Mambo muhimu ya chadema kujifunza kwa haraka

charityboy

Senior Member
Nov 11, 2010
138
4
Ushauri wa bure kwa CDM:

-Zitto ni world player, wamuheshimu tena wamuombe radhi.
-Wawe makini na MBOWE, huenda akawa shushushu (pandikizi la serikali)
-Wabunge wake wasitafute sifa kwenye magazeti, duniani hakuna mbunge anayetoa pesa yake ya mshahara. Mnyika anaandaa mazingira ya ufisadi. Inabidi CDM imkanye haraka sana.
-CDM Hatuna uwezo wa kuendesha upinzani bungeni peke yetu. Ni lazima kuwashirikisha CUF, NCCR, TLP, UDP. Vinginevyo waTZ hawatatuelewa.
-Halafu ukweli ni kwamba CCM ilitushinda kwa halali, tusitumie hoja ya kuchakachua kutafuta support ya nchi za magharibi. Wazungu sio wajinga kiasi hicho. CDM ijipange ifanye kazi. KIKWETE alishinda.
-UDINI pia utatumaliza kama hatutakuwa stable kama CUF. CUF wameonyesha ukomavu wa hali ya juu sana. Ni muhimu kwa CDM kujifunza na kutafuta uzoefu kwa wakongwe kama MAALIM SEIF, Prof Lipumba, HAMAD RASHID na A.L MREMA.


Mimi ni mtetezi wa wanyonge (charityboy)
 
SLAA(PhD) ya ukweli kiongozi wa nguvu ya umma sio wa katiba amekuwa wazi na amekuwa akiweka sawa msimamo wake, chadema na watanzania kabla ya kutangaza matokeo, wakati matokeo ya kidikiteta yakitangazwa na baada ya kuapishana kidikiteta. Asiyetaka kuelewa ni mnafiki na mgonjwa. Dr Slaa anafahamu sheria alikuwa na choice tatu muhim za kuchukua kujitangazia ushindi kama alivyofanya Quattara, au kuamuru nguvu ya umma idai haki au kutumia ustarabu na majadiliano kuweka sawa na kuondoa serikali za kidhalimu ambalo ndilo amelichukua -sasa asiyetaka kuelewa ana lake jambo. Kimsingi Dr.Slaaa na Chadema wanalengo kubadili mfumo huu wa kidikiteta na kinyonyaji hawana fitina na mtu wana fitina na mfumo na wale wanaokumbatia mfumo huo. KWAHIYO KWA GREAT THINKER YOYOTE ATAELEWA NINI CHADEMA WANAFANYA, KWA KATIBA YA SASA INARUHUSU UZANDIKI WOTE ULIOTOKEA NDIO MAANA TUNASEMA KATIBA MPYA NDIO KILIO CHA GREAT THINKERS. THIS IS NOT FOR CHADEMA IT IS FOR TANZANIA OR TANGANYIKA
 
Back
Top Bottom