Mambo kumi ya kuzingatia 2021 ili uishi maisha yako

Nanyaro Ephata

JF-Expert Member
Jan 22, 2011
1,221
1,788
Kwaheri 2020 karibu 2021

Awali ya yote tuna kila sababu ya Kumshukuru Mwenyenzi Mungu mwingi wa neema na Rehema.Mwaka 2020 umekuwa na changamoto lukuki,katika sekta zote,Kiuchumi,kiafya,kijamii na kisiasa.Lakini bado Mungu wetu ni mkuu sana!

Tunafahamu kuwa tuna ndugu,jamaa,marafiki ambao tulianza nao mwaka ila kwa sasa hawapo nasi.Sisi tulio baki tumebaki kwa kusudi la Mwenyenzi Mungu.Sharti tuishi kwa kusudi hilo,mwaka 2021 ukautazame kwa matumaini makubwa huku ukitenda matendo ya huruma,utu na yenye kumpendeza Mwenyenzi Mungu

Tunapoanza mwaka mpya 2021,ninakutakia Baraka za Mwenyenzi Mungu!usonge mbele kwa matumaini na imani kubwa ! lakini pia zingatia mambo haya 10 ambayo yatabadili maisha yako kabisa,yawe maisha ya furaha,upendo,amani,shukurani na ufanisi
Hizi kanuni 10 zitabadili maisha yako kabisa! Zipitie kisha uwe unazifanyia kazi kila siku kama vile ulivojizoesha ku brush meno/kinywa kila siku asubuhi baadae zitakuwa sehemu ya .maisha yako!

1.Orodhesha malengo.Hakikisha unakuwa na malengo yaliyoorodheshwa katika mpangilio unaotekelezeka! Usibuni orodhesha kile tu kinachotekelezeka!

2.Pangilia mapema.Kumbuka kila dakika unayotumia kupangilia itaokoa muda mwingi ambao ungeutumia kutekeleza kisichotekelezeka,hakikisha kila lengo linakuwa kwenye karatasi,fanya kazi kwa karatasi na kalamu daima

3.80/20 .Hakikisha unazingatia kanuni hii kuwa 20% ilete matokeo ya 80%.Yaani nguvu kubwa weka kwenye 20% ambayo italeta matokeo ya 80%

4.Fanya uchaguzi sahihi! Kwa kuwa huwezi kufanya kila kitu kwa wakati mmoja,jifunze kuweka malengo na vipaumbele,sharti vipaumbele viwe kwenye shughuli zinazoleta matokeo bora na sio bora matokeo

5.Kanuni ya Utatu.Tumia hii kanuni kwenye maisha yako yote,itakufanya uwe na muda wa kila jambo.Kanuni hii inataka 1.Fanya Uwezacho,kwa kutumia kile ulicho nacho,kwenye mahali ulipo!(usianze kulaaani kwa nini umezaliwa Tz au kwenye familia fulani au kwenye mjini fulani)

6.Tekeleza moja kwa 100%.Mshika mawili moja humponyoka,jitahidi kuhakikisha kuwa unatekeleza jambo moja kwa ukamilifu ili likupe changamoto ya kusonga mbele kwa ujasiri mkubwa

7.Fanya uchambuzi sahihi.Ukianza utekelezaji wa malengo yako chagua moja ambalo wewe ni mtaalamu wake,au moja ambalo umelitekeleza kwa umakini na weledi wa hali ya juu,kisha hili ndio liwe msingi wa kusonga mbele

8.Jipe motisha.Hakikisha unajimotisha wewe binafsi,tumia 80% ya muda wako kwenye mambo mazuri na 20% au pungufu kwenye matatizo,usiache matatizo yawe kansa kwako!

9.Usiwe mtumwa wa teknolojia. Teknolojia ni nzuri sana ila ifanye iwe mtumwa wako,wewe usiwe mtumwa wa teknolojia.Jifunze muda wa kufanya simu/laptop/tv etc na muda wa kufanya mengine(kuna watu wanaangalia TV anafuatilia tamthilia ya kifilipino hadi analala kwenye kiti)kila jambo lifanyike kwa kiasi,wengine simu hata akienda ibadani yupo busy na simu,huu ni utumwa,fanya ziwe vitendea kazi vyako na wewe uwe juu!

10. Tengeneza jedwali la Maksi.Hakikisha unakuwa na jedwali la maksi ili uzipe maksi kazi/malengo na jinsi ambavo umetekeleza kwa kila lengo na mpango wake.Hili jedwali litakusaidia kujua wapi una nguvu na wapi ni dhaifu,wapi uboreshe,wapi uongezee bidi……………..

Nawatakia nyote Baraka za Mwenyenzi Mungu mwaka huu 2021

Nanyaro EJ
 
Kwaheri 2020 karibu 2021

Awali ya yote tuna kila sababu ya Kumshukuru Mwenyenzi Mungu mwingi wa neema na Rehema.Mwaka 2020 umekuwa na changamoto lukuki,katika sekta zote,Kiuchumi,kiafya,kijamii na kisiasa.Lakini bado Mungu wetu ni mkuu sana!

Tunafahamu kuwa tuna ndugu,jamaa,marafiki ambao tulianza nao mwaka ila kwa sasa hawapo nasi.Sisi tulio baki tumebaki kwa kusudi la Mwenyenzi Mungu.Sharti tuishi kwa kusudi hilo,mwaka 2021 ukautazame kwa matumaini makubwa huku ukitenda matendo ya huruma,utu na yenye kumpendeza Mwenyenzi Mungu

Tunapoanza mwaka mpya 2021,ninakutakia Baraka za Mwenyenzi Mungu!usonge mbele kwa matumaini na imani kubwa ! lakini pia zingatia mambo haya 10 ambayo yatabadili maisha yako kabisa,yawe maisha ya furaha,upendo,amani,shukurani na ufanisi
Hizi kanuni 10 zitabadili maisha yako kabisa! Zipitie kisha uwe unazifanyia kazi kila siku kama vile ulivojizoesha ku brush meno/kinywa kila siku asubuhi baadae zitakuwa sehemu ya .maisha yako!

1.Orodhesha malengo.Hakikisha unakuwa na malengo yaliyoorodheshwa katika mpangilio unaotekelezeka! Usibuni orodhesha kile tu kinachotekelezeka!

2.Pangilia mapema.Kumbuka kila dakika unayotumia kupangilia itaokoa muda mwingi ambao ungeutumia kutekeleza kisichotekelezeka,hakikisha kila lengo linakuwa kwenye karatasi,fanya kazi kwa karatasi na kalamu daima

3.80/20 .Hakikisha unazingatia kanuni hii kuwa 20% ilete matokeo ya 80%.Yaani nguvu kubwa weka kwenye 20% ambayo italeta matokeo ya 80%

4.Fanya uchaguzi sahihi! Kwa kuwa huwezi kufanya kila kitu kwa wakati mmoja,jifunze kuweka malengo na vipaumbele,sharti vipaumbele viwe kwenye shughuli zinazoleta matokeo bora na sio bora matokeo

5.Kanuni ya Utatu.Tumia hii kanuni kwenye maisha yako yote,itakufanya uwe na muda wa kila jambo.Kanuni hii inataka 1.Fanya Uwezacho,kwa kutumia kile ulicho nacho,kwenye mahali ulipo!(usianze kulaaani kwa nini umezaliwa Tz au kwenye familia fulani au kwenye mjini fulani)

6.Tekeleza moja kwa 100%.Mshika mawili moja humponyoka,jitahidi kuhakikisha kuwa unatekeleza jambo moja kwa ukamilifu ili likupe changamoto ya kusonga mbele kwa ujasiri mkubwa

7.Fanya uchambuzi sahihi.Ukianza utekelezaji wa malengo yako chagua moja ambalo wewe ni mtaalamu wake,au moja ambalo umelitekeleza kwa umakini na weledi wa hali ya juu,kisha hili ndio liwe msingi wa kusonga mbele

8.Jipe motisha.Hakikisha unajimotisha wewe binafsi,tumia 80% ya muda wako kwenye mambo mazuri na 20% au pungufu kwenye matatizo,usiache matatizo yawe kansa kwako!

9.Usiwe mtumwa wa teknolojia. Teknolojia ni nzuri sana ila ifanye iwe mtumwa wako,wewe usiwe mtumwa wa teknolojia.Jifunze muda wa kufanya simu/laptop/tv etc na muda wa kufanya mengine(kuna watu wanaangalia TV anafuatilia tamthilia ya kifilipino hadi analala kwenye kiti)kila jambo lifanyike kwa kiasi,wengine simu hata akienda ibadani yupo busy na simu,huu ni utumwa,fanya ziwe vitendea kazi vyako na wewe uwe juu!

10. Tengeneza jedwali la Maksi.Hakikisha unakuwa na jedwali la maksi ili uzipe maksi kazi/malengo na jinsi ambavo umetekeleza kwa kila lengo na mpango wake.Hili jedwali litakusaidia kujua wapi una nguvu na wapi ni dhaifu,wapi uboreshe,wapi uongezee bidi……………..

Nawatakia nyote Baraka za Mwenyenzi Mungu mwaka huu 2021

Nanyaro EJ
Mkuu Nanyaro,

Kwanza pole kwa kuonja machungu ya utafutaji wa riziki na kutumia huku ukihakikisha kila unachopata ni hesabu ya jasho lako.

Pili nakupongezwa kutaka kuwashirikisha wengine uzoefu wako ili waepuke kulalamika bila kujua na wenyewe ni chanzo cha kutofanikiwa.

Tatu, nakuunga mkono kwa wazo hili maana linafundisha kwa vitendo namna ya kujitegemea na kusimamia kwa uchungu kipato chako ili kufikia malengo ya kimaendeleo.

Nne, unaombwa utokea mchanganuo kwa makundi yanayohusu watu waishio mijini, vijijini na wanavyuo ambao wanaweza kuwa wana miradi wakati wakiendelea na masomo ili mfumo wa kujiajiri uanze kuimarika kwenye akili za watu na mfumo wa maisha wa kila siku

Tano, mtu kama wewe nakuhesabu kama daktari mwema anayemwelekeza mgonjwa namna bora ya kupona na kudumu na afya ya kiuchumi, ubunifu tija na hamasa ya matumizi ya mawazo chanya katika jamii. Ubarikiwe sana
 
Hongera Nanyaro kwa muongozo huu muhimu. Wangalau mtu akitekeleza hata nusu ya hiyo list yako, atafanikiwa kwa kiwango cha kuridhisha ama zaidi.
 
Mkuu Nanyaro,

Kwanza pole kwa kuonja machungu ya utafutaji wa riziki na kutumia huku ukihakikisha kila unachopata ni hesabu ya jasho lako.

Pili nakupongezwa kutaka kuwashirikisha wengine uzoefu wako ili waepuke kulalamika bila kujua na wenyewe ni chanzo cha kutofanikiwa.

Tatu, nakuunga mkono kwa wazo hili maana linafundisha kwa vitendo namna ya kujitegemea na kusimamia kwa uchungu kipato chako ili kufikia malengo ya kimaendeleo.

Nne, unaombwa utokea mchanganuo kwa makundi yanayohusu watu waishio mijini, vijijini na wanavyuo ambao wanaweza kuwa wana miradi wakati wakiendelea na masomo ili mfumo wa kujiajiri uanze kuimarika kwenye akili za watu na mfumo wa maisha wa kila siku

Tano, mtu kama wewe nakuhesabu kama daktari mwema anayemwelekeza mgonjwa namna bora ya kupona na kudumu na afya ya kiuchumi, ubunifu tija na hamasa ya matumizi ya mawazo chanya katika jamii. Ubarikiwe sana
Mkuu nakushukuru sana kwa pongezi zako(I am Humbled) kwa utafiti wangu mdogo watu wengi ni sababu ya kutofanikiwa kwao! Yaani wengi wamekuwa manabii wabaya wa maisha yao wenyewe!
 
Kwaheri 2020 karibu 2021

Awali ya yote tuna kila sababu ya Kumshukuru Mwenyenzi Mungu mwingi wa neema na Rehema.Mwaka 2020 umekuwa na changamoto lukuki,katika sekta zote,Kiuchumi,kiafya,kijamii na kisiasa.Lakini bado Mungu wetu ni mkuu sana!

Tunafahamu kuwa tuna ndugu,jamaa,marafiki ambao tulianza nao mwaka ila kwa sasa hawapo nasi.Sisi tulio baki tumebaki kwa kusudi la Mwenyenzi Mungu.Sharti tuishi kwa kusudi hilo,mwaka 2021 ukautazame kwa matumaini makubwa huku ukitenda matendo ya huruma,utu na yenye kumpendeza Mwenyenzi Mungu

Tunapoanza mwaka mpya 2021,ninakutakia Baraka za Mwenyenzi Mungu!usonge mbele kwa matumaini na imani kubwa ! lakini pia zingatia mambo haya 10 ambayo yatabadili maisha yako kabisa,yawe maisha ya furaha,upendo,amani,shukurani na ufanisi
Hizi kanuni 10 zitabadili maisha yako kabisa! Zipitie kisha uwe unazifanyia kazi kila siku kama vile ulivojizoesha ku brush meno/kinywa kila siku asubuhi baadae zitakuwa sehemu ya .maisha yako!

1.Orodhesha malengo.Hakikisha unakuwa na malengo yaliyoorodheshwa katika mpangilio unaotekelezeka! Usibuni orodhesha kile tu kinachotekelezeka!

2.Pangilia mapema.Kumbuka kila dakika unayotumia kupangilia itaokoa muda mwingi ambao ungeutumia kutekeleza kisichotekelezeka,hakikisha kila lengo linakuwa kwenye karatasi,fanya kazi kwa karatasi na kalamu daima

3.80/20 .Hakikisha unazingatia kanuni hii kuwa 20% ilete matokeo ya 80%.Yaani nguvu kubwa weka kwenye 20% ambayo italeta matokeo ya 80%

4.Fanya uchaguzi sahihi! Kwa kuwa huwezi kufanya kila kitu kwa wakati mmoja,jifunze kuweka malengo na vipaumbele,sharti vipaumbele viwe kwenye shughuli zinazoleta matokeo bora na sio bora matokeo

5.Kanuni ya Utatu.Tumia hii kanuni kwenye maisha yako yote,itakufanya uwe na muda wa kila jambo.Kanuni hii inataka 1.Fanya Uwezacho,kwa kutumia kile ulicho nacho,kwenye mahali ulipo!(usianze kulaaani kwa nini umezaliwa Tz au kwenye familia fulani au kwenye mjini fulani)

6.Tekeleza moja kwa 100%.Mshika mawili moja humponyoka,jitahidi kuhakikisha kuwa unatekeleza jambo moja kwa ukamilifu ili likupe changamoto ya kusonga mbele kwa ujasiri mkubwa

7.Fanya uchambuzi sahihi.Ukianza utekelezaji wa malengo yako chagua moja ambalo wewe ni mtaalamu wake,au moja ambalo umelitekeleza kwa umakini na weledi wa hali ya juu,kisha hili ndio liwe msingi wa kusonga mbele

8.Jipe motisha.Hakikisha unajimotisha wewe binafsi,tumia 80% ya muda wako kwenye mambo mazuri na 20% au pungufu kwenye matatizo,usiache matatizo yawe kansa kwako!

9.Usiwe mtumwa wa teknolojia. Teknolojia ni nzuri sana ila ifanye iwe mtumwa wako,wewe usiwe mtumwa wa teknolojia.Jifunze muda wa kufanya simu/laptop/tv etc na muda wa kufanya mengine(kuna watu wanaangalia TV anafuatilia tamthilia ya kifilipino hadi analala kwenye kiti)kila jambo lifanyike kwa kiasi,wengine simu hata akienda ibadani yupo busy na simu,huu ni utumwa,fanya ziwe vitendea kazi vyako na wewe uwe juu!

10. Tengeneza jedwali la Maksi.Hakikisha unakuwa na jedwali la maksi ili uzipe maksi kazi/malengo na jinsi ambavo umetekeleza kwa kila lengo na mpango wake.Hili jedwali litakusaidia kujua wapi una nguvu na wapi ni dhaifu,wapi uboreshe,wapi uongezee bidi……………..

Nawatakia nyote Baraka za Mwenyenzi Mungu mwaka huu 2021

Nanyaro EJ
Shukrani mkuu.

Nitafuata Paretto Principle 80/20
 
Shukrani mkuu.

Nitafuata Paretto Principle 80/20
Mkuu misasa

Ulitakiwa ufafanue hivi kwa faida ya wengi maana kutaja tu kwamba utatumia kanuni ya Pareto yenye uwwiano wa 80/20 ni ngumu kueleweka hatimaye wengi kuiga ulichochagiza.

Manufaa ya Kanuni ya Pareto
Kuna sababu ya vitendo ya kutumia Kanuni ya Pareto. Kwa urahisi, inaweza kukupa dirisha ndani ya nani wa kumzawadia au nini cha kurekebisha. Kwa mfano, ikiwa 20% ya dosari za kubuni kwenye gari zinaongoza kwa 80% ya ajali, unaweza kutambua na kurekebisha dosari hizo. Vivyo hivyo, ikiwa 20% ya wateja wako wanaendesha 80% ya mauzo yako, unaweza kutaka kuzingatia wateja hao na kuwazawadia kwa uaminifu wao. Kwa mantiki hii, Kanuni ya Pareto inakuwa mwongozo wa jinsi ya kutenga rasilimali kwa ufanisi.

Hasara za Kanuni ya Pareto
Wakati 80 / 20 ni kweli kwa uchunguzi wa Pareto, hiyo haimaanishi kuwa daima ni kweli. Kwa mfano, asilimia 30 ya wafanyakazi (au watumishi 30 kati ya 100) wanaweza tu kukamilisha asilimia 60 ya pato. Wafanyakazi waliobaki wanaweza kuwa sio wenye tija au wanaweza tu kukwama kwenye kazi. Hii inarudia zaidi kwamba Kanuni ya Pareto ni uchunguzi tu na sio lazima sheria.
 
Kwa jinsi Saikolojia ya Watanzania wengi ilivyoharibiwa na hali ngumu ya Kimaisha / Uchumi sidhani kama Ushauri wako huu utazingatiwa kivile.
 
Mkuu misasa

Ulitakiwa ufafanue hivi kwa faida ya wengi maana kutaja tu kwamba utatumia kanuni ya Pareto yenye uwwiano wa 80/20 ni ngumu kueleweka hatimaye wengi kuiga ulichochagiza.

Manufaa ya Kanuni ya Pareto
Kuna sababu ya vitendo ya kutumia Kanuni ya Pareto. Kwa urahisi, inaweza kukupa dirisha ndani ya nani wa kumzawadia au nini cha kurekebisha. Kwa mfano, ikiwa 20% ya dosari za kubuni kwenye gari zinaongoza kwa 80% ya ajali, unaweza kutambua na kurekebisha dosari hizo. Vivyo hivyo, ikiwa 20% ya wateja wako wanaendesha 80% ya mauzo yako, unaweza kutaka kuzingatia wateja hao na kuwazawadia kwa uaminifu wao. Kwa mantiki hii, Kanuni ya Pareto inakuwa mwongozo wa jinsi ya kutenga rasilimali kwa ufanisi.

Hasara za Kanuni ya Pareto
Wakati 80 / 20 ni kweli kwa uchunguzi wa Pareto, hiyo haimaanishi kuwa daima ni kweli. Kwa mfano, asilimia 30 ya wafanyakazi (au watumishi 30 kati ya 100) wanaweza tu kukamilisha asilimia 60 ya pato. Wafanyakazi waliobaki wanaweza kuwa sio wenye tija au wanaweza tu kukwama kwenye kazi. Hii inarudia zaidi kwamba Kanuni ya Pareto ni uchunguzi tu na sio lazima sheria.
Mkuu

Sawa naweza kutoa ufafanuzi wa kanuni 80/20 ya mchumi wa Pareto ila si uungwana kuweka UZI juu ya UZI.

Ila naahidi nitafanya hivyo siku nyingine mkuu.
 
Haya mawazo yako yamekaa kinadharia zaidi. Haijazinhatia uncertainties and fatalities, wakati maisha ni mnyororo wa uncertainties and fatalities.
 
Back
Top Bottom