Mambo niliyojifunza kwenye janga la Corona

Lord denning

JF-Expert Member
Jun 3, 2015
13,226
26,048
1. Nikiwa kiongozi wa nchi hii nitajikita sana kujenga sekta binafsi imara. Nitawawekea mazingira mazuri ya kukua na kustawi maana hawa hawajinufaishi peke yao. Kwa walivyojitoa kutoa mapesa kedekede ni dhahiri kuwa hawa ndo engine ya Taifa wakati wa amani na wakati wa vita. Sitaruhusu vyovyote sekta binafsi kubughudhiwa

2. Nitawaheshimu na kuwalinda wafanyabiashara wakubwa na wawekezaji/ Matajiri. Kwa jinsi Rostam alivyotoa misaada amedhihirisha kuwa ni muhimu kuwalinda na kuwathamini wafanyabiashara wakubwa na wawekezaji/ Matajiri. Dunia nzima umeona ni kwa jinsi gani watu hawa wamesaidia masikini na serikali zao kwenye janga hili.

3. Nitahakikisha tunaweka hifadhi kubwa ya Chakula kuwezesha kuwahudumia watu Milioni 20 kwa kipindi cha miezi kuanzia 10 mpaka 12. Ni dhahiri hatukuweka akiba cha chakula na Ndo mana hata tumeshindwa kuweka Lockdown kwenye kipindi hiki.

4.Uhusiano wa kimataifa ndo nguzo kuu kwenye maendeleo ya nchi na watu. Ukiwa kiongozi hakikisha unadumisha na kutengeneza sana mahusiano ya kimataifa maana wakati wa shida ni lazima utahitaji msaada.

5. Huduma ya afya ni jambo kuu kwenye Taifa. Ni bora kuweka huduma bora za vifaa mahospitalini kuliko kuanza kujenga mareli. Watu wanahitaji sana huduma bora za afya kuliko reli na ndege.

6. Kwenye kupanga matumizi lazima bajeti ya dharula iwe ina fedha za kutosha na ni kwa muda wote.

Asanteni
 
Tatizo la Tanzania vilaza ndio wanaongoza nchi na watu makini wapo mtaani hawana maamuzi.
 
Wengine mwaka 2015 tulidhani tunaleta suluhisho bora la Ustawi wa Watanzania kumbe ndiyo tulikuwa tunakaribisha Matatizo.
 
1. Nikiwa kiongozi wa nchi hii nitajikita sana kujenga sekta binafsi imara. Nitawawekea mazingira mazuri ya kukua na kustawi maana hawa hawajinufaishi peke yao. Kwa walivyojitoa kutoa mapesa kedekede ni dhahiri kuwa hawa ndo engine ya Taifa wakati wa amani na wakati wa vita. Sitaruhusu vyovyote sekta binafsi kubughudhiwa

2. Nitawaheshimu na kuwalinda wafanyabiashara wakubwa na wawekezaji/ Matajiri. Kwa jinsi Rostam alivyotoa misaada amedhihirisha kuwa ni muhimu kuwalinda na kuwathamini wafanyabiashara wakubwa na wawekezaji/ Matajiri. Dunia nzima umeona ni kwa jinsi gani watu hawa wamesaidia masikini na serikali zao kwenye janga hili.

3. Nitahakikisha tunaweka hifadhi kubwa ya Chakula kuwezesha kuwahudumia watu Milioni 20 kwa kipindi cha miezi kuanzia 10 mpaka 12. Ni dhahiri hatukuweka akiba cha chakula na Ndo mana hata tumeshindwa kuweka Lockdown kwenye kipindi hiki.

4.Uhusiano wa kimataifa ndo nguzo kuu kwenye maendeleo ya nchi na watu. Ukiwa kiongozi hakikisha unadumisha na kutengeneza sana mahusiano ya kimataifa maana wakati wa shida ni lazima utahitaji msaada.

5. Huduma ya afya ni jambo kuu kwenye Taifa. Ni bora kuweka huduma bora za vifaa mahospitalini kuliko kuanza kujenga mareli. Watu wanahitaji sana huduma bora za afya kuliko reli na ndege.

6. Kwenye kupanga matumizi lazima bajeti ya dharula iwe ina fedha za kutosha na ni kwa muda wote.

Asanteni
Hapo namba 6 . Pesa hiyo inatumika vibaya ktk nchi hii, au labda hawapewi kabisa .
Tetemeko la Kagera haikusaidia kumweka Mzee sawa. Na sasa Covid 19 ndiyo kabisa. Sijui tiss inashauri nini juu ya jambo hilo ?!.

Odhis *
 
Hapo namba 6 . Pesa hiyo inatumika vibaya ktk nchi hii, au labda hawapewi kabisa .
Tetemeko la Kagera haikusaidia kumweka Mzee sawa. Na sasa Covid 19 ndiyo kabisa. Sijui tiss inashauri nini juu ya jambo hilo ?!.

Odhis *
Hali si Hali. Kuanzia sehemu zilizokumbwa na mafuriko hadi kwenye korona. Hatuoni fedha wala bajeti ya dharula ikifanya kazi
 
TANGU 2016 JAMAA HAJANUNUA CHAKULA KUWEKA KWENYE KIHENGE CHA TAIFA,MAHINDI YALIPOPANDA AKAJIDAI NI SOKO HURIA WAKULIMA WAFAIDIKE KUMBE STOCK IKO KWA WAFANYABIASHARA,KACHEZEA AKIBA YA JK MENGINE KAPELEKA MSAADA MALAWI NA MSUMBIJI KWENYE MAFURIKO NYINGINE KAUZA ZIMBABWE MARA BOOM COVID 19 HII HAPA,HATA AKIBA YA CHAKULA HAMNA YAANI VIPAUMBELE VYAKE VINASHANGAZA SANA
Hili limeniuma sana. Kama Taifa lazima tuwe na akiba ya kulia ga at least half of our population kwa kipindi kisichopungua miezi 10 wakati wote.
 
nitawawezesha watu kiuchumi ili waweze kujiwekea akiba kwa kuboresha mazingira ya biashara na kutoa ajira rasmi...kamwe sitathubutu kufanya watu waishi kama mashetani.... Tumeshindwa kujilockdown kwasababu watu wako hoi tangu 2015

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom