Mambo unayohitaji kujua katika ndoto unazoota sehemu ya sita(jambo la 6) by Christopher Mwakasege

Principal Focus

JF-Expert Member
Jan 4, 2013
925
548
Bwana Yesu asifiwe sana sana!
Leo nataka nikushirikishe jambo la 6 kati ya “Mambo unayohitaji kuyajua kuhusu ndoto unazoota ili iwe vyepesi kufanikiwa kimaisha”.
Jambo hilo la 6 ni hili: “Ng’oa kilichopandikizwa na shetani ndani yako kwa njia ya ndoto, na kuondoa madhara yake!”
Ndoto ambazo chanzo chake ni shetani, huwa zina tabia ya “kupandikiza” mambo mabaya kwenye maisha ya mtu aliyeoteshwa ndoto hizo!
Ukisoma kitabu cha Ayubu 4:12 – 16, utaona ya kuwa, Elifazi aliota ndoto iliyopandikiza vitu vifuatavyo kwenye maisha yake:
• Mawazo yake yalipokea neno ambalo kabla ya kuota ndoto ile halikuwemo mawazoni mwake;
• Alisikia “Sauti” kwenye masikio yake;
• Hofu “ilimwangukia” katika mwili wake;
• Mifupa yake ilianza kutetemeka
Ukiyaangalia maandiko hayo kwa mtazamo huu, utajua ya kuwa ndoto ile “ilipandikiza” katika maisha ya Elifazi vitu visivyopungua vinne!
Na vitu hivyo vinne vilimsumbua Elifazi na kwa sababu hiyo angetamani viondoke katika maisha yake, kama angekuwa anajua la kufanya ili kuving’oa!
Ningekuwa katika mazingira ya kumwombea Elifazi juu ya kilichomtokea baada ya kuota ndoto aliyoota – ningemwombea mambo yafuatayo:
(i) Toba kwa kile kilichosababisha “lango” lake la ndoto kufunguka na kupitisha ndoto na vile vilivyobebwa na ndoto ile.
Toba hii ni muhimu ili kwa kupitia msamaha wa Mungu, shetani apoteze uhalali wa kuendelea kumshambulia Elifazi kwa kutumia “lango” lake la ndoto
Na pia toba hiyo inatengeneza “uhalali” katika ulimwengu wa roho, wa Mungu kumsaidia Elifazi apate kushinda “vita” iliyopitia kwenye “ndoto” aliyoota!
(ii) Kung’oa “neno” lisilokuwa la Ki – Mungu lililoingia kwenye mawazo yake kwa kupitia kwenye ndoto aliyoota;
(iii) Kunyamazisha kwa kutumia Damu ya Yesu – “sauti” za kigeni ambazo Elifazi anazisikia “ndani yake” tangu alipoota ndoto ile;
(iv) Kukemea roho ya hofu iliyomwangukia ili iondoke katika maisha yake;
(v) Kumuombea uponyaji wa mifupa yake ili iache kutetemeka, au ili mifupa yake ipone “ugonjwa” wa kutetemeka alioupata tangu siku ile aliyoota ile ndoto!
(vi) Kuziba kwa Damu ya Yesu “lango” lake la ndoto, ili asiote tena ndoto zenye kumletea mashambulizi ya kipepo katika maisha yake!
Ufahamu huu umenisaidia kuwaombea watu wengi ambao walipata mashambulizi ya shetani kwa kupitia kwenye ndoto walizoota.
Kwa – mfano niliwahi kukutana na dada mmoja akitokea hospitali huku mguu wake mmoja akitembea kwa kuchechemea
Nilipomuuliza chanzo cha kuchechemea kwake, akanijibu ya kuwa ilikuwa ni matokeo ya ndoto aliyoota usiku
Ndoto aliyoota alimhusisha yeye akicheza mpira na wenzake, na alipoupiga mpira yeye, mguu wake ukaanza kuuma kwenye ndoto hiyo! Na baada ya hapo akaamka toka usingizini!
Na hata baada ya kuamka toka usingizini akaona mguu alioumia kwenye ndoto akicheza mpira, unaendelea kuuma. Na alipojaribu kutembea alijikuta akichechemea kwa sababu ya maumivu aliyokuwa – nayo kwenye mguu wake, ulioumia alipoupiga mpira kwenye ndoto aliyoota.
Nikamwombea pale pale njiani tulipokutana naye – na maumivu ya mguu yakapona wakati ule ule, na akaweza kuondoka pale huku akitembea bila kuchechemea!
Mfano mwingine ni huu: Mama mmoja aliniandikia kwa ujumbe wa simu ya kuwa aliwahi kuota ndoto ambayo ndani yake nyoka alimuuma yeye kwenye kidole alichokuwa na pete ya ndoa.
Na tangu wakati ule alioota hiyo ndoto, alijikuta akimchukia na kumkinai mume wake.
Lakini alipokuwa anasikiliza kwa njia ya redio mafundisho ya ndoto niliyokuwa nafundisha, na kushiriki maombi ya kung’oa kilichopandwa na shetani kwa njia ya ndoto, alijikuta akitapika povu jeupe!
Na baada ya maombi hayo, hali ya kumchukia na kumkinai mume wake iliisha, na badala yake, hali ya kumpenda ilirudi ndani yake kwa upya!
Je, kuna ndoto uliyoota unayoona ya kuwa “imepandikiza” kitu kibaya kwenye mawazo yako, au katika mwili wako, au katika nafsi yako, au katika roho yako, au katika maisha yako?
Pitia kwa upya hatua za kimaombi, nilizoziweka katika somo la leo, nilipokuwa natoa mfano wa kumwombea Elifazi wa Ayubu 4:12 – 16.
Hatua hizi zitakupa mwongozo wa kujiombea na wa kuwaombea wengine waliopata matatizo kwa njia ya ndoto.
Mungu akubariki sana!
 
Aminaa..
Bwana Yesu asifiwe sana sana!
Leo nataka nikushirikishe jambo la 6 kati ya “Mambo unayohitaji kuyajua kuhusu ndoto unazoota ili iwe vyepesi kufanikiwa kimaisha”.
Jambo hilo la 6 ni hili: “Ng’oa kilichopandikizwa na shetani ndani yako kwa njia ya ndoto, na kuondoa madhara yake!”
Ndoto ambazo chanzo chake ni shetani, huwa zina tabia ya “kupandikiza” mambo mabaya kwenye maisha ya mtu aliyeoteshwa ndoto hizo!
Ukisoma kitabu cha Ayubu 4:12 – 16, utaona ya kuwa, Elifazi aliota ndoto iliyopandikiza vitu vifuatavyo kwenye maisha yake:
• Mawazo yake yalipokea neno ambalo kabla ya kuota ndoto ile halikuwemo mawazoni mwake;
• Alisikia “Sauti” kwenye masikio yake;
• Hofu “ilimwangukia” katika mwili wake;
• Mifupa yake ilianza kutetemeka
Ukiyaangalia maandiko hayo kwa mtazamo huu, utajua ya kuwa ndoto ile “ilipandikiza” katika maisha ya Elifazi vitu visivyopungua vinne!
Na vitu hivyo vinne vilimsumbua Elifazi na kwa sababu hiyo angetamani viondoke katika maisha yake, kama angekuwa anajua la kufanya ili kuving’oa!
Ningekuwa katika mazingira ya kumwombea Elifazi juu ya kilichomtokea baada ya kuota ndoto aliyoota – ningemwombea mambo yafuatayo:
(i) Toba kwa kile kilichosababisha “lango” lake la ndoto kufunguka na kupitisha ndoto na vile vilivyobebwa na ndoto ile.
Toba hii ni muhimu ili kwa kupitia msamaha wa Mungu, shetani apoteze uhalali wa kuendelea kumshambulia Elifazi kwa kutumia “lango” lake la ndoto
Na pia toba hiyo inatengeneza “uhalali” katika ulimwengu wa roho, wa Mungu kumsaidia Elifazi apate kushinda “vita” iliyopitia kwenye “ndoto” aliyoota!
(ii) Kung’oa “neno” lisilokuwa la Ki – Mungu lililoingia kwenye mawazo yake kwa kupitia kwenye ndoto aliyoota;
(iii) Kunyamazisha kwa kutumia Damu ya Yesu – “sauti” za kigeni ambazo Elifazi anazisikia “ndani yake” tangu alipoota ndoto ile;
(iv) Kukemea roho ya hofu iliyomwangukia ili iondoke katika maisha yake;
(v) Kumuombea uponyaji wa mifupa yake ili iache kutetemeka, au ili mifupa yake ipone “ugonjwa” wa kutetemeka alioupata tangu siku ile aliyoota ile ndoto!
(vi) Kuziba kwa Damu ya Yesu “lango” lake la ndoto, ili asiote tena ndoto zenye kumletea mashambulizi ya kipepo katika maisha yake!
Ufahamu huu umenisaidia kuwaombea watu wengi ambao walipata mashambulizi ya shetani kwa kupitia kwenye ndoto walizoota.
Kwa – mfano niliwahi kukutana na dada mmoja akitokea hospitali huku mguu wake mmoja akitembea kwa kuchechemea
Nilipomuuliza chanzo cha kuchechemea kwake, akanijibu ya kuwa ilikuwa ni matokeo ya ndoto aliyoota usiku
Ndoto aliyoota alimhusisha yeye akicheza mpira na wenzake, na alipoupiga mpira yeye, mguu wake ukaanza kuuma kwenye ndoto hiyo! Na baada ya hapo akaamka toka usingizini!
Na hata baada ya kuamka toka usingizini akaona mguu alioumia kwenye ndoto akicheza mpira, unaendelea kuuma. Na alipojaribu kutembea alijikuta akichechemea kwa sababu ya maumivu aliyokuwa – nayo kwenye mguu wake, ulioumia alipoupiga mpira kwenye ndoto aliyoota.
Nikamwombea pale pale njiani tulipokutana naye – na maumivu ya mguu yakapona wakati ule ule, na akaweza kuondoka pale huku akitembea bila kuchechemea!
Mfano mwingine ni huu: Mama mmoja aliniandikia kwa ujumbe wa simu ya kuwa aliwahi kuota ndoto ambayo ndani yake nyoka alimuuma yeye kwenye kidole alichokuwa na pete ya ndoa.
Na tangu wakati ule alioota hiyo ndoto, alijikuta akimchukia na kumkinai mume wake.
Lakini alipokuwa anasikiliza kwa njia ya redio mafundisho ya ndoto niliyokuwa nafundisha, na kushiriki maombi ya kung’oa kilichopandwa na shetani kwa njia ya ndoto, alijikuta akitapika povu jeupe!
Na baada ya maombi hayo, hali ya kumchukia na kumkinai mume wake iliisha, na badala yake, hali ya kumpenda ilirudi ndani yake kwa upya!
Je, kuna ndoto uliyoota unayoona ya kuwa “imepandikiza” kitu kibaya kwenye mawazo yako, au katika mwili wako, au katika nafsi yako, au katika roho yako, au katika maisha yako?
Pitia kwa upya hatua za kimaombi, nilizoziweka katika somo la leo, nilipokuwa natoa mfano wa kumwombea Elifazi wa Ayubu 4:12 – 16.
Hatua hizi zitakupa mwongozo wa kujiombea na wa kuwaombea wengine waliopata matatizo kwa njia ya ndoto.
Mungu akubariki sana!

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom