kikombe kwa maji ya bafuni ukiamini ni uchafu wakati maji hayo hayo unatumia kupigia mswaki.

Una nawa bila sabuni unapotaka kula halafu unakuja kunawa na sabuni baada ya kula kwani ulikuwa unakula mavi?

Unamkiss mwenzio(kumla denda) lakini akikutolea mate yake na kukuwekea kwenye kiganja chake na kusema uyameze unaona kinyaa.

Anakata mti anatengeneza karatasi halafu juu ya karatasi anaandika "usikate mti"
 
Hautaki kusuuza kikombe kwa maji ya bafuni ukiamini ni uchafu wakati maji hayo hayo unatumia kupigia mswaki.

Una nawa bila sabuni unapotaka kula halafu unakuja kunawa na sabuni baada ya kula kwani ulikuwa unakula mavi?

Unamkiss mwenzio(kumla denda) lakini akikutolea mate yake na kukuwekea kwenye kiganja chake na kusema uyameze unaona kinyaa.

Anakata mti anatengeneza karatasi halafu juu ya karatasi anaandika "usikate mti"
Nimeipenda mkuu
 

Similar Discussions

9 Reactions
Reply
Back
Top Bottom