Kiranga
Platinum Member
- Jan 29, 2009
- 71,264
- 105,428
Sawa.Mwambie alipe kodi. Yeye ni mbunge na ana kampuni ya sheria. Alikuwa mwanasheria wa kuiwakilisha BoT/serkali kwenye kesi nyingi za kimataifa na alikuwa analipwa mamillioni ya ya $$$, siyo shilingi bali $$$. Sasa akidaiwa kodi kuna kosa gani. Alitakiwa aklipe kodi na hakulipa. Kama anabambikiwa kodi si akate rufaa au aende mahakama ya kibiashara. Yeye ni msomi na anayajuwa haya. Wewe ulichokifanya ni kusema uongo eti kaonewa. Wabunge wanajuwa pa kwenda kama wameonewa...kwenye vyombo vya sheria.vyombo vya sheria. Kwa nini asiende huko!
Lamini oia, kwa Tanzania ya sasa kodi inaweza kutumika kama fimbo ya kisiasa.
Kodi inatakiwa kuwa wazi, inatakiwa ilipwe na wote na inatakiwa iwe sawa na uzalishaji.
Tanzania hayo yote hayazingatiwi.
Simtetei Mzee Mkono, nasema mapungufu ya kimfumo yanayozaa naswali kwa mtu yeyote mwenye kesi ya kodi.