Mambo matatu (3) ya kuzingatia kabla na wakati wa kumiliki nyumba au kiwanja cha kwanza kwa ajili ya kujenga utajiri

Aliko Musa

Senior Member
Aug 25, 2018
156
240
Kama ulinunua kwa makosa ardhi au nyumba zako, unahitaji kusoma makala hii. Kama una mpango wa kununua ardhi au nyumba, unahitaji kusoma makala hii.

Kama hujui ni nini hasa cha kuandaa kabla ya kununua ardhi au nyumba, unahitaji kusoma makala hii. Kama una nyumba yoyote ya kukuingizia kipato, unahitaji kusoma makala hii.

Kama una kiwanja au shamba, unahitaji kusoma makala hii. Kama una nyumba iliyokamilika na hakuingizii kipato endelevu, unahitaji kusoma makala hii.

Lakini nitaongelea zaidi kwa yule anayeanza kuwekeza katika ardhi na nyumba.

Karibu sana tujifunze mambo matatu (03) muhimu sana ya kuzingatia ili ununue nyumba au kipande cha ardhi:

Moja.

Usichukue Mkopo.

Huu ni ujumbe wa pekee kwako rafiki yangu. Hata kama una kila sababu ya kuona kwamba mkopo unaweza kukunufaisha. Kama ndio unaanza kuwekeza usichukue mkopo. Mazingira yatabadilika na kuifanya njia yako kuwa ndefu mno.

Kanuni niliipata kutoka kwa mwanauchumi G.Timothy Haight inasema kuwa "tawanya utajiri wako katika mlinganyo wa theluthi, theluthi moja weka kwenye ardhi na majengo, theluthi nyingine iweke kwenye biashara utakazokuwa na udhibiti ya moja kwa moja na theluthi ya mwisho iweke kwenye hisa na mitaji".

Kutoka na mlinganyo huu unatakiwa kuchukua jumla ya mkopo wa 30% ya utajiri wako wote. Kanuni hii unaweza kuisoma zaidi kwenye kitabu chake kiitwacho The Real Estate Investment Handbook (Kijtabu cha uwekezaji kwenye ardhi na majengo).

Kwa kanuni hii, asilimia 30 ya fedha zangu zote ninawekeza katika ardhi na majengo. Asilimia 30 ya fedha zangu zote ninapanga kuchukua mkopo. Asilimia 30 ya fedha zangu zote nawekeza katika aseti za nyingine.

Asilimia 10 ya pesa yote ina baki benki kwa ajili ya kushughulikia dharura za biashara zote. Huu mlinganyo wa 30%, 30%, 30% na 10% umeandaliwa na mimi mwenyewe kama maboresho ya kanuni ya Bwana G.Timothy Haight.

Sasa unahitaji mfumo kabla haujaanza kuwekeza katika ardhi na nyumba. Mfano, una tumia mfano wa mgawanyo wa hapo juu. Wewe ndio unaanza hivyo kwenye mkopo utakuwa na kiasi sifuri kabisa. Huhitaji kuchukua mkopo rafiki.

Sababu nyingine ya kutochukua mkopo pale unapoanza kuwekeza katika ardhi na nyumba ni kuwa unapokopa unaongeza kiwango cha kipato kitachokuwa kinaingia kila wiki au mwezi.

Pia mkopo huongeza hatari za kupoteza mtaji fedha hata ambao umetoka au kwa wanahisa wa kampuni lako. Sasa chagua uongeze hatari ya kuanguka au usubiri mfumo ambao utakuwezehsa kupiga hatua kubwa japo kwa kuwa subira.

Mbili.

Tathmini Gharama Za Uendeshaji.

Gharama za ukarabati wa nyumba unayotegemea kumiliki. Gharama ya kodi ya pango la ardhi au kodi ya majengo. Gharama ya usafiri yako wewe mwenyewe.

Gharama za kutafuta wapangaji. Gharama za matangazo ya kuuza au kununua ardhi utakayonunua kama utaiuza baada ya muda mfupi.

Gharama za chakula chako wewe mwenyewe. Hakikisha unatumia nguvu zako sana kuliko kutumia pesa nyingi kwa mambo ambayo unaweza kufanya wewe mwenyewe.

Kwa dunia ya sasa ni rahisi sana kupata mtaji kama utatumia nguvu na ukawa na subira. Hii ni kwa sababu ya teknolojia na maendeleo tuliyonayo ya kuwafikia watu wengi kwa muda mfupi kuliko miaka 200 iliyopita.

Usikubali kuajiri mtaalamu labda kama kitendo hicho kitaboresha sana ufanisi wa uwekezaji wako. Kama unajua kusoma na kuandika unaweza kupiga mahesabu wewe mwenyewe na kupata tathmini kamili. Kumbuka kuwa naongelea zaidi anayeanza kuwekeza katika ardhi na majengo.

Tatu.

Tathmini Asilimia Ya Kipato.

Katika uwekezaji kwenye hisa asilimia 7.5 kwa mwaka inaweza kuwa kipato kizuri tu. Katika hatifungani asilimia 4.5 kwa mwaka inaweza kuwa kipato cha kawaida.

Lakini kama ndio unaanza kuwa mmiliki wa nyumba, asilimia 10 ya kipato ya mtaji fedha inatosha kukufanya uendelee na uwekezaji wako.

Kadri miaka inavyoendelea ndivyo asilimia za kipato zinaongezeka zaidi na zaidi. Usikubali kumiliki nyumba ambayo inaingiza kipato endelevu chini ya 10% ya thamani ya nyumba yako ya kwa mwaka.

Wengi humiliki nyumba za kupangisha ambazo hazina manufaa yoyote. Chanagamoto za nyumba za kupangisha zimewachosha.

Wamiliki hao wanakuwa hawana tena mbinu bora za kuwasaidia kuongeza kipato kupitia nyumba zao za kupangisha.

Jambo hili linakuwa ni tishio zaidi pale ambapo mtu humiliki nyumba ya kwanza ambayo haina manufaa ya moja kwa moja.

Nyumba ya kwanza ambayo haingizi kipato endelevu na kipato chanya inakuwa ni mwiba kwa mmiliki husika.

Nyumba hiyo badala ya kuwa daraja la kukuza uwekezaji wake, inakuwa ni kikwazo cha kumrudisha nyuma.

Hatua tano (5) za kumiliki nyumba ya kipato endelevu na kipato chanya ni kama ifuatavyo;-

✓ Kuwa na mawazo na maarifa sahihi.

✓ Jifunze kutoka kwenye vyanzo sahihi vya maarifa ya uwekezaji kwenye ardhi na majengo.

✓ Chagua na andika mpango sahihi kwako.

✓ Miliki nyumba sahihi ya kupangisha kwako.

✓ Simamia nyumba yako kwa namba sahihi za uwekezaji kwenye nyumba za kupangisha.

Nifanye niwe mmoja wa wanatimu wako wa uwekezaji kwenye ardhi na majengo. Unaweza kunifanya kuwa mmoja wa wanatimu wako kwa kulipia ada ya kundi la UWEKEZAJI MAJENGO.

Ukiwa mwanachama wa kundi hili, nitashirikiana na wewe kwenye kila kitu kuhusu uwekezaji kwenye ardhi na majengo.

Rafiki yako,

Aliko Musa.

WhatsApp/Calls: +255 752 413 711
 
Binafsi huwa naunga mkono masuala ya kitaalamu hasa yaliyofanyiwa tafiti ili kurahisisha maisha kwa watu wengine kupitia kujifunza. Lakini, nimekuja kugundua ( kwa maoni yangu binafsi) kuna baadhi ya mambo yanasemwa na watu ambayo ni nadharia sana na hayana ukweli katika mazingira yetu ya kawaida. Mfano ni suala la kumwambia mtu asikope kwa ajili ya kujenga nyumba, kwamba afanye savings mpaka hapo atakapokuwa na uwezo wa kujenga nyumba yake mwenyewe.

Hivi jamani mtu mwenye mshahara ambao akiupata tu unaishia pengine kwenye madeni anaweza kufanya savings zipi hizo aje afikishe angalau hata 25M za kujenga nyumba? Huyu mtu unakuta kupitia mshahara wake anaweza kukopa akajenga na kuishi kwake ila anaambiwa asikope. Je, hili jambo lipo sawa?

Mfano mwingine ni wale wanakwambia ukipata mshahara utenge 50% iende kwenye mahitaji ya lazima, 30% iende kwenye mahitaji ya muhimu ila si lazima na 20% iende kwenye savings. Sasa jamani mtu mwenye mshahara wenye take home 500K, tukisema 50% iende kwenye mahitaji ya lazima (chakula, mavazi, malazi) maaa yake ni Tsh 250K.

Jamani hivi kweli unaweza kutoboa mjini kwa kulipia 250K chakula, mavazi na ulipe kodi ya nyumba kweli? Labda ukaishi kwenye nyumba ya kupanga ya kodi 30K kwa mwezi na uwe unakula mlo mmoja au miwili (mara chache sana). Sasa kiuhalisia kweli unaweza kuvumilia huko uswazi kwenye nyumba ya 30K kwa mwezi ambako ukiacha hata simu tu sebleni unaweza usiikute?. Kwamba ndio uishi huko miaka tuseme 20 mpaka uhamie kwako kweli? Utaweza wewe kijana mwenzangu? Maish yenyewe haya bongo flavour.. Walikuwa wanaweza wazee wetu wa zamani. Ila kwa sasa kama wapo basi ni vijana wachache sana.

Ukifuatilia vizuri unaona hawa washauri wamesoma vitabu ambapo waandishi wake wanaishi Marekani ama Ulaya ambako watu wanalipwa mishahara inayotosheleza mahitaji ya msingi na kubakiza chenji. Sasa bila kuangalia mazingira, unakuta mambo kama hayo anashauriwa ayafanye mtu wa bongo ambae mshahara wake ni mkia wa mbuzi, hautoboi hata robo ya mwezi. Mie nadhani hawa washauri wawe wanafanya ku-digest vizuri kwanza mambo wanayoyasoma kwenye vitabu vya Ulaya na Marekani kabla hawajawapa hayo mambo watu wa Sumbawanga ufipani ama Buza kwa mama Kibonge.

Otherwise, tuwe tunaambiwa kuwa huu ushauri ni kwa watu wenye maisha flani flani hivi ya kishua ila si kwa kila mtu..Naomba nisipigwe mawe. Ni maoni tu.
 
Binafsi huwa naunga mkono masuala ya kitaalamu hasa yaliyofanyiwa tafiti ili kurahisisha maisha kwa watu wengine kupitia kujifunza. Lakini, nimekuja kugundua ( kwa maoni yangu binafsi) kuna baadhi ya mambo yanasemwa na watu ambayo ni nadharia sana na hayana ukweli katika mazingira yetu ya kawaida. Mfano ni suala la kumwambia mtu asikope kwa ajili ya kujenga nyumba, kwamba afanye savings mpaka hapo atakapokuwa na uwezo wa kujenga nyumba yake mwenyewe.

Hivi jamani mtu mwenye mshahara ambao akiupata tu unaishia pengine kwenye madeni anaweza kufanya savings zipi hizo aje afikishe angalau hata 25M za kujenga nyumba? Huyu mtu unakuta kupitia mshahara wake anaweza kukopa akajenga na kuishi kwake ila anaambiwa asikope. Je, hili jambo lipo sawa?

Mfano mwingine ni wale wanakwambia ukipata mshahara utenge 50% iende kwenye mahitaji ya lazima, 30% iende kwenye mahitaji ya muhimu ila si lazima na 20% iende kwenye savings. Sasa jamani mtu mwenye mshahara wenye take home 500K, tukisema 50% iende kwenye mahitaji ya lazima (chakula, mavazi, malazi) maaa yake ni Tsh 250K.

Jamani hivi kweli unaweza kutoboa mjini kwa kulipia 250K chakula, mavazi na ulipe kodi ya nyumba kweli? Labda ukaishi kwenye nyumba ya kupanga ya kodi 30K kwa mwezi na uwe unakula mlo mmoja au miwili (mara chache sana). Sasa kiuhalisia kweli unaweza kuvumilia huko uswazi kwenye nyumba ya 30K kwa mwezi ambako ukiacha hata simu tu sebleni unaweza usiikute?. Kwamba ndio uishi huko miaka tuseme 20 mpaka uhamie kwako kweli? Utaweza wewe kijana mwenzangu? Maish yenyewe haya bongo flavour.. Walikuwa wanaweza wazee wetu wa zamani. Ila kwa sasa kama wapo basi ni vijana wachache sana.

Ukifuatilia vizuri unaona hawa washauri wamesoma vitabu ambapo waandishi wake wanaishi Marekani ama Ulaya ambako watu wanalipwa mishahara inayotosheleza mahitaji ya msingi na kubakiza chenji. Sasa bila kuangalia mazingira, unakuta mambo kama hayo anashauriwa ayafanye mtu wa bongo ambae mshahara wake ni mkia wa mbuzi, hautoboi hata robo ya mwezi. Mie nadhani hawa washauri wawe wanafanya ku-digest vizuri kwanza mambo wanayoyasoma kwenye vitabu vya Ulaya na Marekani kabla hawajawapa hayo mambo watu wa Sumbawanga ufipani ama Buza kwa mama Kibonge.

Otherwise, tuwe tunaambiwa kuwa huu ushauri ni kwa watu wenye maisha flani flani hivi ya kishua ila si kwa kila mtu..Naomba nisishambuliwe ha ha haa

Umenena Vizuri sana rafiki yangu,

Lakini binafsi ninaamini kuna mikopo mizuri na mikopo mibaya kama ambavyo nimetumia mlinganyo wa 30%.

Ni kweli vyanzo vingi vya maarifa ni ughaibuni.

Pia, kumbuka kuwa makundi mengi ya utaalamu tunategemea vyanzo vya maarifa kutoka ughaibuni kama Marekani, india, canada n.k.

Hii kwangu sio hoja. Hoja ya msingi sana uliyonena ni kuwa tuwe tunadigest maarifa ya kutoa kwa wengine kabla ya kuwashirikisha.

Muhimu; huwa siandiki kuhusu nyumba za kuishi. Nimelenga wawekezaji kwenye ardhi na majengo ambao wanahitaji kujenga utajiri mkubwa kupitia uwekezaji huu.

Na kutokopa kwenye uwekezaji wa ardhi na majengo ni kipengele cha mbinu ya B-R-R-R-R ya nyumba za kupangisha.

Mbinu hii inawafaa ambao wanaweza kuweka kiasi kikubwa cha akiba kwa ajili kumiliki nyumba ya kwanza.

Nashukuru sana kwa kuandika maoni yenye ushauri mzuri ndani.

Karibu sana rafiki.

Rafiki yako,

Aliko Musa.
 
Binafsi huwa naunga mkono masuala ya kitaalamu hasa yaliyofanyiwa tafiti ili kurahisisha maisha kwa watu wengine kupitia kujifunza. Lakini, nimekuja kugundua ( kwa maoni yangu binafsi) kuna baadhi ya mambo yanasemwa na watu ambayo ni nadharia sana na hayana ukweli katika mazingira yetu ya kawaida. Mfano ni suala la kumwambia mtu asikope kwa ajili ya kujenga nyumba, kwamba afanye savings mpaka hapo atakapokuwa na uwezo wa kujenga nyumba yake mwenyewe.

Hivi jamani mtu mwenye mshahara ambao akiupata tu unaishia pengine kwenye madeni anaweza kufanya savings zipi hizo aje afikishe angalau hata 25M za kujenga nyumba? Huyu mtu unakuta kupitia mshahara wake anaweza kukopa akajenga na kuishi kwake ila anaambiwa asikope. Je, hili jambo lipo sawa?

Mfano mwingine ni wale wanakwambia ukipata mshahara utenge 50% iende kwenye mahitaji ya lazima, 30% iende kwenye mahitaji ya muhimu ila si lazima na 20% iende kwenye savings. Sasa jamani mtu mwenye mshahara wenye take home 500K, tukisema 50% iende kwenye mahitaji ya lazima (chakula, mavazi, malazi) maaa yake ni Tsh 250K.

Jamani hivi kweli unaweza kutoboa mjini kwa kulipia 250K chakula, mavazi na ulipe kodi ya nyumba kweli? Labda ukaishi kwenye nyumba ya kupanga ya kodi 30K kwa mwezi na uwe unakula mlo mmoja au miwili (mara chache sana). Sasa kiuhalisia kweli unaweza kuvumilia huko uswazi kwenye nyumba ya 30K kwa mwezi ambako ukiacha hata simu tu sebleni unaweza usiikute?. Kwamba ndio uishi huko miaka tuseme 20 mpaka uhamie kwako kweli? Utaweza wewe kijana mwenzangu? Maish yenyewe haya bongo flavour.. Walikuwa wanaweza wazee wetu wa zamani. Ila kwa sasa kama wapo basi ni vijana wachache sana.

Ukifuatilia vizuri unaona hawa washauri wamesoma vitabu ambapo waandishi wake wanaishi Marekani ama Ulaya ambako watu wanalipwa mishahara inayotosheleza mahitaji ya msingi na kubakiza chenji. Sasa bila kuangalia mazingira, unakuta mambo kama hayo anashauriwa ayafanye mtu wa bongo ambae mshahara wake ni mkia wa mbuzi, hautoboi hata robo ya mwezi. Mie nadhani hawa washauri wawe wanafanya ku-digest vizuri kwanza mambo wanayoyasoma kwenye vitabu vya Ulaya na Marekani kabla hawajawapa hayo mambo watu wa Sumbawanga ufipani ama Buza kwa mama Kibonge.

Otherwise, tuwe tunaambiwa kuwa huu ushauri ni kwa watu wenye maisha flani flani hivi ya kishua ila si kwa kila mtu..Naomba nisishambuliwe ha ha haa
Upo sahihi mkuu, japo inawezekana ukiweza kuji control na kuishi kimachale kama vile kesho hautopata kitu.
Ubaya ni kwamba nature ya human behavior as income inavyoongezeka automatically spending zinaongezeka.
Ni ngumu ila inawezekana, wa chagga ukikutana nao yani unaweza mdharau kinoma, coz hawapandi na maisha wakiwa kwenye utafutaji, akifika level flani ndio anaanza kupanda sasa na kuishi kulingana na kipato chake ila mwanzo huwa wnajinyima mno mpaka wawe financially stable.
Same thing to Wapemba na Wachina, yani mpemba utakuta kavaa kanzu yake ndani ana bukta ya kutunzia mauzo yake, anaishi pa kawaida huku akikuza biashara yake, asubuhi unaweza kuta kabeba lunch box yake kutoka nyumbani .
Ni ngumu ila inawezekana
 
Upo sahihi mkuu, japo inawezekana ukiweza kuji control na kuishi kimachale kama vile kesho hautopata kitu.
Ubaya ni kwamba nature ya human behavior as income inavyoongezeka automatically spending zinaongezeka.
Ni ngumu ila inawezekana, wa chagga ukikutana nao yani unaweza mdharau kinoma, coz hawapandi na maisha wakiwa kwenye utafutaji, akifika level flani ndio anaanza kupanda sasa na kuishi kulingana na kipato chake ila mwanzo huwa wnajinyima mno mpaka wawe financially stable.
Same thing to Wapemba na Wachina, yani mpemba utakuta kavaa kanzu yake ndani ana bukta ya kutunzia mauzo yake, anaishi pa kawaida huku akikuza biashara yake, asubuhi unaweza kuta kabeba lunch box yake kutoka nyumbani .
Ni ngumu ila inawezekana

Nimependa sana mchango wako.
 
Binafsi huwa naunga mkono masuala ya kitaalamu hasa yaliyofanyiwa tafiti ili kurahisisha maisha kwa watu wengine kupitia kujifunza. Lakini, nimekuja kugundua ( kwa maoni yangu binafsi) kuna baadhi ya mambo yanasemwa na watu ambayo ni nadharia sana na hayana ukweli katika mazingira yetu ya kawaida. Mfano ni suala la kumwambia mtu asikope kwa ajili ya kujenga nyumba, kwamba afanye savings mpaka hapo atakapokuwa na uwezo wa kujenga nyumba yake mwenyewe.

Hivi jamani mtu mwenye mshahara ambao akiupata tu unaishia pengine kwenye madeni anaweza kufanya savings zipi hizo aje afikishe angalau hata 25M za kujenga nyumba? Huyu mtu unakuta kupitia mshahara wake anaweza kukopa akajenga na kuishi kwake ila anaambiwa asikope. Je, hili jambo lipo sawa?

Mfano mwingine ni wale wanakwambia ukipata mshahara utenge 50% iende kwenye mahitaji ya lazima, 30% iende kwenye mahitaji ya muhimu ila si lazima na 20% iende kwenye savings. Sasa jamani mtu mwenye mshahara wenye take home 500K, tukisema 50% iende kwenye mahitaji ya lazima (chakula, mavazi, malazi) maaa yake ni Tsh 250K.

Jamani hivi kweli unaweza kutoboa mjini kwa kulipia 250K chakula, mavazi na ulipe kodi ya nyumba kweli? Labda ukaishi kwenye nyumba ya kupanga ya kodi 30K kwa mwezi na uwe unakula mlo mmoja au miwili (mara chache sana). Sasa kiuhalisia kweli unaweza kuvumilia huko uswazi kwenye nyumba ya 30K kwa mwezi ambako ukiacha hata simu tu sebleni unaweza usiikute?. Kwamba ndio uishi huko miaka tuseme 20 mpaka uhamie kwako kweli? Utaweza wewe kijana mwenzangu? Maish yenyewe haya bongo flavour.. Walikuwa wanaweza wazee wetu wa zamani. Ila kwa sasa kama wapo basi ni vijana wachache sana.

Ukifuatilia vizuri unaona hawa washauri wamesoma vitabu ambapo waandishi wake wanaishi Marekani ama Ulaya ambako watu wanalipwa mishahara inayotosheleza mahitaji ya msingi na kubakiza chenji. Sasa bila kuangalia mazingira, unakuta mambo kama hayo anashauriwa ayafanye mtu wa bongo ambae mshahara wake ni mkia wa mbuzi, hautoboi hata robo ya mwezi. Mie nadhani hawa washauri wawe wanafanya ku-digest vizuri kwanza mambo wanayoyasoma kwenye vitabu vya Ulaya na Marekani kabla hawajawapa hayo mambo watu wa Sumbawanga ufipani ama Buza kwa mama Kibonge.

Otherwise, tuwe tunaambiwa kuwa huu ushauri ni kwa watu wenye maisha flani flani hivi ya kishua ila si kwa kila mtu..Naomba nisishambuliwe ha ha haa
Safi Sana ndugu .
Nyongeza ya hapo ni kwamba kwa maisha yetu ya kibongo bongo ,mtu una mshahara ila unategemewa na ukoo mzima alafu ufanye serving kwa njia ipi
 
Upo sahihi mkuu, japo inawezekana ukiweza kuji control na kuishi kimachale kama vile kesho hautopata kitu.
Ubaya ni kwamba nature ya human behavior as income inavyoongezeka automatically spending zinaongezeka.
Ni ngumu ila inawezekana, wa chagga ukikutana nao yani unaweza mdharau kinoma, coz hawapandi na maisha wakiwa kwenye utafutaji, akifika level flani ndio anaanza kupanda sasa na kuishi kulingana na kipato chake ila mwanzo huwa wnajinyima mno mpaka wawe financially stable.
Same thing to Wapemba na Wachina, yani mpemba utakuta kavaa kanzu yake ndani ana bukta ya kutunzia mauzo yake, anaishi pa kawaida huku akikuza biashara yake, asubuhi unaweza kuta kabeba lunch box yake kutoka nyumbani .
Ni ngumu ila inawezekana
Mkuu, kwa jinsi nijuavyo, vijana wengi huanza kupambana rasmi na maisha kuanzia miaka 25 na kuendelea. Huu ni wakati ambao vijana wengi wanakuwa wamemaliza masomo ya Chuo Kikuu. Sasa tunaposema tu adopt hii theory ya kujibana sana ili huko baade tutoboe kama hao wachagga, wapemba n.k uliowataja, kwa uzoefu wangu, ili mtu mwenye kipato cha 500K kwa mwezi afanye savings 20% ya kipato chake mpaka aweze kufikisha angalau 25M, itachukuwa angalau si chini ya miaka 15. Kama atatoboa chini ya hapo kutokana na kuongezeka kwa kipato chake basi ni jambo la kumshukuru sana Mungu. Japo kutokana na uncertainties za hapa na pale si kawaida sana. Mara nyingi mambo hayaendi kama ulivyotarajia.

Sasa tukichukua miaka 25 alipoanza huko kujibana unakokusema, ukajumlisha hiyo miaka 15 maana yake anakuwa na miaka 40 kipindi hicho. Hapo anakuwa amebakiza miaka 10 tu afikishe miaka 50 ambapo tayari anakuwa ameingia katika kundi la watu waliopo kwenye risks kubwa ya kupatwa magonjwa ya uzeeni ikiwamo pressure, kisukari, mgongo, miguu n.k

Sasa Mkuu wangu, we unaona ni sawa uishi maisha ya shida kwa miaka 15 kisha uje upate kaunafuu kwa miaka 10 tu ambapo napo hauna uhakika sana maana inategemea? Hii ni kwasababu hata hizo pesa ulizokusanya kumbuka siyo nyingi za kukufanya uishi maisha ya kishua kivile. Kama huna nyumba zitaishia kwenye ujenzi. Kama umeziweka kwenye biashara napo itategemea.

Badala yake, kwa maoni yangu, nini kifanyike?

1. Binadamu hasa wabongo tupunguze kuwa 'over ambitious' kuhusu maisha ya mafanikio.

2. Appreciate ulichonacho na jitahidi kuishi maisha ya kawaida kulingana kipato chako. Siyo kimaskini sana wala siyo kwa kutapanya pesa.

3. Ni vizuri kuwa na malengo na kufanya kazi kwa bidii katika maisha, ila katu usijipe pressure ya kukimbizana na kitu kinaitwa mafanikio. Utaishia kupata magonjwa ya moyo tu. Fanya kazi kwa bidii na tumia pesa kidogo ulizonazo vizuri uishi maisha ya kawaida na endapo hayo mafanikio yatakuja basi iwe ni matokeo tu katika maisha. Ila lengo la la kwanza isiwe ni kujitaabisha kuutafuta utajiri.

4. Ukiwasikiliza vizuri watu wanaohamasisha watu wengine wawe matajiri utagundua wamesoma kwenye vitabu vinavyohamasisha maisha ya mafanikio kutoka kwa waandishi ambao wengi wo, siyo wote lakini, ni wazee wanaoishi Ulaya ama Marekani. Wanasahau kuwaambia watu ukweli kuwa masuala ya mafanikio siyo rahisi na hayaji kwa muda mfupi ndio maana na wao wanayasema hayo mafanikio baada ya kuishi muda mrefu karibia na uzeeni kabisa. Tena ni watu wachache tu.

5. Isitoshe, waandishi wengi wanaishi Ulaya na Marekani ambako mazingira na mifumo yao ya maisha ni tofauti kabisa na maisha yetu. Huko Marekani na Ulaya watu wanalipwa pesa zinazotosha mahitaji ya kila mwezi na kubakiza savings. Sasa huku kwetu ni asilimia ngapi ya watu tunaishi kwa maisha hayo?

6. Mkuu, siyo kwamba nipo hapa kukatisha tamaa watu, ila ukweli ni kuwa, kwa uchunguzi wangu, katika watu angalau 100 wanaotoboa kimaisha wanaweza wasifike hata watano. Kutoboa kwenye maisha ni suala complex sana.

7. Izingatiwe kuwa sihamasishi watu wasivisome vitabu vinavyohamasisha mafanikio badala yake tuwe tuna digest sana na kuangalia uhalisia katika maisha yetu.

8. Ukivisoma hivyo vitabu unaweza dhani kwamba Ulaya na Marekani watu wanaishi maisha yenye kufuata sana malengo na utajiri. Mimi nimefanikiwa kuishi nchi mbili za Ulaya, kwa kaisi kikubwa watu wa Ulaya wanaishi maisha ya kawaida tu. Mtu anazaliwa, anasoma (tena mwisho wengi wanakomea bachelor tu), kisha wanaajiriwa na kufanya kazi na kula maisha bila kukimbizana na kinachoitwa kutafuta mafanikio ama utajiri.

9. Kinachowasaidia wao ni kuwa miondombinu yao ni mizuri na vipato wanavyopata vinatosheleza kukidhi mahitaji ya mwezi mzima na kubakiza chenji kidogo. Tena wengi wao wanaishi tu kwenye apartments. Ulaya mtu anayeishi kwenye nyumba yake kwa kumiliki ni wachache sana hasa wenye vipato vya juu sana.

10. Ofcourse, mambo ya kutafuta sana mafanikio yapo kwenye nchi zetu maskini ambako kuna madaraja makubwa kati ya watu wenye nacho na wasio kuwa nacho. Kingine ni kuwa miundombinu yetu kama usafiri, elimu na afya bado ni changamoto. Ila wenzetu hiyo miundombinu ipo vizuri na wanachokiangalia raia wengi ni kwamba wanaishi kwa furaha na familia zao na wanafanya kazi za kupata vipato kutosheleza mahitaji yao basi.


Ni hayo tu kwa sasa. Naomba nisipigwe mawe.!
 
Mkuu, kwa jinsi nijuavyo, vijana wengi huanza kupambana rasmi na maisha kuanzia miaka 25 na kuendelea. Huu ni wakati ambao vijana wengi wanakuwa wamemaliza masomo ya Chuo Kikuu. Sasa tunaposema tu adopt hii theory ya kujibana sana ili huko baade tutoboe kama hao wachagga, wapemba n.k uliowataja, kwa uzoefu wangu, ili mtu mwenye kipato cha 500K kwa mwezi afanye savings 20% ya kipato chake mpaka aweze kufikisha angalau 25M, itachukuwa angalau si chini ya miaka 15. Kama atatoboa chini ya hapo kutokana na kuongezeka kwa kipato chake basi ni jambo la kumshukuru sana Mungu. Japo kutokana na uncertainties za hapa na pale si kawaida sana. Mara nyingi mambo hayaendi kama ulivyotarajia.

Sasa tukichukua miaka 25 alipoanza huko kujibana unakokusema, ukajumlisha hiyo miaka 15 maana yake anakuwa na miaka 40 kipindi hicho. Hapo anakuwa amebakiza miaka 10 tu afikishe miaka 50 ambapo tayari anakuwa ameingia katika kundi la watu waliopo kwenye risks kubwa ya kupatwa magonjwa ya uzeeni ikiwamo pressure, kisukari, mgongo, miguu n.k

Sasa Mkuu wangu, we unaona ni sawa uishi maisha ya shida kwa miaka 15 kisha uje upate kaunafuu kwa miaka 10 tu ambapo napo hauna uhakika sana maana inategemea? Hii ni kwasababu hata hizo pesa ulizokusanya kumbuka siyo nyingi za kukufanya uishi maisha ya kishua kivile. Kama huna nyumba zitaishia kwenye ujenzi. Kama umeziweka kwenye biashara napo itategemea.

Badala yake, kwa maoni yangu, nini kifanyike?

1. Binadamu hasa wabongo tupunguze kuwa 'over ambitious' kuhusu maisha ya mafanikio.

2. Appreciate ulichonacho na jitahidi kuishi maisha ya kawaida kulingana kipato chako. Siyo kimaskini sana wala siyo kwa kutapanya pesa.

3. Ni vizuri kuwa na malengo na kufanya kazi kwa bidii katika maisha, ila katu usijipe pressure ya kukimbizana na kitu kinaitwa mafanikio. Utaishia kupata magonjwa ya moyo tu. Fanya kazi kwa bidii na tumia pesa kidogo ulizonazo vizuri uishi maisha ya kawaida na endapo hayo mafanikio yatakuja basi iwe ni matokeo tu katika maisha. Ila lengo la la kwanza isiwe ni kujitaabisha kuutafuta utajiri.

4. Ukiwasikiliza vizuri watu wanaohamasisha watu wengine wawe matajiri utagundua wamesoma kwenye vitabu vinavyohamasisha maisha ya mafanikio kutoka kwa waandishi ambao wengi wo, siyo wote lakini, ni wazee wanaoishi Ulaya ama Marekani. Wanasahau kuwaambia watu ukweli kuwa masuala ya mafanikio siyo rahisi na hayaji kwa muda mfupi ndio maana na wao wanayasema hayo mafanikio baada ya kuishi muda mrefu karibia na uzeeni kabisa. Tena ni watu wachache tu.

5. Isitoshe, waandishi wengi wanaishi Ulaya na Marekani ambako mazingira na mifumo yao ya maisha ni tofauti kabisa na maisha yetu. Huko Marekani na Ulaya watu wanalipwa pesa zinazotosha mahitaji ya kila mwezi na kubakiza savings. Sasa huku kwetu ni asilimia ngapi ya watu tunaishi kwa maisha hayo?

6. Mkuu, siyo kwamba nipo hapa kukatisha tamaa watu, ila ukweli ni kuwa, kwa uchunguzi wangu, katika watu angalau 100 wanaotoboa kimaisha wanaweza wasifike hata watano. Kutoboa kwenye maisha ni suala complex sana.

7. Izingatiwe kuwa sihamasishi watu wasivisome vitabu vinavyohamasisha mafanikio badala yake tuwe tuna digest sana na kuangalia uhalisia katika maisha yetu.

8. Ukivisoma hivyo vitabu unaweza dhani kwamba Ulaya na Marekani watu wanaishi maisha yenye kufuata sana malengo na utajiri. Mimi nimefanikiwa kuishi nchi mbili za Ulaya, kwa kaisi kikubwa watu wa Ulaya wanaishi maisha ya kawaida tu. Mtu anazaliwa, anasoma (tena mwisho wengi wanakomea bachelor tu), kisha wanaajiriwa na kufanya kazi na kula maisha bila kukimbizana na kinachoitwa kutafuta mafanikio ama utajiri.

9. Kinachowasaidia wao ni kuwa miondombinu yao ni mizuri na vipato wanavyopata vinatosheleza kukidhi mahitaji ya mwezi mzima na kubakiza chenji kidogo. Tena wengi wao wanaishi tu kwenye apartments. Ulaya mtu anayeishi kwenye nyumba yake kwa kumiliki ni wachache sana hasa wenye vipato vya juu sana.

10. Ofcourse, mambo ya kutafuta sana mafanikio yapo kwenye nchi zetu maskini ambako kuna madaraja makubwa kati ya watu wenye nacho na wasio kuwa nacho. Kingine ni kuwa miundombinu yetu kama usafiri, elimu na afya bado ni changamoto. Ila wenzetu hiyo miundombinu ipo vizuri na wanachokiangalia raia wengi ni kwamba wanaishi kwa furaha na familia zao na wanafanya kazi za kupata vipato kutosheleza mahitaji yao basi.


Ni hayo tu kwa sasa. Naomba nisipigwe mawe.!
Upo sahihi kabisa na nakubaliana na wewe, sema tu njia yako wewe ni kuwashauri watu wasiwe too ambitious which i support but savings, investing, ni vitu ambavyo wanatakiwa wajifunze.
Umepigia hesabu kuwa it will take them 15 years ili wafikie malengo, ila umesahau kuwa akianza na salary ya 500k kuwa atakuja kupandishwa cheo, au kama ameanza na biashara slowly itakuja kumpa profit zaidi nk
Huenda asifike 15 years within 5 years akaanza kutoboa taratibu.
Hio pesa pia kama ameiweka kama savings ndio haitokuwa, ila kama kai invest hio pesa thamani yake itapanda kadri miaka inavyozidi kwenda.
Motivational speakers wengi ubaya ni wanaharibu vijana wengi kuwaza kuwa atakaa nyumbani tu bila kujituma alafu atatoboa maisha, anawaza kufanya kazi ni upuuzi anataka apewe mtaji wa million 10 wakat hata biashara ndogo ndogo hajawai kujaribu, anawaza kufanya internship au volunteer ni waste of time wakati kuna skills ange gain ambazo zingekuja kumsaidia kwenye career yake au biashara zake.
Ninachoona tukubaliane kuwa kujifunza about savings, investment sio shida sema shida ipo kwa mtu kukaa na kusubiri kikubwa na kuamini kuwa pamoja na elimu yake, nguvu zake hawezi kufanya kitu.
 
Binafsi huwa naunga mkono masuala ya kitaalamu hasa yaliyofanyiwa tafiti ili kurahisisha maisha kwa watu wengine kupitia kujifunza. Lakini, nimekuja kugundua ( kwa maoni yangu binafsi) kuna baadhi ya mambo yanasemwa na watu ambayo ni nadharia sana na hayana ukweli katika mazingira yetu ya kawaida. Mfano ni suala la kumwambia mtu asikope kwa ajili ya kujenga nyumba, kwamba afanye savings mpaka hapo atakapokuwa na uwezo wa kujenga nyumba yake mwenyewe.

Hivi jamani mtu mwenye mshahara ambao akiupata tu unaishia pengine kwenye madeni anaweza kufanya savings zipi hizo aje afikishe angalau hata 25M za kujenga nyumba? Huyu mtu unakuta kupitia mshahara wake anaweza kukopa akajenga na kuishi kwake ila anaambiwa asikope. Je, hili jambo lipo sawa?

Mfano mwingine ni wale wanakwambia ukipata mshahara utenge 50% iende kwenye mahitaji ya lazima, 30% iende kwenye mahitaji ya muhimu ila si lazima na 20% iende kwenye savings. Sasa jamani mtu mwenye mshahara wenye take home 500K, tukisema 50% iende kwenye mahitaji ya lazima (chakula, mavazi, malazi) maaa yake ni Tsh 250K.

Jamani hivi kweli unaweza kutoboa mjini kwa kulipia 250K chakula, mavazi na ulipe kodi ya nyumba kweli? Labda ukaishi kwenye nyumba ya kupanga ya kodi 30K kwa mwezi na uwe unakula mlo mmoja au miwili (mara chache sana). Sasa kiuhalisia kweli unaweza kuvumilia huko uswazi kwenye nyumba ya 30K kwa mwezi ambako ukiacha hata simu tu sebleni unaweza usiikute?. Kwamba ndio uishi huko miaka tuseme 20 mpaka uhamie kwako kweli? Utaweza wewe kijana mwenzangu? Maish yenyewe haya bongo flavour.. Walikuwa wanaweza wazee wetu wa zamani. Ila kwa sasa kama wapo basi ni vijana wachache sana.

Ukifuatilia vizuri unaona hawa washauri wamesoma vitabu ambapo waandishi wake wanaishi Marekani ama Ulaya ambako watu wanalipwa mishahara inayotosheleza mahitaji ya msingi na kubakiza chenji. Sasa bila kuangalia mazingira, unakuta mambo kama hayo anashauriwa ayafanye mtu wa bongo ambae mshahara wake ni mkia wa mbuzi, hautoboi hata robo ya mwezi. Mie nadhani hawa washauri wawe wanafanya ku-digest vizuri kwanza mambo wanayoyasoma kwenye vitabu vya Ulaya na Marekani kabla hawajawapa hayo mambo watu wa Sumbawanga ufipani ama Buza kwa mama Kibonge.

Otherwise, tuwe tunaambiwa kuwa huu ushauri ni kwa watu wenye maisha flani flani hivi ya kishua ila si kwa kila mtu..Naomba nisishambuliwe ha ha haa
Nakazia
 
Upo sahihi kabisa na nakubaliana na wewe, sema tu njia yako wewe ni kuwashauri watu wasiwe too ambitious which i support but savings, investing, ni vitu ambavyo wanatakiwa wajifunze.
Umepigia hesabu kuwa it will take them 15 years ili wafikie malengo, ila umesahau kuwa akianza na salary ya 500k kuwa atakuja kupandishwa cheo, au kama ameanza na biashara slowly itakuja kumpa profit zaidi nk
Huenda asifike 15 years within 5 years akaanza kutoboa taratibu.
Hio pesa pia kama ameiweka kama savings ndio haitokuwa, ila kama kai invest hio pesa thamani yake itapanda kadri miaka inavyozidi kwenda.
Motivational speakers wengi ubaya ni wanaharibu vijana wengi kuwaza kuwa atakaa nyumbani tu bila kujituma alafu atatoboa maisha, anawaza kufanya kazi ni upuuzi anataka apewe mtaji wa million 10 wakat hata biashara ndogo ndogo hajawai kujaribu, anawaza kufanya internship au volunteer ni waste of time wakati kuna skills ange gain ambazo zingekuja kumsaidia kwenye career yake au biashara zake.
Ninachoona tukubaliane kuwa kujifunza about savings, investment sio shida sema shida ipo kwa mtu kukaa na kusubiri kikubwa na kuamini kuwa pamoja na elimu yake, nguvu zake hawezi kufanya kitu.

Safi sana.

Nakuunga mkono kwa 100%
 
Mkuu, kwa jinsi nijuavyo, vijana wengi huanza kupambana rasmi na maisha kuanzia miaka 25 na kuendelea. Huu ni wakati ambao vijana wengi wanakuwa wamemaliza masomo ya Chuo Kikuu. Sasa tunaposema tu adopt hii theory ya kujibana sana ili huko baade tutoboe kama hao wachagga, wapemba n.k uliowataja, kwa uzoefu wangu, ili mtu mwenye kipato cha 500K kwa mwezi afanye savings 20% ya kipato chake mpaka aweze kufikisha angalau 25M, itachukuwa angalau si chini ya miaka 15. Kama atatoboa chini ya hapo kutokana na kuongezeka kwa kipato chake basi ni jambo la kumshukuru sana Mungu. Japo kutokana na uncertainties za hapa na pale si kawaida sana. Mara nyingi mambo hayaendi kama ulivyotarajia.

Sasa tukichukua miaka 25 alipoanza huko kujibana unakokusema, ukajumlisha hiyo miaka 15 maana yake anakuwa na miaka 40 kipindi hicho. Hapo anakuwa amebakiza miaka 10 tu afikishe miaka 50 ambapo tayari anakuwa ameingia katika kundi la watu waliopo kwenye risks kubwa ya kupatwa magonjwa ya uzeeni ikiwamo pressure, kisukari, mgongo, miguu n.k

Sasa Mkuu wangu, we unaona ni sawa uishi maisha ya shida kwa miaka 15 kisha uje upate kaunafuu kwa miaka 10 tu ambapo napo hauna uhakika sana maana inategemea? Hii ni kwasababu hata hizo pesa ulizokusanya kumbuka siyo nyingi za kukufanya uishi maisha ya kishua kivile. Kama huna nyumba zitaishia kwenye ujenzi. Kama umeziweka kwenye biashara napo itategemea.

Badala yake, kwa maoni yangu, nini kifanyike?

1. Binadamu hasa wabongo tupunguze kuwa 'over ambitious' kuhusu maisha ya mafanikio.

2. Appreciate ulichonacho na jitahidi kuishi maisha ya kawaida kulingana kipato chako. Siyo kimaskini sana wala siyo kwa kutapanya pesa.

3. Ni vizuri kuwa na malengo na kufanya kazi kwa bidii katika maisha, ila katu usijipe pressure ya kukimbizana na kitu kinaitwa mafanikio. Utaishia kupata magonjwa ya moyo tu. Fanya kazi kwa bidii na tumia pesa kidogo ulizonazo vizuri uishi maisha ya kawaida na endapo hayo mafanikio yatakuja basi iwe ni matokeo tu katika maisha. Ila lengo la la kwanza isiwe ni kujitaabisha kuutafuta utajiri.

4. Ukiwasikiliza vizuri watu wanaohamasisha watu wengine wawe matajiri utagundua wamesoma kwenye vitabu vinavyohamasisha maisha ya mafanikio kutoka kwa waandishi ambao wengi wo, siyo wote lakini, ni wazee wanaoishi Ulaya ama Marekani. Wanasahau kuwaambia watu ukweli kuwa masuala ya mafanikio siyo rahisi na hayaji kwa muda mfupi ndio maana na wao wanayasema hayo mafanikio baada ya kuishi muda mrefu karibia na uzeeni kabisa. Tena ni watu wachache tu.

5. Isitoshe, waandishi wengi wanaishi Ulaya na Marekani ambako mazingira na mifumo yao ya maisha ni tofauti kabisa na maisha yetu. Huko Marekani na Ulaya watu wanalipwa pesa zinazotosha mahitaji ya kila mwezi na kubakiza savings. Sasa huku kwetu ni asilimia ngapi ya watu tunaishi kwa maisha hayo?

6. Mkuu, siyo kwamba nipo hapa kukatisha tamaa watu, ila ukweli ni kuwa, kwa uchunguzi wangu, katika watu angalau 100 wanaotoboa kimaisha wanaweza wasifike hata watano. Kutoboa kwenye maisha ni suala complex sana.

7. Izingatiwe kuwa sihamasishi watu wasivisome vitabu vinavyohamasisha mafanikio badala yake tuwe tuna digest sana na kuangalia uhalisia katika maisha yetu.

8. Ukivisoma hivyo vitabu unaweza dhani kwamba Ulaya na Marekani watu wanaishi maisha yenye kufuata sana malengo na utajiri. Mimi nimefanikiwa kuishi nchi mbili za Ulaya, kwa kaisi kikubwa watu wa Ulaya wanaishi maisha ya kawaida tu. Mtu anazaliwa, anasoma (tena mwisho wengi wanakomea bachelor tu), kisha wanaajiriwa na kufanya kazi na kula maisha bila kukimbizana na kinachoitwa kutafuta mafanikio ama utajiri.

9. Kinachowasaidia wao ni kuwa miondombinu yao ni mizuri na vipato wanavyopata vinatosheleza kukidhi mahitaji ya mwezi mzima na kubakiza chenji kidogo. Tena wengi wao wanaishi tu kwenye apartments. Ulaya mtu anayeishi kwenye nyumba yake kwa kumiliki ni wachache sana hasa wenye vipato vya juu sana.

10. Ofcourse, mambo ya kutafuta sana mafanikio yapo kwenye nchi zetu maskini ambako kuna madaraja makubwa kati ya watu wenye nacho na wasio kuwa nacho. Kingine ni kuwa miundombinu yetu kama usafiri, elimu na afya bado ni changamoto. Ila wenzetu hiyo miundombinu ipo vizuri na wanachokiangalia raia wengi ni kwamba wanaishi kwa furaha na familia zao na wanafanya kazi za kupata vipato kutosheleza mahitaji yao basi.


Ni hayo tu kwa sasa. Naomba nisipigwe mawe.!

Vizuri sana,

Maisha ni uchaguzi rafiki yangu, kwa asilimia kubwa umeandika ukweli.

Lakini usiogope kupigwa mawe hata siku nyingine. Ni kawaida kutofautiana hoja.

Hivyo hoja zako na za mwingine zikitofautiana hamna shida kwa sababu tuna historia tofauti, mtazamo tofauti, elimu tofauti, mazingira tofauti, tunasoma vitabu tofauti, tunazungukwa na watu tofauti.

Nashukuru sana kwa maoni yako mazuri.

Rafiki yako,

Aliko Musa.

Mbobezi wa ardhi na majengo.
 
Upo sahihi kabisa na nakubaliana na wewe, sema tu njia yako wewe ni kuwashauri watu wasiwe too ambitious which i support but savings, investing, ni vitu ambavyo wanatakiwa wajifunze.
Umepigia hesabu kuwa it will take them 15 years ili wafikie malengo, ila umesahau kuwa akianza na salary ya 500k kuwa atakuja kupandishwa cheo, au kama ameanza na biashara slowly itakuja kumpa profit zaidi nk
Huenda asifike 15 years within 5 years akaanza kutoboa taratibu.
Hio pesa pia kama ameiweka kama savings ndio haitokuwa, ila kama kai invest hio pesa thamani yake itapanda kadri miaka inavyozidi kwenda.
Motivational speakers wengi ubaya ni wanaharibu vijana wengi kuwaza kuwa atakaa nyumbani tu bila kujituma alafu atatoboa maisha, anawaza kufanya kazi ni upuuzi anataka apewe mtaji wa million 10 wakat hata biashara ndogo ndogo hajawai kujaribu, anawaza kufanya internship au volunteer ni waste of time wakati kuna skills ange gain ambazo zingekuja kumsaidia kwenye career yake au biashara zake.
Ninachoona tukubaliane kuwa kujifunza about savings, investment sio shida sema shida ipo kwa mtu kukaa na kusubiri kikubwa na kuamini kuwa pamoja na elimu yake, nguvu zake hawezi kufanya kitu.

Kwangu mimi, utajiri ni perception. Hapa nina maana kuwa ukiwa na malengo ya kutengeneza milioni moja kwa mwezi na ukaona kwako ni mafanikio makubwa ni jambo zuri sana.

Kila mtu apambanie malengo yake ya kimafanikio. Lakini kutokuwa na malengo na kuishi kama kuku wa kienyeji hapo ndipo inaanzia changamoto.

KUANZIA CHINI KABISA.

Nimependa sana ushauri wako wa vijana kutosubiri mitaji mikubwa ndipo waanze kujishughulisha.

Rafiki yako,

Aliko Musa.

Mbobezi wa ardhi na majengo.
 
Back
Top Bottom