Mambo muhimu ambayo mwanamke anapaswa ayajue!

Red Scorpion

JF-Expert Member
Feb 1, 2012
5,736
4,252
*MAMBO MUHIMU KUHUSU WANAUME AMBAYO MWANAMKE AKIYAJUA HATAPATA UGONJWA WA MOYO....*

KUTOKA MTANDAONI

1.. Wanaume wengi hawawezi kufanya mapenzi na mwanamke mmoja tu maishani mwao.

2..Wanaume wameumbwa na matamanio tofauti. Wapo wanaoweza kukaa miaka miwili bila ngono na wapo wasioweza kupitisha siku mbili bila kuchovya.

3..Mwanaume aliyezama kwenye penzi na mwanamke...anaweza kuwa na uhusiano na mwanamke mwingine lakini bado akawa anampenda mpenzi wake sana.

4..Waume wazuri huwa wanakuwa na mpango wa kando (nyumba ndogo)... Hizi huwasaidia kuondoa tension za ngono na kutatua migogoro ya kimapenzi hususani katika umri wa kati....

5..Kama mume wako ana uhusiano wa kimapenzi na kabinti kazuri, karembo chini ya miaka 20 USIOGOPE ila kama mume wako anapiga simu au kutumiana sms na mwanamke mwingine usiku wa manane na kuongea muda mrefu OGOPA SANA.

6..Kabla hujachagua mwanaume hakikisha anaamini kuna UKIMWI, magonjwa ya zinaa na ngono salama....kwa namna hii utakuwa na hakika hawezi kukuletea magonjwa nyumbani.

7.. Waume wengi waaminifu ndio hupiga wake zao.....hawa huwa hawana visaidizi vya ndoa...

8..Niamini. Wanaume wenye upendo wa ziada kwa wake zao huwa wana mpenzi wa ziada..... Wapenzi wa ziada ndio huwapatia utaalamu wa kuwafanya wake zao wafurahi.

9.. Mpenzi wa mume wako hana shida na nyumba yako....ameshaona picha zako na watoto wako kupitia simu ya mumeo.
Wao wana mahusiano ya kimapenzi tu baina yao kwa lengo la kusaidiana kufurahia maisha yao.

10. Wewe kama mwanamke unaweza kumuwekea mtego mumeo na kweli UTAMKAMATA....... Halafu ukishamkamata?

11. Muhukumu mume wako kwa jinsi anavyotimiza majukumu yake kwako na kwa watoto wenu na SIYO kumuhukumu anatembea na nani.......
 
nimeipenda aiseee asante kwa mada nzuri na tamu kama hii sema mimi shida yangu nimezaa na mdada mmoja wa chuo nilichosoma ila ninamichepuko hatari yaani mkoani kwetu ipo kama 8 na hapa nilipo ipo kama mitatu hivii siwezi kuiacha na inanifariji sana sana
 
Back
Top Bottom